• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
    • Idara
      • Fedha
      • Rasilimali watu
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
  • Nyaraka
    • Fomu za kujinga na Kidato cha Tano
      • Shule ya Sekondari Kishapu
      • Shule ya Sekondari Shinyanga
    • Mpango wa bajeti wa mwaka 2021/2022
    • Matangazo
    • Sheria ndogo ya ushuru wa huduma
    • Mifumo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
      • Uvuvi wa Samaki katika Bwawa la Songwa, Bwawa mhumbu
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Mhe. William Luhende Jijimya - Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Mhe. Francis Manyanda - Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Mhe. Joel Ndettoson - Diwani kata ya Kishapu
      • Mhe. Mohamed Aman - Diwani kata ya Ndoleleji
      • Mhe. Lucas Nkende - Diwani kata ya Mwamashele
      • Mhe. Pontias Daud - Diwani kata ya Mwataga
      • Mhe. James Kasomi - Diwani kata ya Bubiki
      • Mhe. Bushi Mpina - Diwani kata ya Mwamalasa
      • Mhe. Nyama Kisinza - Diwani kata ya Somagedi
      • Mhe. Mashini W. Washima - Diwani kata ya Uchunga
      • Mhe. Anderson Mandia - Diwani kata ya Ukenyenge
      • Mhe. Edward Manyama - Diwani kata ya Kiloleli
      • Mhe. Reuben Siyabo - Diwani kata ya Bupigi
      • Mhe. Bujiku Nyanda - Diwani kata ya Mwaweja
      • Mhe. Michael Paul - Diwani kata ya Shagihilu
      • Mhe. Luhende S. Luhende - Diwani kata ya Lagana
      • Mhe. Richard Dominico - Diwani kata ya Talaga
      • Mhe. James Kamuga - Diwani kata ya Igaga
      • Mhe. Lameck Nsubata - Diwani kata ya Itilima
      • Mhe. Mpemba Malangahe - Diwani kata ya Bunambiyu
      • Mhe. Makenzi Charles - Diwani kata ya Busangwa
      • Mhe. Nestory Kalugula - Diwani kata ya Ngofila
      • Mhe. Lwinzi Kidiga - Diwani kata ya Maganzo
      • Mhe. Samson Gelewa - Diwani kata ya Mwasubi
      • Mhe. Sarah Marco - Diwani kata ya Idukilo
      • Mhe. Enock Bundala - Diwani kata ya Masanga
      • Mhe. Thabidha Mmbando - Diwani kata ya Mwakipoya
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Mwenyekiti wa Halmashauri
  • miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
  • Kituo Cha Habari
    • maktaba ya picha
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa za Vyombo vya Habari
  • Maeneo
    • Kata
      • Orodha ya Kata
    • Tarafa
      • Orodha ya Tarafa
    • Vijiji
      • Orodha ya Vijiji

VIJIJI 16 VINAVYOZUNGUKA MIGODI KISHAPU MIGOGORO YA ARDHI KUKOMESHWA

Posted on: June 27th, 2025

Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi Kanda ya Kaskazini imekamilisha zoezi la kuandaa mpango wa matumizi ya ardhi Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga katika Vijiji Kumi na sita (16) vinavyozunguka maeneo ya migodi ya Williamson na Al hilal.

Mkuu wa Kanda ya Kaskazini wa Tume hiyo Bw.Amos Mpuga akizungumza mbele ya Mkuu wa Wilaya hiyo na Mkurugenzi Mtendaji amesema zoezi hilo lililenga Vijiji 16 na vyote vimefikiwa ikiwa ni utekelezaaji wa maelekezo ya Kamati ya Mawaziri ya kufanya tathimini ya maeneo yenye migogoro iliyoundwa chini ya Hayati Mhe.Rais Dkt John Pombe Magufuri.

"Kwa Wilaya ya Kishapu ilibainika kuwa maeneo yenye migogoro ni Vijiji vinavyopakana na migodi ya madini kwani vipo baadhi ya vijiji vilikuwa vimeingilia mipaka ya maeneo ya migodi na vingine vinavyozunguka vilikuwa vinaendelea kuingilia migodi, hivyo mapendekezo ya Mawaziri yalikuwa Vijiji vilivyovamia kwa kiwango kikubwa maeneo ya migodi waachiwe maeneo hayo wananchi na maeneo ambayo hayajavamiwa na wananchi yalindwe kwa ajili ya migodi" amesema Mpuga.

Mpuga ameongeza kuwa baada ya serikali kubaini hivyo Kamati ilitoa maelekezo ya uandaaaji wa mipango wa matumizi ya ardhi ili kuondoa migogoro inayosababishwa na wananchi kuvamia maeneo ya migodi.

"Kipekee nikushukuru Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi kwa kutupa ushirikiano kwani tumefaanikiwa kwa kiwango kikubwa ukamilishaji wa zoezi hili ndani muda uliopangwa,tumekamilisha hatua ya kwanza hadi ya nne kwa kutenga maeneo ya matumizi mbalimbali ikiwemo Kilimo,Malisho,uchimbaji mdogo na mengine yaliyopendekezwa na wananchi kulingana na uhitaji wao na Vijiji vyote wameunda sheria ndogo ya kulinda maeneo yaliyotengwa kwa matumizi husika"Ameongeza.

Amesema zimebakia hatua mbili ikiwa ni hatua ya Mipango Kina na utoaji Hati Milki kwenye maeneo hayo ili yawe na tija kwa wananchi lengo likiwa ni kuondoa migogoro na wananchi kujikwamua kiuchumi kupitia ardhi waliyonayo.

"Kama eneo limetengwa kwa ajili ya kilimo hivyo ni wajibu wa Maafisa kilimo kuwaelimisha kuhusiana na kilimo bora na cha kisasa ili wananchi wazalishe kwa kiwango kikubwa na wajipatie kipato na maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya migodi wataalamu wake pia watatoa elimu ya kina ili wachimbaji wetu wadogowadogo wachimbe kwa tija na kujikwamua kiuchumi vivyo hivyo na maeneo mengine wataalamu husika watatoa elimu ya kina" Ameongeza Mpuga

Amesema baada ya hayo maeneo kufanyiwa mpango kina kila mwananchi atapewa hati milki kwa ajili ya kumiliki rasmi maeneo yao kwani hadi sasa bado wanayamiliki kienyeji hivyo usalama wake bado ni mdogo ni rahisi mtu kudhurumiwa ama kunyang'anywa eneo lake ambalo halina hati ila eneo lililopimwa na kuwa na hati linakuwa na ulinzi wa kisheria.

Ametoa rai kwa serikali ya Halmashauri ya Wilaya hiyo kuwa na utaratibu wa kutenga bajeti za ukamilishaji hatu zilizobakia na Tume itasaaidia kujenga uwezo kwa timu ya Mipango ya matumzi ya ardhi ya Wilaya ili waendelee na mchakato wa upimaji na utoaji wa hati milki kwenye meneo ya wananchi.

Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe.Peter Masindi amepongeza jitihada za serikali za kuhakikisha amani na utulivu unaendelea kuimarishwa kwa wananchi kwani baada ya hatua zote kukamilika hakutakuwa na migogoro ambayo imekuwa ikisababisha baadhi ya maisha ya watu kuwa hatarini na wengine kupoteza maisha kwa kugombania ardhi.

"Zoezi hili likikamilika kila mwananchi atajua mipaka yake na hakuna atakayeweza kumuingilia mwingine maana kila ardhi itatambulika kisheria tofauti na umilki wa kienyeji ambao watu uweka mawe ama kupanda KataniMpaka ambavyo kiuhalisia vinamishika, hivyo niiombe Tume tena endapo mtapata fedha mtusaidie kwenye Vijiji vingine vilivyobakia hata visivyo zunguka migodi kwani migogoro ya ardhi bado ni kitendawili kwa baadhi ya maeneo"Amesema Mkuu huyo.

Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Emmanuel Johnson amekiri kuwepo kwa migogoro kwenye Vijiji 16 vinavyozunguka migodi hiyo hivyo kutokana na ushirikishwaji wananchi katika mpango huo umesaidia kuwaelimisha na kuwapa imani Halmashauri ya uwepo wa utatuzi wa kudumu wa migogoro ya ardhi kwenye maeneo hayo kwani wawekezaji na wananchi watakuwa salama kila mmoja kwenye eneo lake.

Johnson amesema lengo la Halmashauri ni kufikia Vijiji vyote kwa kutengenezewa mpango wa matumizi bora ya ardhi huku akiahidi Halmashauri itatenga fedha kupitia mapato ya ndani,Csr na wadau mbalimbali ili kuhakikisha Vijiji vyote vinafikiwa na mpango huo.

'Tunatamani kuona mpango huu ukifikia mwisho tunaamini tutapata faida kubwa katika Wilaya yetu mapato yataongezeka kwa sababu pindi tu ukamilikashwaji ugawaji Hati Milki ukikamilika wananchi watapata mikopo na kufanya biashara na uwekezaji mbalimbali watajikwamua kiuchumi na watalipa kodi ya serikali pia"Amesema Johnson

Mkuu wa Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi Kanda ya Kaskazini Bw.Amos Mpuga

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Mhe Peter Masindi 

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Emmanuel Johnson 

Matangazo

  • TAARIFA YA MTIRIRIKO WA FEDHA KWA KIPINDI KILICHOISHIA TAREHE 30 JUNE. 2022 August 14, 2023
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI November 03, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MFAMASIA December 14, 2021
  • Orodha ya Walioitwa kwenye Usaili September 20, 2024
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • VIJIJI 16 VINAVYOZUNGUKA MIGODI KISHAPU MIGOGORO YA ARDHI KUKOMESHWA

    June 27, 2025
  • TAKUKURU YAZINDUA JENGO JIPYA KISHAPU, LAWAPA WANANCHI IMANI NA UJASIRI KUPINGA RUSHWA

    June 26, 2025
  • DED KISHAPU AHIMIZA USHIRIKIANO KATI YA NGO's NA SERIKALI

    June 23, 2025
  • TIP YAENDESHA MAFUNZO YA KUPINGA UKATILI KISHAPU

    June 17, 2025
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa