• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
    • Idara
      • Fedha
      • Rasilimali watu
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii

CCM YAIBUKA KIDEDEA JIMBO LA KISHAPU

Posted on: October 29th, 2020

Katika Uchaguzi mkuu wa Rais, Ubunge na Udiwani wa Oktoba 28, 2020 Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeibuka kidedea katika ngazi ya Ubunge Jimbo la Kishapu.

Matokeo hayo yametangazwa na Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Kishapu Emmanuel Johnson leo Oktoba 29 ambapo Boniphace N. Butondo  kutoka Chama Cha Mapinduzi  (CCM) ameibuka kinara kwa idadi ya kura 54, 864 kutoka katika kata zote 29 za jimbo la Kishapu,  huku Idd Salum Amri wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) akifuatia kwa kupata kura 9,903.    

Msimamizi huyo  amempongeza Mbunge huyo huku akimtakia mafanikio mema katika kulitumikia taifa na kutatua kero za wananchi wa Kishapu.     

“Kwa mamlaka niliyopewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Namtangaza Mheshimiwa Boniphace Butondo kwa kuchaguliwa kuwa Mbunge mteule wa Jimbo Kishapu katika uchaguzi uliofanyika tarehe 28 Oktoba 2020” Amesema Johnson alipokuwa akimtangaza mbunge huyo.

 Katika uchaguzi huo idadi ya wapiga kura walioandikishwa ni 155,785, huku idadi halisi ya wapiga kura ikiwa ni 66,422, idadi ya kura halali ikiwa ni 64,764na idadi ya kura zilizokataliwa ni 1,655.           

Naye Mshindi wa uchaguzi huo Mheshimiwa Boniphace Butondo amewashukuru sana wananchi wote waliomchagua kuwa Mbunge wa Jimbo la Kishapu na kuahidi mara maada ya kuapishwa na kuwa mbunge ramsi atawatumikia kwa moyo mmoja.

“Nawashukuru kwa moyo wangu, wote waliojitokeza kupiga kura na kunichagua katika nafasi hii. Mmeonyesha upendo wa hali ya juu kwangu, naahidi kurudisha fadhila hizi kwa kuwatumikia ipasavyo. ”amesema Mheshimiwa Butondo.     

 Aidha katika uchaguzi huo nafasi za Madiwani katika kata zote 29 za Jimbo la Kishapu zimechukuliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM.   

                                                                                               

Matangazo

  • Tangazo la kazi kada ya Afya December 12, 2018
  • Majina ya walioitwa kwenye usaili nafasi ya watendaji May 10, 2018
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • Wanafunzi Waaswa Kusoma kwa Bidii Wakizingatia Uzalendo

    January 11, 2021
  • Wachimbaji wadogo wa madini waliovamia eneo la Mgodi wa Al-Hilal watakiwa kuondoka.

    January 21, 2021
  • Milioni 42.6 kutoka mfuko wa Jimbo kuendeleza ujenzi Madarasa na Maabara.

    January 17, 2021
  • Ziara ya Mkuu wa Wilaya ya Kishapu kukagua mradi mkakati wa ujenzi wa vyumba vya madarasa.

    January 13, 2021
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu:

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa