• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
    • Idara
      • Fedha
      • Rasilimali watu
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
  • Nyaraka
    • Fomu za kujinga na Kidato cha Tano
      • Shule ya Sekondari Kishapu
      • Shule ya Sekondari Shinyanga
    • Mpango wa bajeti wa mwaka 2021/2022
    • Matangazo
    • Sheria ndogo ya ushuru wa huduma
    • Mifumo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
      • Uvuvi wa Samaki katika Bwawa la Songwa, Bwawa mhumbu
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Mhe. William Luhende Jijimya - Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Mhe. Francis Manyanda - Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Mhe. Joel Ndettoson - Diwani kata ya Kishapu
      • Mhe. Mohamed Aman - Diwani kata ya Ndoleleji
      • Mhe. Lucas Nkende - Diwani kata ya Mwamashele
      • Mhe. Pontias Daud - Diwani kata ya Mwataga
      • Mhe. James Kasomi - Diwani kata ya Bubiki
      • Mhe. Bushi Mpina - Diwani kata ya Mwamalasa
      • Mhe. Nyama Kisinza - Diwani kata ya Somagedi
      • Mhe. Mashini W. Washima - Diwani kata ya Uchunga
      • Mhe. Anderson Mandia - Diwani kata ya Ukenyenge
      • Mhe. Edward Manyama - Diwani kata ya Kiloleli
      • Mhe. Reuben Siyabo - Diwani kata ya Bupigi
      • Mhe. Bujiku Nyanda - Diwani kata ya Mwaweja
      • Mhe. Michael Paul - Diwani kata ya Shagihilu
      • Mhe. Luhende S. Luhende - Diwani kata ya Lagana
      • Mhe. Richard Dominico - Diwani kata ya Talaga
      • Mhe. James Kamuga - Diwani kata ya Igaga
      • Mhe. Lameck Nsubata - Diwani kata ya Itilima
      • Mhe. Mpemba Malangahe - Diwani kata ya Bunambiyu
      • Mhe. Makenzi Charles - Diwani kata ya Busangwa
      • Mhe. Nestory Kalugula - Diwani kata ya Ngofila
      • Mhe. Lwinzi Kidiga - Diwani kata ya Maganzo
      • Mhe. Samson Gelewa - Diwani kata ya Mwasubi
      • Mhe. Sarah Marco - Diwani kata ya Idukilo
      • Mhe. Enock Bundala - Diwani kata ya Masanga
      • Mhe. Thabidha Mmbando - Diwani kata ya Mwakipoya
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Mwenyekiti wa Halmashauri
  • miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
  • Kituo Cha Habari
    • maktaba ya picha
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa za Vyombo vya Habari
  • Maeneo
    • Kata
      • Orodha ya Kata
    • Tarafa
      • Orodha ya Tarafa
    • Vijiji
      • Orodha ya Vijiji

WATABIBU KISHAPU WAPATIWA MAFUNZO YA MATUMIZI UMEME JUA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA

Posted on: May 14th, 2025

Watabibu wa vituo 15 vya kutolea huduma za afya katika Wilaya ya Kishapu wamepatiwa mafunzo maalum ya kuwajengea uwezo kuhusu matumizi sahihi ya mfumo wa umeme jua uliofungwa katika vituo hivyo, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuboresha utoaji wa huduma za afya kwa msaada wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na watoto (UNICEF).

Mafunzo hayo yamefanyika leo tarehe 14 Mei 2025, katika ukumbi wa Hospitali ya Wilaya ya Kishapu Dkt. Jakaya Kikwete, yakihusisha wataalamu wa afya kutoka vituo mbalimbali vya huduma ya afya. Mafunzo yamelenga kuwawezesha wahudumu wa afya kutumia kwa ufanisi mifumo ya nishati ya jua kwa ajili ya kuendesha vifaa vya kitabibu, kuhifadhi dawa zinazohitaji ubaridi, pamoja na kuwezesha huduma za usiku na dharura.

Mkufunzi mkuu wa mafunzo hayo, Bw. George Michael, kutoka kampuni ya Solar AG Energies, alieleza kuwa elimu waliyoitoa inalenga kuleta mabadiliko ya kweli katika utoaji wa huduma. “Mfumo wa umeme jua una faida nyingi hasa katika maeneo ya vijijini. Tunataka kuhakikisha kwamba kila mhudumu wa afya anaujua vyema mfumo huu, na anaweza kuutumia na kuufanyia matengenezo madogo pasipo usumbufu,” alisema Bw. Michael.

Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Dkt. Joseph Stephano Bahati, ambaye pia alikuwa mratibu wa mafunzo hayo, alieleza kuwa mradi huo ni hatua kubwa katika kuimarisha huduma bora za afya vijijini. “Tunashukuru sana kwa msaada huu wa UNICEF. Kupitia mafunzo haya, tunategemea maboresho makubwa katika huduma za afya hususan katika usimamizi wa vifaa vya kitabibu vinavyotegemea nishati ya umeme,” alisema Dkt. Bahati.

Msimamizi wa mafunzo hayo, Mhandisi Fredy Peter, ambaye ni mhandisi wa wilaya ya Kishapu, alieleza kuwa usimikaji wa mifumo ya umeme jua katika vituo 15 vya afya ni sehemu ya utekelezaji wa mpango wa serikali wa kutumia nishati jadidifu katika huduma za jamii. “Tulihakikisha kwamba mifumo iliyofungwa ni ya kisasa na yenye uwezo mkubwa wa kuhifadhi umeme kwa muda mrefu. Sasa tunawapa watumiaji uwezo wa kuisimamia vyema,” alieleza Mhandisi Fredy.

Mafunzo haya yanaakisi dhamira ya serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo katika kuhakikisha kuwa kila mwananchi anapata huduma bora za afya, bila kujali eneo analoishi. Kupitia ushirikiano huu na UNICEF, Wilaya ya Kishapu imepiga hatua muhimu katika kuhakikisha vituo vyote vya afya vinapata nishati ya uhakika, jambo ambalo litaongeza ufanisi na kuokoa maisha ya wananchi wengi

Matangazo

  • TAARIFA YA MTIRIRIKO WA FEDHA KWA KIPINDI KILICHOISHIA TAREHE 30 JUNE. 2022 August 14, 2023
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI November 03, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MFAMASIA December 14, 2021
  • Orodha ya Walioitwa kwenye Usaili September 20, 2024
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • CPA. MAKALA AIPONGEZA SERIKALI MAENDELEO KISHAPU – BUTONDO AOMBA DED ASIONDOLEWE

    May 23, 2025
  • DC KISHAPU AWAONYA WAVURUGA AMANI KATA YA MWASUBI NA BUNAMBIYU

    May 16, 2025
  • SERIKALI KUTUMIA DOLA MILIONI 77.4 KUZIWEZESHA KAYA DUNI LAKI MBILI NA ELFU 60 KILIMO NA UVUVI TANZANIA BARA

    May 15, 2025
  • WILAYA YA KISHAPU YAANZA MAANDALIZI YA KUPOKEA MWENGE WA UHURU AGOSTI 8, 2025

    May 14, 2025
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa