• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
    • Idara
      • Fedha
      • Rasilimali watu
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
  • Nyaraka
    • Fomu za kujinga na Kidato cha Tano
      • Shule ya Sekondari Kishapu
      • Shule ya Sekondari Shinyanga
    • Mpango wa bajeti wa mwaka 2021/2022
    • Matangazo
    • Sheria ndogo ya ushuru wa huduma
    • Mifumo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
      • Uvuvi wa Samaki katika Bwawa la Songwa, Bwawa mhumbu
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Mhe. William Luhende Jijimya - Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Mhe. Francis Manyanda - Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Mhe. Joel Ndettoson - Diwani kata ya Kishapu
      • Mhe. Mohamed Aman - Diwani kata ya Ndoleleji
      • Mhe. Lucas Nkende - Diwani kata ya Mwamashele
      • Mhe. Pontias Daud - Diwani kata ya Mwataga
      • Mhe. James Kasomi - Diwani kata ya Bubiki
      • Mhe. Bushi Mpina - Diwani kata ya Mwamalasa
      • Mhe. Nyama Kisinza - Diwani kata ya Somagedi
      • Mhe. Mashini W. Washima - Diwani kata ya Uchunga
      • Mhe. Anderson Mandia - Diwani kata ya Ukenyenge
      • Mhe. Edward Manyama - Diwani kata ya Kiloleli
      • Mhe. Reuben Siyabo - Diwani kata ya Bupigi
      • Mhe. Bujiku Nyanda - Diwani kata ya Mwaweja
      • Mhe. Michael Paul - Diwani kata ya Shagihilu
      • Mhe. Luhende S. Luhende - Diwani kata ya Lagana
      • Mhe. Richard Dominico - Diwani kata ya Talaga
      • Mhe. James Kamuga - Diwani kata ya Igaga
      • Mhe. Lameck Nsubata - Diwani kata ya Itilima
      • Mhe. Mpemba Malangahe - Diwani kata ya Bunambiyu
      • Mhe. Makenzi Charles - Diwani kata ya Busangwa
      • Mhe. Nestory Kalugula - Diwani kata ya Ngofila
      • Mhe. Lwinzi Kidiga - Diwani kata ya Maganzo
      • Mhe. Samson Gelewa - Diwani kata ya Mwasubi
      • Mhe. Sarah Marco - Diwani kata ya Idukilo
      • Mhe. Enock Bundala - Diwani kata ya Masanga
      • Mhe. Thabidha Mmbando - Diwani kata ya Mwakipoya
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Mwenyekiti wa Halmashauri
  • miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
  • Kituo Cha Habari
    • maktaba ya picha
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa za Vyombo vya Habari
  • Maeneo
    • Kata
      • Orodha ya Kata
    • Tarafa
      • Orodha ya Tarafa
    • Vijiji
      • Orodha ya Vijiji

SERIKALI KISHAPU YAZUIA TANI 30 ZA PAMBA ZILIZOPIMWA KINYUME NA TARATIBU

Posted on: June 4th, 2025


Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Mhe. Peter Masindi akizungumza na wananchi wa Ngofila wakati wa ziara yake ya ukaguzi wa ununuzi wa pamba katika vyama vya msingi na kufanya mkutano wa hadhara Ngofila lengo ikiwa ni kufuatilia mafanikio na changamoto za msimu wa ununuzi wa pamba ili kuhakikisha mnyororo wa masoko unakwenda vizuri bila kukwamishwa na ukiukwaji wa taratibu wa ununuzi.

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Mhe. Peter Masindi ameagiza kampuni ya Aham Limited kushusha tani 30 za pamba zilizonunuliwa kinyume na taratibu kutoka Chama cha Msingi cha Kiloleli (Amcos), akisisitiza kuwa ununuzi huo ulifanyika kwa kutumia mizani isiyo rasmi na hivyo kukiuka kanuni za ununuzi wa zao hilo.

Akizungumza Juni 3,2025, wakati wa ziara yake ya ukaguzi wa ununuzi wa pamba katika vyama vya msingi vya Mwamashele, Mwamanota, Inolelo (Amcos ya Raha ya Balimi), Ngofila, Kalitu na Kiloleli na kufanya mkutano wa hadhara Ngofila, Mhe. Masindi amesema lengo ni kufuatilia mafanikio na changamoto za msimu wa ununuzi wa pamba ili kuhakikisha mnyororo wa masoko unakwenda vizuri bila kukwamishwa na ukiukwaji wa taratibu.

"Aham amenunua pamba kupitia mzani ya kawaida badala ya mzani wa kidijitali kama inavyotakiwa, kuanzia sasa naagiza pamba yote ishushwe na ipimwe upya kwa kutumia mzani wa kidijitali ili kuwezesha serikali kupata mapato stahiki na taarifa sahihi kwa Bodi ya Pamba," amesema Masindi.

Ameeleza kuwa matumizi ya mizani isiyo rasmi yanapotosha takwimu muhimu kwa Halmashauri, husababisha kukosekana kwa makadirio sahihi ya ushuru wa 3% kwa kilo moja, na hata kuathiri taarifa za idadi ya wakulima husika jambo ambalo ni muhimu kwa maandalizi ya msimu ujao kwa bodi ya pamba vilevile, ameonya kuwa mkulima huenda akapunjwa, huku mnunuzi akijikuta akikumbwa na adhabu za kusafirisha mazao bila vibali halali.

Katika hatua nyingine, kufuatia malalamiko kutoka kwa wakulima wa Kata ya Ngofila kuhusu kucheleweshwa kwa malipo Masindi amemuelekeza mnunuzi kutoka Lugeye Company Limited anayenunua pamba katika vyama vya msingi vya Mwamanota, Ngofila na Kalitu kuhakikisha anawalipa wakulima wote kwa wakati.

"Mpango wa serikali ya awamu ya sita ni kuhakikisha mkulima ananufaika hivyo kama mnunuzi hana fedha za kulipa, apishe mnunuzi mwingine hatutaki ucheleweshaji wa malipo wala ubadhirifu wowote kwenye mizani na wote wanaonunua pamba kwenye maeneo husika waende kwa wakati kama kuna sababu nyingine watueleze mapema ili turuhusu wanunuzi wengine kuendelea na ununuzi pamba" amepngeza kwa msisitizo.

Mkuu huyo wa Wilaya pia amewasihi wakulima kuuza pamba kwenye vyama vya msingi pekee huku wakijiwekea mipango ya muda mfupi, kati na mrefu kwa ajili ya kuboresha maisha yao kupitia zao la pamba akiwakumbusha umuhimu wa kuwekeza katika elimu ya watoto wao,kuweka akiba ya fedha na vyakula, ujenzi wa nyumba bora na uzingatiaji wa lishe bora kutokana na fedha watakazozipata.

"Mwanaume aliyefanikiwa huwa na mwanamke nyuma yake hivyo msitumie fedha za pamba kwa 'nzige' (wanawake wauzao miili yao) watamaliza fedha zenu na kuwaachia magonjwa, mwisho wake mtawatesa wake na watoto wenu",ameongeza.

Masindi ameeleza kuridhishwa na mwenendo wa ukusanyaji wa pamba huku akihimiza wakulima kuuza pamba safi ili wapate bei nzuri na kuhakikisha vyama vya msingi vinafuata maelekezo ya serikali na Bodi ya Pamba katika ununuzi na uuzaji.

Mwakilishi wa Kampuni ya ununzi wa pamba ya Lugeye, Juni Butina akizungumza kuhusiana na ucheleweshwaji malipo kwa wakulima amesema changamoto iliyotokea ni ucheleweshwaji wa taarifa ya kuomba fedha kutoka kwa viongozi wa Amcos ili waletewe kwa wakati lakini kampuni hiyo itahakikisha inafuata taratibu zote za ununuzi walizoelekezwa na serikali ya Wilaya na bodi ya pamba.

Takwimu za Ukusanyaji Pamba (Hadi Juni 3, 2025)

Mwamashele Amcos Tani 7 Mnunuzi ni Bioustain Tanzania Ltd,Mwamanota Amcos Tani 12,Inolelo (Raha ya Balimi) Tani 14,Ngofila & Kalitu Amcos zaidi ya Tani 10Mnunuzi ni Lugeye Company Ltd pamoja   Kiloleli Amcos zaidi ya Tani 50 na Mnunuzi ni Aham Company Limited.

Mnamo mwezi Mei,15,2025 Mkuu wa Wilaya ya Kishapu alizindua msimu mpya wa pamba 2025/2026 kwa ngazi ya Wilaya akikutana na wadau mbalimbali wa zao hilo ambapo masuala muhimu yalizungumziwa kuhusu bei,mizani,ubora wa pamba,uuzaji na ununuzi ambapo pamba safi itauzwa kwa bei elekezi ya Tsh. 1,150 kwa kilo, huku pamba fifi ikiuzwa kwa Tsh. 575 kwa kilo.


Matangazo

  • TAARIFA YA MTIRIRIKO WA FEDHA KWA KIPINDI KILICHOISHIA TAREHE 30 JUNE. 2022 August 14, 2023
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI November 03, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MFAMASIA December 14, 2021
  • Orodha ya Walioitwa kwenye Usaili September 20, 2024
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • MCHAKATO WAANZA UJENZI DAMPO LA KISASA KISHAPU KUIMARISHA USAFI WA MAZINGIRA

    July 26, 2025
  • RC MHITA AFANYA ZIARA YA KIKAZI KISHAPU

    July 22, 2025
  • WANANCHI 1,200 VIJIJI VYA MFANO KISHAPU WAPEWA HATI MILKI ZA KIMILA

    July 23, 2025
  • LISHE BORA YAPAA SHULENI KISHAPU

    July 16, 2025
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa