Idara ya Fedha inasimamia ukusanyaji wa mapato na matumizi ya fedha katika Halmashauri na kutoa ushauri wa namna bora ya matumizi ya fedha.
Katika kusimamia huko inahakikisha kunakuwa na mfumo thabiti wa udhibiti wa ndani ambao pamoja na kuzingatia masuala ya kiutendaji pia unalenga katika kuangazia taratibu nzima za kifedha za Halmashauri.
Pia ina kazi ya kuwasilisha taratibu za kifedha kwenye kamati ya fedha kwa ajili ya mapitio kuhakikisha kunakuwa na udhibiti wa kutosha wa mali za Halmashauri pamoja na fedha, hii ikiwa ni kuwa na mpango kazi mzuri wa wafanyakazi na utawala ndani ya idara.
Shughuli
Kuandaa malipo yote
Kuandaa Bajeti ya matumizi ya kawaida,
Kuhakikisha uwepo wa nyaraka zote za malipo kabla na baada ya kulipa, kuhakikisha taratibu na sheria za kifedha zinatekelezwa,
Kuhakikisha kuwepo na majalada ya kumbukumbu kwa malipo yaliyolipwa,
Kufanya usaili wa kimahesabu kati ya benki na vitabu vya kumbukumbu vya halmashauri.
Kuandaa taarifa za fedha na kuziwasilisha sehemu husika kwa wakati.
Kuhakikisha inakusanya mapato yote ya halmashauri,
Kuhakikisha kuna udhibiti mzuri wa mapato ya Halmashauri,
Kupeleka fedha taslimu na hundi benki
Kuandaa ripoti mbalimbali na kuziwasilisha sehemu husika, (v)Kuweka utaratibu rahisi wa malipo ya fedha taslimu kwa wateja,
Kubuni vyanzo vipya vya mapato,
Kuandaa orodha ya watumishi kwa ajili ya kulipwa mishahara
Kutunza orodha ya watumishi wanaolipwa mishahara na kutunza kumbukumbu za makato yakatwayo watumishi kwenye mishahara yao
Kuandaa bajeti ya mishahara kwa watumishi
Kuandaa taarifa mbalimbali za mishahara na kupeleka sehemu husika
Kushughulikia matatizo yote ya mishahara inayotokea kwa watumishi
Halmashauri ya Wilaya Kishapu
Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU
Simu ya mezani: +255282770020
Simu:
Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz
Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa