Kitengo cha sheria cha Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu kina majukumu mbalimbali yakiwepo.
Kutoa ushauri kwa masuala yote ya kisheria kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya na kwa wakuu wote wa idara na vitengo pamoja na watumishi kwa ujumla.
Kuiwakilisha Halmashauri mahakamani katika mashauri yote yanayoihusu Halmashauri kwa maana ya kushtaki au kushtakiwa.
Kufanya mapitio ya uhalali wa mikataba kwa mujibu wa sheria na kuandaa mikataba mbalimbali inayoihusu Halmashauri au Taasisi zake.
Kuandaa sheria ndogo za halmashauri na sheria ndogo za vijiji vilivyoko ndani ya eneo la Halmashauri.
Kusimamia na kutoa mafunzo ya uendeshaji wa Mabaraza ya Kata.
Kuratibu na kusajili vyombo vya watumia maji wilayani Kishapu.
Halmashauri ya Wilaya Kishapu
Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU
Simu ya mezani: +255282770020
Simu:
Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz
Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa