• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Utawala
      • Biashara, Viwanda na Uwekezaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya jamii
      • Afya
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Tehama
      • Utamaduni, Sanaa na Michezo
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Usafi wa Mazingira na Udhibiti Taka
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Kilimo na Mifugo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya kuonana na mwenyekiti wa Halmashauri
    • Ratiba za vikao vya kisheria vya MSM
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya picha na video za shughuli za maendeleo

MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI WAMTEUA MWENYEKITI MPYA HALMASHAURI YA WILAYA KISHAPU

Posted on: December 3rd, 2025

Mwenyekiti mpya wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu na Diwani wa Kata ya Ndoleleji Mhe. Josephat Limbe Emmanuel, akizungumza kwenye mkutano wa kwanza wa baraza la madiwani uliofanyika leo Disemba 03,2025 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo.

Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu kupitia baraza jipya la Madiwani limemteua Mwenyekiti  na Makamu Mwenyekiti watakaowaongoza madiwani wateule katika kipindi kijacho. Mkutano huo umefanyika leo Disemba 03,2025 katika ukumbi wa Halmashauri hiyo, ambapo shughuli muhimu za kiutawala zimefanyika ikiwemo madiwani wateule kuapishwa, kuundwa kwa kamati za kudumu za Halmashauri  na kupitisha ratiba ya vikao vya Halmashauri.

Akizungumza mara baada ya kutangazwa mshindi; Mwenyekiti Mteule wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu ambaye ni diwani wa kata ya Ndoleleji  kupitia Chama cha Mapinduzi, Mhe.Josephat .L. Emmanuel amewashukuru madiwani wenzake kwa kumuamini kumpa nafasi hiyo na kuahidi kuongoza baraza hilo kwa uadilifu, weledi na misimamo inayojenga mustakabali wa wananchi wa Kishapu.

“Tunalo jukumu kubwa la kwenda kuwatumikia Wanamchi wetu ambao wametuamini kwa lengo kubwa la kuwapatia maendeleo, na huduma za kijamii ziwafikie popote pale walipo. Tutahakikisha tunasimamia maelekezo ya Mheshimiwa Rais na maazimio ya baraza letu” Alisema.

Aidha Mhe. Enock Reuben Bundala ambaye ni diwani wa kata ya Masanga alichaguliwa kuwa makamu Mwenyekiti wa Halmashauri,huku akiwashukuru Mkuu wa Wilaya,madiwani wenzake na wananchi wa Kishapu kwa kumuamini kumpa nafasi hiyo.Mhe.Bundala ameomba ushirikiano na kusisitiza kushauriana kwa pamoja ili Kishapu isonge mbele.

Makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu na diwani wa kata ya Masanga Mhe. Enock .R. Bundala akizungumza kwenye mkutano wa  kwanza wa baraza la madiwani uliofanyika leo Disemba 03, 2025 katika ukumbi wa Halmashauri hiyo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kishapu katika hotuba yake amewapongeza viongozi hao huku akiwakumbusha thamani ya imani waliyopewa na wananchi wa Kishapu.

“Nafasi mliyopewa ni dhamana nzito. Wajibu wenu kama madiwani ni kuhakikisha mnasikiliza na kutatua kero za wananchi. Shirikianeni na watendaji wenu, maana ninyi ndio viongozi mnaowaongoza katika maeneo mnayoyasimamia” Amesema

Mhe. Masindi amesisitiza pia viongozi hao kutojihusisha na maslahi binafsi kwenye miradi ya Serikali. “Vunjeni makundi ya kisiasa yaliyokuepo kabla ya uchaguzi ili mkumbatie wawekezaji. Zingatieni mipaka ya utendaji. Tunataka Kishapu iwe mfano wa utawala bora.” Ameongeza Mhe. Masindi.

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga Mhe.Peter Masindi akizungumza kwenye mkutano wa kwanza wa baraza la madiwani uliofanyika leo Disemba 03,2025 katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo.

Naye, Katibu Tawala wa Wilaya ya Kishapu Bi. Fatma Mohamed, aliyekuwa mwenyekiti wa muda wa kikao kabla ya kuapishwa na kuchaguliwa kwa Mwenyekiti mpya, amewapongeza madiwani hao kwa kukamilisha uchaguzi na kuwataka waende kwenye hatua ya utekelezaji.

“Wananchi wamewachagua kwa imani kubwa. Huu  sio wakati wa maneno tena ni wakati wa kazi. Tekelezeni yale mliyoyaahidi wakati wa kampeni.” Amesema.

Katibu Tawala Wilayani Kishapu mkoani Shinyanga, Bi. Fatma Mohammed akizungumza kwenye mkutano wa kwanza wa baraza la Madiwani uliofanyika Disema 03,2025 katika ukumbi wa Halmashauri hiyo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Ndg. Emmanuel Johnson amewataka madiwani kuimarisha ushirikiano katika ngazi zote za utendaji ili kujenga mazingira mazuri ya kazi.

“Ili tujenge Kishapu tunayoiota ni lazima tushirikiane. Fanyeni maamuzi kwa kuzingatia mapato halisi ya Halmashauri, na tumieni busara katika kushughulikia makosa ya Watumishi. Mko hapa kuwaongoza, kuwashauri na kuwaweka kwenye mstari”. Amesema Mkurugenzi

 Pia amewakumbusha umuhimu wa kuzifahamu kwa kina kanuni, taratibu na sheria za Halmashauri pamoja na kanuni za Utumishi wa Umma ili kuhakikisha utendaji wenye uwazi na uadilifu.

 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Ndg. Emmanuel Johnson akizungumza kwenye mkutano wa kwanza wa baraza la madiwani uliofanyika  Disemba 03,2025 katika ukumbi wa Halmashauri hiyo.

Katika hatua nyingine, madiwani wapya 39 waliapishwa,huku Hakimu Mkazi Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Bi. Johanitha Projest akiratibu zoezi hilo na kisha kuunda kamati za kudumu za Halmashauri ambazo ndizo muhimili wa utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo.

Hakimu mkazi Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Bi. Joanitha Projest akiongoza zoezi la kutoa viapo kwa madiwani wateule,Disemba 03,2025 katika ukumbi wa Halmashauri hiyo.

Baadhi ya Madiwani wateule kutoka katika kata mbalimbali za Wilaya ya Kishapu wakila kiapo mara baada ya kuapishwa na Hakimu Mkazi Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, leo Disemba 03,2025 katika ukumbi wa Halmashauri hiyo.

Aidha Mkutano huu wa baraza la kwanza la madiwani umeudhuriwa na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kishapu, mwakilishi wa Katibu Tawala mkoa wa Shinyanga, wajumbe wa Tume ya Uchaguzi, Taasisi za kifedha za benki ya NMB na CRDB pamoja na watumishi Wakuu wa idara na vitengo wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu. 







Matangazo

  • TANGAZO LA MWALIKO WA MKUTANO January 20, 2026
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI December 22, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI November 21, 2025
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • SHINYANGA YAJIPIMA UTEKELEZAJI MKATABA WA LISHE NA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    January 16, 2026
  • KAMATI YA FUM KISHAPU YAKAGUA MIRADI YA ZAIDI YA TSH. B. 1.2

    January 15, 2026
  • RC MHITA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI NA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI KISHAPU.

    January 10, 2026
  • RC MHITA AWATAKA MADIWANI KISHAPU KUDUMISHA USHIRIKIANO NA MSHIKAMANO - NGUZO KUFANIKISHA MIPANGO YA MAENDELEO.

    December 19, 2025
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa