Ilianza mwaka 2013 baada ya kutenganisha idara mama ya kilimo na mifugo.
Mkuu wa idara ni George S. Kessy , mwenye taaluma ya Afisa Ushirika akiwa ni Afisa Ushirika Mkuu Daraja la 1.
Idara ina jumla ya watumishi 59 .Kati yao, 2 ni maafisa ushirika, watumishi 4 ni maafisa kilimo (wenye shahada), waliobaki 53 ni maafisa kilimo wasaidizi (wenye stashahada na astashahada).
Halmshauri ya wilaya ya Kishapu ina jumla ya kata 29 zenye jumla ya vijiji 117. Kata zote 29 zimepangiwa wataalamu (maafisa kilimo wa kata) ikiwa ni mmoja kwa kila kata. Aidha ni vijiji 24 tu zenye wataalamu wa kilimo , kila kijiji mtaalamu mmoja. Vijiji vinavyobaki (93) havina wataalamu .
MAJUKUMU
-Kutoa elimu ya kilimo bora kwa wakulima ili kuwezesha wakulima kuongeza tija katika uzalishaji .
-Kusimamia miradi ya kilimo
-kutoa elimu ya hifadhi bora ya mazao ili kuzuia upotevu na hivyo kupunguza hasara inayotokana na upotevu na uharibifu wa mazao.
-Kutathimini visumbufu vya mazao na kutoa taarifa kwa taasisi zinazoshughulika na udhibiti wa visumbufu vya mazao.
-Kuratibu na kusaidia upatikanaji wa pembejeo (mbegu bora, mbolea na viuatilifu) kwa wakulima .
-Kushirikiana na jamii katika kuandaa miradi ya kilimo ambayo inatokana na hitaji la wakulima wenyewe.
-Kukusanya taarifa za hali ya hewa na kuziwasilisha kwa wakulima kwa ajili ya kujiandaa na kalenda ya kilimo msimu unaofuata.
-Kutoa ushauri kwa wakulima juu ya kilimo cha mazao yanayostahimili ukame kwa vile wastani wa mvua katika wilaya hii ni kati ya 450mm hadi 950mm kwa mwaka , wastani ambao ni kidogo sana na haufai kwa kulima mazao yanayohitaji maji mengi na muda mrefu kukomaa.
-Kueneza teknolojia mpya ya kilimo kama vile mbegu bora, mbegu kinzani na magonjwa na wadudu,kutumia zana au nyenzo bora za kilimo.
-Kuandaa na kutoa taarifa ya utekelezaji wa shughuli za kilimo kwa baraza la madiwani na kamati za kudumu za Halmashauri ya wilaya ya Kishapu.
-Kutoa mafunzo kwa wakulima kuhusu matumizi sahihi ya teknolojia mpya.
HUDUMA ZA JAMII.
-Kufanya tathimini ya hali ya chakula (usalama wa chakula)
-Kutoa elimu ya hifadhi na matumizi bora ya chakula kwa wakulima.
-Kutoa mafunzo kwa wakulima.
MATARAJIO
Idara inatarajia kuona wakulima wanaolima kitaalamu ,wanaotumia pembejeo na zana bora za kilimo katika kuzalisha na kuwa na kilimo cha kibiashara na uchumi wa viwanda (Agro-industries)
Halmashauri ya Wilaya Kishapu
Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU
Simu ya mezani: +255282770020
Simu:
Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz
Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa