• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
    • Idara
      • Fedha
      • Rasilimali watu
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii

Ujenzi

Inaundwa na vitengo viwili saidizi yaani, kitengo cha barabara na majengo. Ilianza rasmi kutoa huduma zake kwa jamii wakati wa kuanzishwa kwake tarehe  01/07/2006 wakati huo ikiwa na watumishi wake watatu waliotwaliwa kutoka Halmashauri mama ya Shinyanga vijijini.Watumishi hawa walikuwa ni Eng. P.Malimi,mkuu wa idara,Leonard N.Machiya,fundi sanifu na msaidizi pekee na Mikael N.Mpanduji,dereva (Marehemu).

Waajiriwa wengine wapya wa kwanza mwaka huo 2006 walikuwa ni Eng. Leonard B.L.Mashamba (Marehemu), aliye kuwa mkuu wa idara baada ya kuacha kazi kwa kustaafu kwenye utumishi wa umma kwa aliyekuwepo wakati huo ndugu P.Malimi na ndugu Richard Kachwele (Fundi sanifu uhandisi wa ujenzi),pamoja na ndugu Maduhu V.Fundi (Fundi sanifu uhandisi wa ujenzi) ambaye baadaye mwaka 2013 alihamia Halmashauri ya wilaya ya Meatu.

 

Kwa sasa idara ya ujenzi ya wilaya ya kishapu imekua na kuwa kubwa yenye watumishi wapatao wanane (08). Idara inavyo vitengo vikuu viwili tofauti , yaani kitengo cha barabara na majengo. Pamoja na vitengo hivi,idara husimamia na kuratibu pia shughuli za uendeshaji na usimamizi wa mitambo na magari yanayomilikiwa chini ya  mamlaka za Serikali za mitaa ambayo ni mali  ya Halmashauri ya wilaya ya Kishapu.

        II.    TAARIFA ZA WATUMISHI NA WASIFU WAO KITAALUMA

 

Idara ya ujenzi ya wilaya ya Kishapu sasa ina Wahandisi na Mafundi sanifu wenye sifa na walio fuzu vyema ambao ni  wachapakazi wenye bidii na nguvu ,wenye historia,uwezo majukumu na elimu mbalimbali. Idara inao wahandisi wanne (04) waliosajiriwa kwenye  Mamlaka ya bodi  ya Wahandisi (ERB);ambao ni Eng. Samson Pamphili (P.E), B.SC-CIVIL-UDSM( Mhandisi wa Wilaya na mkuu wa idara), Eng.Chiyando M.Matoke (G.E),B.E-CIVIL, D.I.T-DAR; (Mkuu wa kitengo cha barabara), Eng.Gemmastella Issack (G.E), B.E-CIVIL, MIST-MBEYA; (Mkuu wa kitengo cha majengo) na Eng.Richard Kachwele  (G.E),B.E-CIVIL,D.I.T/STJUIT-DAR. 

Sambamba  na hawa wapo pia mafundi sanifu walio fuzu vyema, wenye elimu na ujuzi mzuri pamoja na uzoefu wa kitaalam. Hawa ni  Leonard N.Machiya (Fundi sanifu mkuu,uhandisi wa ujenzi), CDTE-MISUNGWI, MWANZA; Victoria Pamba (Fundi sanifu uhandisi wa ujenzi), CDTE-MISUNGWI, MWANZA; Godson B. Katuba (Fundi sanifu uhandisi wa ujenzi), CDTE-MISUNGWI, MWANZA; and Paul S. Maganga (Fundi sanifu uhandisi wa mitambo na magari).A.T.C-ARUSHA.

III.0    WAJIBU NA MAJUKUMU YA UWAJIBIKAJI WA IDARA YA UJENZI NA VITENGO VYAKE

Idara  ya ujenzi ya umma ya wilaya ya kishapu  pamoja na vitengo vyake ina wajibika katika majukumu ikiwa na malengo ya kutoa huduma zake za jamii kwa ajili ya kuinua maendeleo ya kiuchumi wa jamii katika wilaya kama ilivyo kusudiwa katika kuanzishwa kwake

  • Idara kupitia kitengo cha barabara ina wajibu kusimamia na kuhakikisha kuwa barabara zote katika ngazi ya mjini na vijijini zinapitika kwa mwaka mzima.
  • Idara ina wajibika kupitia kitengo cha barabara ikishirikiana na wadau wengine kubaini,kuandaa,kutathmini na kuchanganua mahitaji ya matengenezo ya mabarabara mapya na miundo mbinu mingine kama madaraja ya chini,madaraja makubwa, mabawa n.k.na kuziwasilisha kwenye mamlaka za juu kwa hatua zaidi.
  • Idara kupitia kitengo cha barabara ina wajibu wa kutayarisha bajeti za  mwaka za matengenezo ya barabara katika wilaya kwa mwaka wa fedha mwingine na kuziwasilisha wizarani.
  • Idara kupitia kitengo cha barabara inawajibu wa kuandaa nyaraka za mikataba za matengenezo ya barabara za wilaya. 
  • Idara kupitia kitengo cha barabara ina wajibu wa  kushirikisha,kuhusianisha na kuwa unga mkono wadau wengine,wafadhili ndani na nje ya wilaya katika masuala ya ushauri wa shughuli za ujenzi,usimamizi na matengenezo.
  • Idara kupitia kitengo cha barabara inao wajibu wa kuandaa usanifu wa awali na wa  kina wa mabarabara mapya na miundo mbinu mingine kwa utekelezaji zaidi katika wilaya
  • Idara kupitia kitengo cha majengo ikishirikiana na wadau wengine ina wajibu wa kukagua,kutathmini na kuchanganua kwa ajili ya matengenezo mapya na ukarabati wa majengo ya serikali na kuwasilisha taarifa kwa mamlaka za juu kwa ajili ya utekelezaji zaidi.
  • Idara kupitia kitengo cha majengo inahakikisha kuwa majengo na miundo mbinu nyinginezo za serikali ambazo zimejengwa kwa njia ya mikataba zinakidhi ubora kwa kuonyesha  uwepo wa thamani ya pesa zilizotumika kwakuwa na usimamizi na utoaji wa  ushauri wa kitaalam ulio makini.
  • Idara inawajibika kutoa huduma za ushauri wa kitaalam kwa wananchi waliopo wilayani zinazohusiana na majenzi.
  • Idara inao wajibu kuandaa,kutathmini,kuchanganua na kutunza kumbukumbu za mikataba kwa ajili ya ukaguzi.
  • Idara ina wajibu wa kufanya usanifu,kuandaa michoro na miongozo ya bajeti za majenzi (B.O.Q) zitakazohitajika kwa kwa ajili ya zabuni.
  • Idara huwajibika kuandaa bajeti za matengenezo ya majenzi mapya ya serikali na ukarabati wake kwa mwaka na kuziwasilisha wizarani kwa idhini.
  • Idara inao wajibu wa kuandaa taarifa za mwezi,robo na mwaka za miundombinu ya  barabara,majengo na zisizo majengo za mara kwa mara  kwa ajili ya kuwasilishwa kwenye mabaraza ya kamati za halmashauri au mamlaka ya juu zaidi kwa  manufaa ya utawala bora.

IV.0    MATARAJIO YA IDARA YA UJENZI YA WILAYA YA KISHAPU

  •  
  • Idara ya ujenzi ya wilaya ya kishapu imedhamiria kufikia kiwango cha juu cha ufanisi wake katika utekelezaji na utoaji wa huduma zake zinazohusu ujenzi kwa jamii ndani ya wilaya ili kuwawezesha wananchi wajinusuru tokana na  miundombinu hizi kutoka kwenye lindi la umaskini.Kutokana na hili,idara imejiwekea mikakati ili kufikia kiwango hicho,baadhi ya mikakati hiyo imeorodheshwa hapa chini
  • Kutenda,kudumisha umoja na ushirikiano miongoni mwa wadau ndani ya idara mambo ambayo ni ya mhimu ili kuyafikia mahitaji ya watu na maendeleo yao kwa kufanya kazi bega kwa bega ili kufikisha huduma za kijamii karibu nao kama zilivyo lengwa na uongozi wa halmashauri ya wilaya ya Kishapu.
  • Kusimamia kazi zote za majenzi ya barabara,majengo na madaraja kwa kiwango kikubwa kwa kuhakikisha uwepo wa thamani ya pesa zilizotumika.
  • Kutoa huduma nzuri na bora za ushauri wa kitaalam kwa kazi zote za barabara na majengo ili kupunguza umaskini kwa jamii na hivyo kuendana na dhamira ya taifa kwa kutumia maarifa na ujuzi wote kwa wana idara.
  •  Kutekeleza majukumu kwa mjibu wa kanuni,sheria na maadili ili kifikisha idara pa hali pazuri.
  • Kushirikiana kikamilifu na wadau wote katika masuala yanayohusu huduma za ujenzi na utunzaji wa miundombinu ili kupunguza umaskini kwa kuwaelimisha mara inapotengenezwa kwenye maeneo yao mahalia.
  • Kuiwezesha idara ya ujenzi ya wilaya ya kishapu kupata ushindi kwenye ngazi za mkoa na taifa katika medani za utoaji wa huduma nzuri ,bora na zinazoendana na thamani ya pesa kwa jamii..

Matangazo

  • Tangazo la kazi kada ya Afya December 12, 2018
  • Majina ya walioitwa kwenye usaili nafasi ya watendaji May 10, 2018
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • Wanafunzi Waaswa Kusoma kwa Bidii Wakizingatia Uzalendo

    January 11, 2021
  • Wachimbaji wadogo wa madini waliovamia eneo la Mgodi wa Al-Hilal watakiwa kuondoka.

    January 21, 2021
  • Milioni 42.6 kutoka mfuko wa Jimbo kuendeleza ujenzi Madarasa na Maabara.

    January 17, 2021
  • Ziara ya Mkuu wa Wilaya ya Kishapu kukagua mradi mkakati wa ujenzi wa vyumba vya madarasa.

    January 13, 2021
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu:

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa