• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
    • Idara
      • Fedha
      • Rasilimali watu
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii

Wakulima wa Pamba Kishapu Waishukuru Serikali

Posted on: December 28th, 2020

Wakulima wa zao la pamba wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga wameishukuru serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli kupitia uongozi wa Halmashauri ya Wilaya a Kishapu kwa kuwapatia kwa mkopo dawa za kuulia wadudu waharibifu ambapo kwa sasa wataepukana na mikopo umiza waliyokuwa wakitozwana watu binafsi.

Shukrani hizo zimetolewa mwishoni mwa wiki iliyopita na wanachama wa Chama cha Ushirika cha Msingi cha Kishapu (AMCOS) wilayani Kishapu wakati wa uzinguzi wa ugawaji wa viutilifu vilivyotolewa kwa mkopo na Bodi ya Pamba Tanzania (TCB) Kanda ya Magharibi.

Wakulima hao walisema uamuzi wa serikali kuwapatia dawa za kuulia wadudu kwa njia ya mkopo utaongeza ufanisi katika shughuli zao za kilimo na hawatahangaika tena kutafuta viuatilifu hivyo kutoka kwa watu binafsi wanaowatoza riba kubwa na kusababisha washindwe kunufaika na kilimo chao.

Mmoja wa wakulia hao, Ally Mfaume alisema kitendo cha serikali kuwakumbuka wakulima kwa kuwapatia viuatilifu hivyo itawasaidia wakulima kuepuka changamoto ya pembejeo hivyo watapulizia dawa mapema katika pamba zao tofauti na msimu uliopita.

“Mwanzo tulikuwa tunaingia mkataba na wafanyabiashara binafsi kwa sharti bada ya mavuno kuwalipa pamba mbegu, kwa mfano mtu unapewa gunia mbili za pamba sawa na kilo mia moja kalini ukivuna unatakiwa umpatie aliyekukopesha kilo mia mbili za pamba”

“Kwa kweli tulikuwa tunapata hasara, kilo mia mbili ni nyingi sana, ukizipunguza kwenye mavuno yako mkulima unajikuta unapata hasara. Lakini kwa utaratibu huu wa kukopeshwa na serikali tutaepukana na mikopo kandamzi, na tunaomba hii huduma iwe endelevu, maana uwezo wa kulipa tunao” alieleza Mfaume.

Akwa upande wake mgeni rasmi katika ugawaji wa viuadudu hivyo, David Isanga aliyemwakilisha mkuu wa wilaya ya Kishapu Nyabaganga Taraba amewatahadharisha viongozi wa Kishapu AMCOS kutofanya udanganyifu wa aina yoyote katika zoezi la ugawaji wa viuadudu hivyo kwa wakulima.

Matangazo

  • Tangazo la kazi kada ya Afya December 12, 2018
  • Majina ya walioitwa kwenye usaili nafasi ya watendaji May 10, 2018
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • Wanafunzi Waaswa Kusoma kwa Bidii Wakizingatia Uzalendo

    January 11, 2021
  • Wachimbaji wadogo wa madini waliovamia eneo la Mgodi wa Al-Hilal watakiwa kuondoka.

    January 21, 2021
  • Milioni 42.6 kutoka mfuko wa Jimbo kuendeleza ujenzi Madarasa na Maabara.

    January 17, 2021
  • Ziara ya Mkuu wa Wilaya ya Kishapu kukagua mradi mkakati wa ujenzi wa vyumba vya madarasa.

    January 13, 2021
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu:

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa