• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Utawala
      • Biashara, Viwanda na Uwekezaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya jamii
      • Afya
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Tehama
      • Utamaduni, Sanaa na Michezo
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Usafi wa Mazingira na Udhibiti Taka
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Kilimo na Mifugo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya kuonana na mwenyekiti wa Halmashauri
    • Ratiba ya vikao vya kisheria vya MSM
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Sheria ndogo ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya picha na video za shughuli za maendeleo

MWENYEKITI KISHAPU ARIDHISHWA NA HUDUMA ZA AFYA

Posted on: February 19th, 2026

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga, Mhe. Josephat Limbe, akizungumza kwenye ziara yake ya kikazi Februari 19, 2026 katika Hospitali ya Wilaya ya Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kwa lengo la kukagua utoaji wa huduma na kuzungumza na watumishi wa afya


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga, Mhe. Josephat Limbe, amefanya ziara ya kikazi Februari 19, 2026 katika Hospitali ya Wilaya ya Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kwa lengo la kukagua utoaji wa huduma na kuzungumza na watumishi wa afya.

Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Kishapu mkoani Shinyanga, Pius Mwandu, akizungumza kwenye ziara ya kikazi ya Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe. Josephat Limbe Februari 19, 2026 katika Hospitali ya Wilaya ya Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kwa lengo la kukagua utoaji wa huduma na kuzungumza na watumishi wa afya

Katika ziara hiyo, Mhe. Limbe amepongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuimarisha sekta ya afya kupitia maboresho ya miundombinu na upatikanaji wa vifaa tiba, hali inayowezesha wananchi kupata huduma bora karibu na maeneo yao.

Mganga Mfawidhi wa hospitali ya Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga ya Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Dkt. Mohamed Ally Mkumbwa, akizungumza kwenye ziara ya kikazi ya Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe. Josephat Limbe Februari 19, 2026 katika Hospitali ya Wilaya ya Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kwa lengo la kukagua utoaji wa huduma na kuzungumza na watumishi wa afya


Aidha, amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Emmanuel Johnson, kwa usimamizi madhubuti wa fedha za Serikali uliowezesha utekelezaji mzuri wa miradi ya maendeleo na kuinua kiwango cha huduma hospitalini hapo.

Gabriel K. Pastory Afisa tawala Ofisi ya Mkurugenzi, akizungumza kwenye ziara ya kikazi ya Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe. Josephat Limbe Februari 19, 2026 katika Hospitali ya Wilaya ya Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kwa lengo la kukagua utoaji wa huduma na kuzungumza na watumishi wa afya


Akizungumza na watumishi wa hospitali, Mhe. Limbe amewahimiza kuendelea kufanya kazi kwa kuzingatia misingi ya taaluma zao, kutoa huduma kwa wakati, kushirikisha jamii kwa kuwapa elimu ya afya na kulinda heshima ya taaluma zao.

“Nimeridhishwa na jinsi mnavyotoa huduma kwa wateja wenu licha ya kuwa jukumu la kuponya mlilonalo ni gumu na zito. Ninawapongeza sana,” amesema Mhe. Limbe.

Kwa upande wake, Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo, Dkt. Mohamed Ally Mkumbwa, ameishukuru Serikali kwa kuweka mazingira mazuri ya utoaji wa huduma za afya na kuomba kuendelea kuboreshwa kwa mazingira ya kazi kwa watumishi wa afya.

Dkt. Mkumbwa amesema hospitali hiyo kwa sasa ina wodi tano za kulaza wagonjwa ambazo ni wodi ya wanawake, wanaume, watoto, wazazi pamoja na wodi ya watoto wachanga mahututi (NCU), ikiwa na jumla ya vitanda 156.

Ameeleza kuwa huduma zinazotolewa ni pamoja na huduma za meno, macho, dharura, upasuaji, maabara, kuhifadhi maiti, kulaza wagonjwa, mazoezi ya viungo, huduma za baba, mama na mtoto (RCH), ustawi wa jamii, kliniki ya CTC, huduma za mawimbi ya sauti (Ultrasound), huduma za mionzi (X-Ray) pamoja na huduma za dawa.

Kwa mujibu wa Dkt. Mkumbwa, maboresho hayo yamechangia kupunguza vifo vya wajawazito kutoka vifo sita mwaka 2021 hadi kifo kimoja mwaka 2025, huku vifo vya watoto chini ya miaka mitano vikishuka kutoka 24 mwaka 2021 hadi sita mwaka 2025.

Ameongeza kuwa kwa juhudi za Serikali na wadau mbalimbali, hospitali imefanikiwa kuongeza majengo hadi kufikia 20, hatua inayoimarisha zaidi utoaji wa huduma.


Akizungumza katika kikao hicho, kwa niaba ya Mkuu wa Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu. Gabriel K. Pastory ambaye ni Afisa tawala Ofisi ya Mkurugenzi, amewasisitiza watumishi kuendelea kufanya kazi kwa kuzingatia miongozo, kanuni, sheria na taratibu za utumishi wa umma. Amesema kuwa nidhamu na ufuataji wa taratibu ni msingi wa utoaji wa huduma bora na endelevu kwa wananchi.

Gabriel ameongeza kuwa Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji itaendelea kuwa karibu na watumishi hao, kuwapa ushirikiano unaohitajika na kuhakikisha wanapata mazingira wezeshi ya kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Naye Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Kishapu, Pius Mwandu, amesema kutokana na utendaji mzuri wa watumishi wa hospitali hiyo, Mbunge wa Jimbo hilo, Lucy Mayenga, atafanya jambo maalum la kuwapongeza na kuwatia moyo ili waendelee kutoa huduma bora kwa wananchi.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA February 16, 2026
  • TANGAZO LA MWALIKO WA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI January 20, 2026
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI December 22, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI November 21, 2025
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • MWENYEKITI KISHAPU ARIDHISHWA NA HUDUMA ZA AFYA

    February 19, 2026
  • KISHAPU YAONGEZA KASI UTEKELEZAJI WA PJT-MMMAM

    February 19, 2026
  • WAKULIMA WA PAMBA WANAOZINGATIA KANUNI BORA WAPEWA VIFAA VYA PEMBEJEO-KISHAPU

    February 18, 2026
  • KISHAPU YAPITISHA BAJETI YA BILIONI 54.3 2026/2027

    February 12, 2026
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa