• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Utawala
      • Biashara, Viwanda na Uwekezaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya jamii
      • Afya
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Tehama
      • Utamaduni, Sanaa na Michezo
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Usafi wa Mazingira na Udhibiti Taka
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Kilimo na Mifugo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya kuonana na mwenyekiti wa Halmashauri
    • Ratiba ya vikao vya kisheria vya MSM
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Sheria ndogo ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya picha na video za shughuli za maendeleo

MAAFISA UGANI NA WADAU WA PAMBA KUHAKIKISHA WANAONGEZA TIJA KATIKA ZAO LA PAMBA

Posted on: March 11th, 2025

Maafisa Ugani na Wadau wa zao la pamba  wametakiwa kushiriki kikamilifu katika kuhakikisha wanaongeza uzalishaji na tija kwenye zao la pamba kwa kutoa michango mbalimbali kwasababu wao ni wadau muhimu katika maendeleo ya zao hilo na si wakulima pekee.

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Peter Masindi ameyesema hayo leo Machi 11, 2025 wakati wa kikao cha Maafisa Ugani, watendaji wa Vijiji, AMCOS pamoja na Wadau wa Zao la Pamba kilichofanyika katika Ukumbi wa SHIRECU kwaajili ya  kutathmini Maendeleo ya Zao la Pamba kwa Wakulima

Akizungumza na Wadau wa Pamba,  AMCOS, Bodi ya Pamba, Maafisa Ugani, Watendaji wa Kijiji na Vijana wa BBT amewataka kushirikiana kwa pamoja katika kuhakikisha wanakuwa kitu kimoja wanapokutana na changamoto, kero na matatizo katika kipindi hiki ili iwe rahisi katika Kumsaidia Mkulima na kuhakikisha Pamba inapatikana kwa Wingi ili kufikia Malengo yaliyokusudiwa katika uzalishaji wa zao la Pamba

"Mnapotoka hapa mhakikishe mnaenda kukaa pamoja Afisa Ugani, Bodi ya Pamba, Mtu wa BBT, Afisa Ushirika, Mtendaji wa kata mkatafute Solution mnafanyaje ili  kufanikisha uzalishaji wa Pamba Mwezi wa Tano, Binadamu ameumbwa kutatua Changamoto za Watu wengine, hamna Binadamu aliyeumbwa kusababisha matatizo ya Watu hivyo mkawe kitu kimoja katika kutatua Changamoto za Wakulima Kwa kushirikia Pamoja" alisema Masindi

Aidha kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kishapu Mwl Sigthbeth Rwezahula amewataka Maafisa Ugani pamoja na Wadau wa Pamba kushirikiana kwa pamoja ndiyo kuleta Tija katika uzalishaji wa Zao la Pamba 2025 na Miaka ijayo



Aidha DC Masindi amepiga Marufuku Maafisa Ugani kujihusisha na Shughuli zingine tofauti na Kilimo, Shughuli ambazo zinapelekea  kushindwa kuwahudumia Wakulima wa Zao la Pamba ipasavyo


Pia amewataka wataalamu wa kilimo Wilayani Kishapu  kuendelea kutoa Elimu kwa wakulima wa zao la pamba kuzingatia taratibu za kilimo cha zao hilo ili kuongeza tija na uzalishaji na kuacha kilimo cha mazoea.


Hata na Hivyo Wakulima Wameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Dkt, Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwajali katika kilimo cha Pamba licha ya Changamoto ndogondogo kama vile Sumu kwaajili ya kupulizia wadudu kutokufika kwa Wakati.

Matangazo

  • TANGAZO LA MWALIKO WA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI January 20, 2026
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI December 22, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI November 21, 2025
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • KISHAPU YAJIPANGA KUONGEZA UZALISHAJI PAMBA

    February 04, 2026
  • BARAZA LA WAFANYAKAZI KISHAPU LAPITISHA MWELEKEO MPYA MASLAHI YA WATUMISHI

    February 03, 2026
  • VIKUNDI 21 MAKUNDI MAALUMU VYAPATIWA MIKOPO KISHAPU

    January 29, 2026
  • BARAZA LA MADIWANI KISHAPU LAAZIMIA SOKO HURIA LA PAMBA, LATOA MSISITIZO WA LISHE NA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    January 28, 2026
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa