• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Utawala
      • Biashara, Viwanda na Uwekezaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya jamii
      • Afya
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Tehama
      • Utamaduni, Sanaa na Michezo
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Usafi wa Mazingira na Udhibiti Taka
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Kilimo na Mifugo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya kuonana na mwenyekiti wa Halmashauri
    • Ratiba ya vikao vya kisheria vya MSM
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Sheria ndogo ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya picha na video za shughuli za maendeleo

BARAZA LA MADIWANI KISHAPU LAAZIMIA SOKO HURIA LA PAMBA, LATOA MSISITIZO WA LISHE NA BIMA YA AFYA KWA WOTE

Posted on: January 28th, 2026

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga Mhe. Josephat Limbe akizungumza kwenye Baraza la Madiwani, likilenga kujadili Taarifa za Robo ya Pili wa mwaka wa fedha 2025/2026 (Oktoba-Disemba) katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri.

Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga limefanya mkutano wa kujadili taarifa za Robo ya Pili ya mwaka wa fedha 2025/2026 (Oktoba-Disemba), Januari 28, 2026 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, ambapo Waheshimiwa Madiwani wamepata nafasi ya kujadili mada mbalimbali za maendeleo sambamba na kupokea taarifa za kamati za kudumu.

Akizungumza katika Baraza la Madiwani, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Mhe. Josephat Limbe, amesema Baraza haliridhishwi na mfumo wa mnunuzi mmoja wa zao la pamba, hivyo limeazimia uwepo wa soko huria ili wakulima wanufaike zaidi na zao lao. Amebainisha kuwa mfumo wa mnunuzi mmoja umekuwa ukilalamikiwa na wakulima kutokana na changamoto za bei ndogo na kukosa ushindani, hali inayowanyima fursa ya kupata thamani halisi ya mazao yao. Kupitia soko huria, wakulimawatapata uhuru wa kuchagua wanunuzi, kuongeza ushindani na hatimaye kuinua kipato cha wananchi.

Mbunge wa Jimbo la Kishapu, Mhe. Lucy Thomas Mayenga, amewapongeza Waheshimiwa Madiwani kwa mjadala mpana na wenye tija kuhusu masuala ya maendeleo na ameahidi kufuatilia kwa karibu ili kuhakikisha suala la pamba linapatiwa ufumbuzi wa kudumu. Aidha, amesisitiza kuwa Baraza la Madiwani lina nafasi muhimu katika kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuhakikisha changamoto zinazowakabili wananchi zinapatiwa ufumbuzi kupitia ushirikiano wa karibu kati ya madiwani, wataalamu wa Halmashauri na Serikali Kuu.

Mbunge wa Jimbo la Kishapu mkoani Shinyanga Mhe. Lucy Mayenga akizungumza kwenye Baraza la Madiwani, likilenga kujadili Taarifa za Robo ya Pili wa mwaka wa fedha 2025/2026 (Oktoba-Disemba) katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Mhe. Peter Masindi, amesisitiza umuhimu wa kuimarisha masuala ya lishe mashuleni akieleza kuwa lishe bora ni msingi wa maendeleo ya elimu, afya na ustawi wa watoto. Vilevile, amehimiza utekelezaji wa mpango wa Bima ya Afya kwa Wote, akiwataka madiwani kuchukulia kwa uzito suala hilo na kuhamasisha wananchi kujiunga, akibainisha kuwa jukumu hilo ni la kila kiongozi na mshiriki wa mkutano huo.

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga Mhe. Peter Masindi akizungumza kwenye Baraza la Madiwani, likilenga kujadili Taarifa za Robo ya Pili wa mwaka wa fedha 2025/2026 (Oktoba-Disemba) katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) katika Wilaya ya Kishapu, Shija Ntelezu ameweka mkazo kwenye hoja ya lishe na kuwataka madiwani kuhakikisha mpango uliowekwa unatekelezwa kwa vitendo, huku Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo Wilayani humo, akilipongeza Baraza kwa jinsi lilivyoongozwa na kusisitiza kuwa kiu ya maendeleo ya Kishapu ni ya kila mtu bila kujali chama, jambo linalodhihirisha ushirikiano wa kisiasa kwa maslahi ya wananchi.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) katika Wilaya ya Kishapu, Shija Ntelezu na Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo Wilayani humo wakizungumza kwenye Baraza la Madiwani, likilenga kujadili Taarifa za Robo ya Pili wa mwaka wa fedha 2025/2026 (Oktoba-Disemba) katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri.

Katika mkutano huo, kamati za kudumu zilizowasilisha taarifa zake ni pamoja na Kamati ya Kudhibiti UKIMWI, Kamati ya Huduma za Jamii, Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira pamoja na Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango. 

Wenyeviti na wawakilishi wa kamati za kudumu wakiwasilisha Taarifa za Robo ya Pili wa mwaka wa fedha 2025/2026 (Oktoba-Disemba) katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri.

Mkutano umehitimishwa kwa wito wa madiwani na wataalamu kuibua vyanzo vipya vya mapato, kuimarisha ukusanyaji wa mapato na kuendeleza ushirikiano kati ya viongozi, wataalamu na wananchi ili kupelekea kasi ya maendeleo katika Wilaya ya Kishapu.



Matangazo

  • TANGAZO LA MWALIKO WA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI January 20, 2026
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI December 22, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI November 21, 2025
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • VIKUNDI 21 MAKUNDI MAALUMU VYAPATIWA MIKOPO KISHAPU

    January 29, 2026
  • BARAZA LA MADIWANI KISHAPU LAAZIMIA SOKO HURIA LA PAMBA, LATOA MSISITIZO WA LISHE NA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    January 28, 2026
  • DED KISHAPU AKABIDHI VIFAA VYA TEHAMA KUWAWEZESHA WAALIMU WENYE CHANGAMOTO YA UONI

    January 28, 2026
  • BARAZA LA MADIWANI KISHAPU LAPOKEA NA KUJADILI TAARIFA ZA KATA ROBO YA PILI 2025/2026

    January 27, 2026
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa