• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
    • Idara
      • Fedha
      • Rasilimali watu
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii

Milioni 42.6 kutoka mfuko wa Jimbo kuendeleza ujenzi Madarasa na Maabara.

Posted on: January 17th, 2021

Mbunge wa Jimbo la Kishapu, Boniphace Nyangindu Butondo amewapongeza wananchi kwa nguvu kazi na michango ya fedha kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa na maabara Wilayani Kishapu.

Mhe. Butondo ameyasema hayo alipokuwa na ziara yake ya siku mbili Jimboni humo ambapo alizindua mfuko wa Jimbo na kutambulisha kikao cha kwanza kupitia mwenyekiti wa wa mfuko huo.

Kikao hicho kiliazimia kutoa fadha kwa ajili kuunga mkono miradi ya maendeleo iliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi hasa vyumba vya madarasa na maabara kwa lengo la kutekeleza agizo la Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Mjaliwa la kuongeza vyumba vya madarasa ili ifikapo Februari 2021 wanafunzi wapate mazigira mazuri ya kujisomea.

Katika ziara yake alitembelea tarafa za Mondo, Negezi na Kishapu ambapo jumla ya miradi ya maendeleo 15 imenufaika na mfuko huo wa Jimbo huku jumla ya kiasi cha fedha shilingi milioni 42.6 kilitolewa na Mbunge huyo kupitia mfuko wa jimbo kwa ajili ya kufanikisha miradi hiyo ukiwemo na mradi wa Ofisi ya Makao Makuu ya Polisi Wilaya ya Kishapu unaojengwa kwa nguvu za wananchi.

“Fedha hizi zitaenda kukamilisha ujenzi wa vyumba vya madarasa pamoja na maabara ulioanzishwa kwa nguvu za wananchi ikiwa ni kuunga mkono jitihada za serikali ya awamu ya tano ya elimu bure kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari” alisema Butondo.

Mhe. Butondo ameendelea kuwashukuru na kuwapongeza wananchi wa Jimbo la Kishapu kwa kuwachagua kwa kishindo katika uchaguzi mkuu iliopita wa Rais, wabunge na Madiwani na kuahidi kuwatumikia kwa nguvu zote.

“Wananchi wa Kishapu mliniamini mkanichagua ili tufanye maendeleo naomba tushirikiane ili kwa umoja wetu tuwezek uleta maendeleo katika Jimbo letu, naomba tuzidi kushikana mkono hasa katika mradi mkakati huu wa ujenzi wa vyumba vya madarasa na maabara ili watoto wetu wapate elimu kwenye mazingira rafiki” aliongeza Butondo.

Aidha Mbunge huyo aliwaasa viongozi wa ngazi zote kuanzia kata, vijiji na vitongoji kusoma taarifa za mapato na matumizi kwa wananchi wao kupitia vikao na mikutano ya hadhara kwani kufanya hivyo kutawajengea uaminigu kwa wananchi wao.

Katika ziara hiyo amesisitiza pia suala zima la usimamizi wa thamani ya fedha kutokana na utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuwataka wataalamu ngazi ya Halmashauri kusimamia ujenzi huo  ili uwe katika kiwango kinachitakiwa na kudumu kwa muda mrefu.

Matangazo

  • Tangazo la kazi kada ya Afya December 12, 2018
  • Majina ya walioitwa kwenye usaili nafasi ya watendaji May 10, 2018
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • OPE yafanya Tathimini juu ya Mimba na Ndoa za Utotoni

    February 04, 2021
  • Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango kukagua Miradi ya Maendeleo

    February 02, 2021
  • Milioni 34.4 kunufaisha Vikundi vya Ujasiriamali Kushapu

    January 18, 2021
  • Wanafunzi Waaswa Kusoma kwa Bidii Wakizingatia Uzalendo

    January 11, 2021
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu:

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa