• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
    • Idara
      • Fedha
      • Rasilimali watu
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
  • Nyaraka
    • Fomu za kujinga na Kidato cha Tano
      • Shule ya Sekondari Kishapu
      • Shule ya Sekondari Shinyanga
    • Mpango wa bajeti wa mwaka 2021/2022
    • Matangazo
    • Sheria ndogo ya ushuru wa huduma
    • Mifumo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
      • Uvuvi wa Samaki katika Bwawa la Songwa, Bwawa mhumbu
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Mhe. William Luhende Jijimya - Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Mhe. Francis Manyanda - Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Mhe. Joel Ndettoson - Diwani kata ya Kishapu
      • Mhe. Mohamed Aman - Diwani kata ya Ndoleleji
      • Mhe. Lucas Nkende - Diwani kata ya Mwamashele
      • Mhe. Pontias Daud - Diwani kata ya Mwataga
      • Mhe. James Kasomi - Diwani kata ya Bubiki
      • Mhe. Bushi Mpina - Diwani kata ya Mwamalasa
      • Mhe. Nyama Kisinza - Diwani kata ya Somagedi
      • Mhe. Mashini W. Washima - Diwani kata ya Uchunga
      • Mhe. Anderson Mandia - Diwani kata ya Ukenyenge
      • Mhe. Edward Manyama - Diwani kata ya Kiloleli
      • Mhe. Reuben Siyabo - Diwani kata ya Bupigi
      • Mhe. Bujiku Nyanda - Diwani kata ya Mwaweja
      • Mhe. Michael Paul - Diwani kata ya Shagihilu
      • Mhe. Luhende S. Luhende - Diwani kata ya Lagana
      • Mhe. Richard Dominico - Diwani kata ya Talaga
      • Mhe. James Kamuga - Diwani kata ya Igaga
      • Mhe. Lameck Nsubata - Diwani kata ya Itilima
      • Mhe. Mpemba Malangahe - Diwani kata ya Bunambiyu
      • Mhe. Makenzi Charles - Diwani kata ya Busangwa
      • Mhe. Nestory Kalugula - Diwani kata ya Ngofila
      • Mhe. Lwinzi Kidiga - Diwani kata ya Maganzo
      • Mhe. Samson Gelewa - Diwani kata ya Mwasubi
      • Mhe. Sarah Marco - Diwani kata ya Idukilo
      • Mhe. Enock Bundala - Diwani kata ya Masanga
      • Mhe. Thabidha Mmbando - Diwani kata ya Mwakipoya
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Mwenyekiti wa Halmashauri
  • miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
  • Kituo Cha Habari
    • maktaba ya picha
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa za Vyombo vya Habari
  • Maeneo
    • Kata
      • Orodha ya Kata
    • Tarafa
      • Orodha ya Tarafa
    • Vijiji
      • Orodha ya Vijiji

WATENDAJI WA UCHAGUZI JIMBO LA KISHAPU WATAKIWA KUWA WAADILIFU NA WAAMINIFU

Posted on: October 25th, 2025

Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Kishapu Mkoani Shinyanga Joseph Sahani Swalala akizungumza wakati akifungua mafunzo kwa makarani waongozaji wapiga kura Oktoba 52,2025 katika Ukumbi wa Stage II Hoteli wilayani humo


Katika kuhakikisha Uchaguzi Mkuu unaendeshwa kwa weledi, uwazi na uadilifu, Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) Jimbo la Kishapu Mkoani Shinyanga imeendesha mafunzo maalum kwa watendaji wa uchaguzi wakiwemo makarani waongozaji wapiga kura kutoka katika Kata mbalimbali za Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu.


Mafunzo hayo yaliyofanyika Oktoba 25 Ukumbi wa Stage II Hotel ni sehemu muhimu ya maandalizi ya Uchaguzi Mkuu ujao Oktoba 29,2025 yakilenga kuwajengea uwezo washiriki ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kwa kuzingatia sheria, kanuni na maelekezo yaliyowekwa.

Kujenga Uelewa na Uadilifu

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa makarani waongozaji wapiga kura, Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo Hilo Joseph Sahani Swalala ambae ni mwakilishi wa Tume amesisitiza umuhimu wa watendaji wa uchaguzi kutambua dhamana kubwa waliyonayo kwa taifa, akieleza kuwa kazi ya kusimamia upigaji na kuhesabu kura ni jukumu nyeti linalohitaji uaminifu, umakini na uzingatiaji wa maadili ya kazi za umma.


“Dhamana mliyopewa ni kubwa na muhimu kwa mustakabali wa Taifa letu. Hivyo, mnatakiwa kufuata sheria, kanuni na maelekezo yote mtakayopatiwa hadi kukamilika kwa jukumu hili muhimu la Uchaguzi Mkuu,” amesema Swalala.


Jumla ya makarani 614 wameshiriki katika mafunzo hayo kutoka vituo 556 vilivyopo katika kata 29 za Halmashauri ya Kishapu. Washiriki hawa ni makarani waongozaji wapiga kura watakaosimamia shughuli za upigaji na kuhesabu kura katika vituo vyao husika.


Kupitia mafunzo haya, watendaji hao wamepata nafasi ya kubadilishana uzoefu, kujadili changamoto zinazoweza kujitokeza wakati wa uchaguzi, na kujifunza mbinu bora za kuhakikisha zoezi linakuwa huru, wazi na lenye amani na Kukuza Ujuzi na Uzoefu


Kwa wale wanaoshiriki kwa mara ya kwanza
Aidha Swalala ameongeza kuwa mafunzo hayo yamekuwa fursa adhimu ya kujifunza kutoka kwa watendaji wenye uzoefu mkubwa katika usimamizi wa chaguzi zilizopita. Kadhalika, kwa wale walio na uzoefu, yamekuwa jukwaa la kujiongezea maarifa mapya na kuimarisha mbinu za kiutendaji.


Wamekumbushwa kuwa Uchaguzi ni mchakato unaojumuisha hatua kadhaa za kikatiba na kisheria, na kwamba kila hatua inapaswa kufuatwa kwa umakini mkubwa ili kuhakikisha matokeo ya mwisho yanakuwa sahihi, halali na yanayokubalika na pande zote.


“Hatua na taratibu hizi ndizo msingi wa uchaguzi huru na wa haki, ambao hupunguza au kuondoa kabisa malalamiko au vurugu wakati wa mchakato wa uchaguzi,” amesisitiza


Akizungumza wakati akifunga mafunzo hayo Mgeni rasmi, Bi. Mona S. Bitakwate, amewataka watafsiri mafunzo hayo kwa kuhusianisha na zoezi la upigaji kura. Amesema kuwa mafunzo haya yamewajengea uwezo washiriki na kuwakumbusha umuhimu wa kutunza siri, kwa mujibu wa kiapo walichoapa chini ya sheria. Pia amewasisitiza kupunguza matumizi ya makundi ya WhatsApp ili kuepuka makosa yatakayoweza kusababisha taarifa za siri kuvuja.

Aidha, amehitimisha kwa kusisitiza kufuata muda wa kufungua na kufunga vituo vya kupigia kura, kufanya kazi kwa uzalendo na weledi, kushirikiana vizuri kazini, kutumia lugha nzuri, na kuwapa kipaumbele wapiga kura wenye mahitaji maalum watakapofika vituoni.


Kwa ujumla, mafunzo haya ni ushahidi wa dhamira ya dhati ya Tume ya Uchaguzi kuandaa watendaji wake kwa ufanisi, kuhakikisha kila hatua ya uchaguzi inatekelezwa kwa weledi na uadilifu. Huu ni msingi imara wa kujenga uchaguzi huru, haki na wenye kuaminika — nguzo muhimu ya demokrasia ya Tanzania.


Matangazo

  • TAARIFA YA MTIRIRIKO WA FEDHA KWA KIPINDI KILICHOISHIA TAREHE 30 JUNE. 2022 August 14, 2023
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI November 03, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MFAMASIA December 14, 2021
  • Orodha ya Walioitwa kwenye Usaili September 20, 2024
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI

    November 21, 2025
  • WATUMISHI KISHAPU WAPEWA MAFUNZO YA ELIMU YA FEDHA NA KUKABILIANA NA CHANGAMOTO YA AFYA YA AKILI

    November 20, 2025
  • DC,DED NA MSIMAMIZI WA UCHAGUZI JIMBO LA KISHAPU WAUNGANA NA WANANCHI KUPIGA KURA

    October 29, 2025
  • WASIMAMIZI WA VITUO KISHAPU WAONYWA KUTOKUWA CHANZO CHA MIGOGORO

    October 27, 2025
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa