Vyanzo vikuu vya maji kwa wananchi wa wilaya ya Kishapu ni visima vifupi, Virefu, mabwawa na miradi michache ya maji ya bomba. Mahitaji halisi ya maji kwa sasa ni mita za ujazo 15,303 kwa siku, lakini kiasi cha mita za ujazo 7,860.7.
Kwa kuzingatia lengo la Taifa la kuwafikishia wananchi wa vijiji asilimia 90 maji safi na salama ndani ya umbali wa mita 400 ya makazi yao ifikapo 2020, kwa sasa wakazi wa Wilaya ya Kishapu wananufaika na huduma hii kwa kiwango cha wasani wa asilimia 51.6% vijijini na asilimia 45% mjini.
TAKWIMU ZA MIUNDOMBINU YA MAJI
Halmashauri ya wilaya ya Kishapu kwa kushirikisha wadau wa Maendeleo, Serikali kuu na Wananchi wenyewe imeweza kupunguza tatizo la upatikanaji wa maji na Salama kama ifuatavyo:
Jedwali 58: Takwimu za Miundombinu ya maji
Mwaka |
Malambo/Mabwawa |
Visima |
Skimu ya Maji ya Bomba na windmill |
Matanki ya Maji ya Mvua |
% ya Wanufaika |
|
Virefu
|
Vifupi
|
|||||
2013/2014
|
20 |
8 |
245 |
14 |
118 |
49 |
2014/2015
|
23 |
10 |
248 |
17 |
120 |
50.2 |
2015/2016
|
26 |
12 |
251 |
19 |
125 |
51.3 |
2016/2017
|
28 |
12 |
258 |
20 |
129 |
51.4 |
2017/2018
|
29 |
12 |
263 |
21 |
135 |
51.6 |
Utekelezaji wa Programu ya Maji na Usafi wa Mazingira katika vijiji 10 ulianza kwa mchakato wa kupata Wataalam Washauri(Consultants) ambao walihusika katika kusaidia kusanifu miradi, kufanya utafiti wa maji ya ardhini na kusimamia kuchimba visima virefu na baadaye kuanza ujenzi wa miundombinu ya maji.
Programu ya maji vijijini awamu ya I ulijenga miradi ya maji katika baadhi ya vijiji kadri fedha ilivyokuwa ikipatikana. Vijiji vilivyopewa kipaumbele katika ujenzi wa miundombinu ya maji kupitia awamu ya kwanza ya utekelezaji wa Programu hii yaani (WSDPI) vilikuwa vijiji 9 ambavyo ni Nyenze, Iboja, Sekeididi, Mwigumbi, Mwamashimba, Bubinza, Mwamadulu, Idukilo na Bunambiyu. Jumla ya Tsh 3,471,700,912/= zimetumika kutekeleza miradi ya maji awamu ya kwanza kuanzia hatua ya usanifu mpaka ujenzi wa miundombinu ya Maji. Kwa pamoja Miradi hii inahudumia watu wapatao 24,750
Katika Mpango na Bajeti ya mwaka wa fedha 2017/2018 Halmshauri iliidhinishiwa kiasi cha Tsh. 1,597,855,000/= kwa ajili ya kutekeleza miradi ya Maji na Usafi wa Mazingira.
Hadi kufikia Mwezi Novemba 2017, Halmashauri imeshapokea jumla Tsh. 26,000,000/= ambazo ni kwa ajili ya usanifu, usimamizi na ufuatiliaji wa miradi.
Mhe, Naibu Waziri, utekelezaji wa programu ya sekta ya maji awamu ya pili (WSDP II), umeanza katika mwaka huu wa fedha 2017/2018 kwa kuhusisha jumla ya miradi 5 katika vijiji vya Shagihilu, Ndoleleji, Lagana, Ikonongo na Unyanyembe, wakandarasi wako eneo la kazi (site) wakiendelea na ujenzi ambao uko katika hatua mbalimbali za utekelezaji. Ujenzi huu utagharimu zaidi ya Tsh. 1,500,000,000/=.
Halmashauri ya Wilaya Kishapu
Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU
Simu ya mezani: +255282770020
Simu:
Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz
Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa