• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
    • Idara
      • Fedha
      • Rasilimali watu
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
  • Nyaraka
    • Fomu za kujinga na Kidato cha Tano
      • Shule ya Sekondari Kishapu
      • Shule ya Sekondari Shinyanga
    • Mpango wa bajeti wa mwaka 2021/2022
    • Matangazo
    • Sheria ndogo ya ushuru wa huduma
    • Mifumo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
      • Uvuvi wa Samaki katika Bwawa la Songwa, Bwawa mhumbu
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Mhe. William Luhende Jijimya - Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Mhe. Francis Manyanda - Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Mhe. Joel Ndettoson - Diwani kata ya Kishapu
      • Mhe. Mohamed Aman - Diwani kata ya Ndoleleji
      • Mhe. Lucas Nkende - Diwani kata ya Mwamashele
      • Mhe. Pontias Daud - Diwani kata ya Mwataga
      • Mhe. James Kasomi - Diwani kata ya Bubiki
      • Mhe. Bushi Mpina - Diwani kata ya Mwamalasa
      • Mhe. Nyama Kisinza - Diwani kata ya Somagedi
      • Mhe. Mashini W. Washima - Diwani kata ya Uchunga
      • Mhe. Anderson Mandia - Diwani kata ya Ukenyenge
      • Mhe. Edward Manyama - Diwani kata ya Kiloleli
      • Mhe. Reuben Siyabo - Diwani kata ya Bupigi
      • Mhe. Bujiku Nyanda - Diwani kata ya Mwaweja
      • Mhe. Michael Paul - Diwani kata ya Shagihilu
      • Mhe. Luhende S. Luhende - Diwani kata ya Lagana
      • Mhe. Richard Dominico - Diwani kata ya Talaga
      • Mhe. James Kamuga - Diwani kata ya Igaga
      • Mhe. Lameck Nsubata - Diwani kata ya Itilima
      • Mhe. Mpemba Malangahe - Diwani kata ya Bunambiyu
      • Mhe. Makenzi Charles - Diwani kata ya Busangwa
      • Mhe. Nestory Kalugula - Diwani kata ya Ngofila
      • Mhe. Lwinzi Kidiga - Diwani kata ya Maganzo
      • Mhe. Samson Gelewa - Diwani kata ya Mwasubi
      • Mhe. Sarah Marco - Diwani kata ya Idukilo
      • Mhe. Enock Bundala - Diwani kata ya Masanga
      • Mhe. Thabidha Mmbando - Diwani kata ya Mwakipoya
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Mwenyekiti wa Halmashauri
  • miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
  • Kituo Cha Habari
    • maktaba ya picha
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa za Vyombo vya Habari
  • Maeneo
    • Kata
      • Orodha ya Kata
    • Tarafa
      • Orodha ya Tarafa
    • Vijiji
      • Orodha ya Vijiji

MBUNGE BUTONDO ATOA VIFAA VYA TEHAMA KUUNGA MKONO SEKTA YA ELIMU KISHAPU

Posted on: May 26th, 2025

Mbunge wa Jimbo la Kishapu, Mheshimiwa Boniphace Butondo, ameendelea kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita katika kuboresha sekta ya elimu nchini kwa kukabidhi vifaa vya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika shule za sekondari Ngofila na Lagana.

Zoezi hilo limefanyika jana katika shule hizo kwa nyakati tofauti, ambapo Mbunge Butondo aliambatana na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kishapu, Shija Ntelezu.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Mheshimiwa Butondo alisema lengo la msaada huo ni kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuinua kiwango cha elimu kwa kuwezesha wanafunzi kujifunza kwa vitendo na kuongeza ufaulu.

“Vifaa vya TEHAMA nilivyokabidhi ni pamoja na printer, seti kamili ya monitá, CPU na projector. Vifaa hivi vitasaidia kuinua taaluma ya wanafunzi na kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia,” alisema Butondo.

Aliongeza kuwa vifaa hivyo vitarahisisha kazi kwa walimu katika maandalizi ya masomo na uchapaji wa mitihani, hivyo kuondoa utegemezi kwa vituo binafsi vya uchapaji na kupunguza gharama za uendeshaji.

Mbunge huyo pia alitoa maelekezo kuwa vifaa hivyo vitunzwe kwa umakini, mazingira ya matumizi yawe safi, na kusisitiza uanzishwaji wa somo la Kompyuta katika shule ya sekondari Lagana ambayo kwa sasa haina somo hilo.

Mkuu wa Shule ya Sekondari Ngofila, Bi. Matrida Mwaliaje, alieleza kuwa upatikanaji wa vifaa hivyo ni chachu ya kuongeza ufaulu, kwani sasa wanafunzi watakuwa wanapatiwa majaribio mara kwa mara ili kutathmini maendeleo yao ya kitaaluma.

Amesema vifaa hivyo pia vitapunguza gharama na adha ya kusafiri umbali mrefu hadi shule za Kishapu na Ukenyenge, zilizoko zaidi ya kilomita 60, kwa ajili ya kuchapisha mitihani.

Kwa upande wake, Mkuu wa Shule ya Sekondari Lagana, Bw. Adam Malongo, alishukuru kwa msaada huo akisema ni mchango mkubwa katika kuinua viwango vya elimu shuleni hapo.

Baadhi ya wanafunzi, wakiwemo Hadija Pambe, walionesha furaha yao kwa kupatiwa vifaa hivyo, wakisema vitawawezesha kusoma kwa vitendo na kufanya majaribio ya mitihani mara kwa mara.

Naye Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kishapu, Bw. Shija Ntelezu, alitoa pongezi kwa Mbunge Butondo kwa kuendelea kutekeleza kwa vitendo Ilani ya Chama Cha Mapinduzi, hasa katika sekta ya elimu.

Hadi sasa, Mbunge Butondo ameshakabidhi vifaa vya TEHAMA katika shule tatu za sekondari jimboni humo, ambazo ni Kishapu, Ngofila na Lagana.

Matangazo

  • TAARIFA YA MTIRIRIKO WA FEDHA KWA KIPINDI KILICHOISHIA TAREHE 30 JUNE. 2022 August 14, 2023
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI November 03, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MFAMASIA December 14, 2021
  • Orodha ya Walioitwa kwenye Usaili September 20, 2024
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • DC MASINDI ATAKA WAUGUZI KISHAPU WAFANYE KAZI KWA NIDHAMU NA UPENDO

    May 31, 2025
  • REDESO NA CARE INTERNATIONAL WAWEZESHA WAKULIMA WADOGO KISHAPU KUPITIA MRADI WA UFUGAJI WA KUKU NA ZAO LA MKONGE

    May 30, 2025
  • MBUNGE BUTONDO ATOA VIFAA VYA TEHAMA KUUNGA MKONO SEKTA YA ELIMU KISHAPU

    May 26, 2025
  • CPA. MAKALA AIPONGEZA SERIKALI MAENDELEO KISHAPU – BUTONDO AOMBA DED ASIONDOLEWE

    May 23, 2025
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa