• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
    • Idara
      • Fedha
      • Rasilimali watu
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
  • Nyaraka
    • Fomu za kujinga na Kidato cha Tano
      • Shule ya Sekondari Kishapu
      • Shule ya Sekondari Shinyanga
    • Mpango wa bajeti wa mwaka 2021/2022
    • Matangazo
    • Sheria ndogo ya ushuru wa huduma
    • Mifumo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
      • Uvuvi wa Samaki katika Bwawa la Songwa, Bwawa mhumbu
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Mhe. William Luhende Jijimya - Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Mhe. Francis Manyanda - Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Mhe. Joel Ndettoson - Diwani kata ya Kishapu
      • Mhe. Mohamed Aman - Diwani kata ya Ndoleleji
      • Mhe. Lucas Nkende - Diwani kata ya Mwamashele
      • Mhe. Pontias Daud - Diwani kata ya Mwataga
      • Mhe. James Kasomi - Diwani kata ya Bubiki
      • Mhe. Bushi Mpina - Diwani kata ya Mwamalasa
      • Mhe. Nyama Kisinza - Diwani kata ya Somagedi
      • Mhe. Mashini W. Washima - Diwani kata ya Uchunga
      • Mhe. Anderson Mandia - Diwani kata ya Ukenyenge
      • Mhe. Edward Manyama - Diwani kata ya Kiloleli
      • Mhe. Reuben Siyabo - Diwani kata ya Bupigi
      • Mhe. Bujiku Nyanda - Diwani kata ya Mwaweja
      • Mhe. Michael Paul - Diwani kata ya Shagihilu
      • Mhe. Luhende S. Luhende - Diwani kata ya Lagana
      • Mhe. Richard Dominico - Diwani kata ya Talaga
      • Mhe. James Kamuga - Diwani kata ya Igaga
      • Mhe. Lameck Nsubata - Diwani kata ya Itilima
      • Mhe. Mpemba Malangahe - Diwani kata ya Bunambiyu
      • Mhe. Makenzi Charles - Diwani kata ya Busangwa
      • Mhe. Nestory Kalugula - Diwani kata ya Ngofila
      • Mhe. Lwinzi Kidiga - Diwani kata ya Maganzo
      • Mhe. Samson Gelewa - Diwani kata ya Mwasubi
      • Mhe. Sarah Marco - Diwani kata ya Idukilo
      • Mhe. Enock Bundala - Diwani kata ya Masanga
      • Mhe. Thabidha Mmbando - Diwani kata ya Mwakipoya
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Mwenyekiti wa Halmashauri
  • miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
  • Kituo Cha Habari
    • maktaba ya picha
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa za Vyombo vya Habari
  • Maeneo
    • Kata
      • Orodha ya Kata
    • Tarafa
      • Orodha ya Tarafa
    • Vijiji
      • Orodha ya Vijiji

LISHE BORA YAPAA SHULENI KISHAPU

Posted on: July 16th, 2025

Msimamo wa Wilaya ya Kishapu kuhusu umuhimu wa lishe Shuleni umeendelea kuimarika, huku viongozi wakihimiza usimamizi madhubuti wa afua za lishe kama silaha ya kupambana na utoro na kuongeza ufaulu kwa wanafunzi wa Shule za Msingi na Sekondari.

Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Bw. Tano John Malele, ambaye pia ni Mwakilishi wa Mwenyekiti wa Kamati ya Lishe ya Wilaya hiyo amesema wakati wa kikao cha tathmini ya utekelezaji wa afua za lishe kilichofanyika Julai 16, 2025 Katika ukumbi wa Halmashauri ya Kishapu amesema lishe si jambo la hiari bali ni msingi wa maendeleo ya elimu.

“Serikali ya awamu ya sita imetoa kipaumbele kwa watoto kupata chakula mashuleni. Hatutarajii kuona shule yoyote haina uji au chakula cha mchana kwa wanafunzi wa sekondari katika robo ijayo,” ameisitiza  Malele mbele ya wajumbe wa kikao hicho.

                                                                                                 Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Tano Malele akizungumza.

Katika hotuba yake, Bw. Malele amewakumbusha Watendaji wa Kata na Vijiji kuwa wao ni kielelezo kwa jamii, hivyo ni muhimu wakajitokeza mbele kwa kuhamasisha wananchi kuchangia chakula cha wanafunzi huku wakianza wao kutoa.

Amewataka wasimamizi wa chakula shuleni kuwa waaminifu katika utekelezaji wa majukumu yao kama sehemu ya kuthamini juhudi za serikali na wananchi.

Mtendaji wa Kata ya Mwamashele ametunukiwa zawadi ya fedha taslimu kutokana na utekelezaji mzuri wa afua za lishe, pamoja na mwandishi wa vikao na mtumishi kutoka shirika la World Vision kwa mchango wao muhimu.

Afisa Maendeleo ya Jamii wa Wilaya ya Kishapu, Bw. Joseph Swalala, amewahimiza watendaji kuendelea kutoa elimu kuhusu lishe bora katika ngazi ya jamii akisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya watendaji, jamii na wadau wa maendeleo kama nguzo ya mafanikio ya afua za lishe.

                                                                                                                    Afisa maendeleo Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga Joseph Swalala

Naye Afisa Lishe wa Wilaya, Bi. Hadija Ahmed Nchakwi, ameeleza kuwa jitihada za serikali zimeanza kuzaa matunda hasa katika kupunguza viwango vya udumavu kwa watoto walio na umri chini ya miaka mitano pamoja na wajawazito.

“Jamii imeanza kuelewa umuhimu wa lishe. Hata wajawazito wanaokuja kliniki, hali zao zinaonyesha mabadiliko chanya. Changamoto kubwa iliyobaki ni kuhakikisha kila shule inatekeleza kikamilifu mpango wa lishe,” amesema Bi. Nchakwi.

                                                                                                                               Afisa lishe Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga Hdija Nchakwi

Kwa mujibu wa taarifa za kikao hicho, Wilaya ya Kishapu ina jumla ya shule 168 za msingi na sekondari. Katika robo ya tatu, shule 152 (sawa na asilimia 90.5%) zilikuwa zinatoa chakula kwa wanafunzi, na robo ya nne idadi hiyo ilipanda hadi asilimia 97.62%.

Jumla ya taarifa tisa zimewasilishwa kutoka Idara mbalimbali ikiwemo Afya, Elimu Awali na Msingi, Elimu Sekondari, Kilimo,Mifugo na Uvuvi,Maendeleo ya Jamii, RUWASA, na Redeso, pamoja na wawakilishi wa madhehebu ya Kiislamu.

Taarifa hizo zimeeleza hatua zilizopigwa na mapendekezo ya kuimarisha zaidi utekelezaji wa afua za lishe.

Kikao hicho kimedhihirisha kuwa mafanikio katika elimu hayategemei tu vitabu na walimu, bali pia hali ya lishe ya wanafunzi. Hivyo, kuweka mkazo katika lishe bora si tu kuongeza ufaulu, bali pia ni hatua muhimu ya kulinda afya, kupunguza udumavu katika jamii.

Matangazo

  • TAARIFA YA MTIRIRIKO WA FEDHA KWA KIPINDI KILICHOISHIA TAREHE 30 JUNE. 2022 August 14, 2023
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI November 03, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MFAMASIA December 14, 2021
  • Orodha ya Walioitwa kwenye Usaili September 20, 2024
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • LISHE BORA YAPAA SHULENI KISHAPU

    July 16, 2025
  • DC KISHAPU AWATAKA WANANCHI KUTUMIA KWA TIJA MBEGU ZILIZOBARIKIWA BUSIYA

    July 08, 2025
  • KISHAPU YAGAWA CHANJO 300,000 YA KUKU WA KIENYEJI

    July 01, 2025
  • VIJIJI 16 VINAVYOZUNGUKA MIGODI KISHAPU MIGOGORO YA ARDHI KUKOMESHWA

    June 27, 2025
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa