DC MKUDE AWASIHI WATANZANIA KUENDELEA KUUENZI NA KUULINDA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR VIZAZI NA VIZAZI
Mkuu wa Wilaya Kishapu Mhe. Joseph Mkude, amewasihi Watanzania kuendelea kuuenzi na kuulinda Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwa vizazi vyote, ili kuendelea kufurahia Amani, Mshikamano na Umoja ulioachwa na Waasisi wa Muungano huo.
Waasisi wa Muungano ni Hayati Abeid Amani Karume ambaye alikuwa Rais wa kwanza Zanzibar,pamoja na Hayati Julius Kambarage Nyerere alikuwa Rais wa kwanza Tanganyika, ambao waliunganisha nchi hizo mbili kuwa moja tarehe 26/4/ 1964 na kuitwa Tanzania. Mkude amezungumza hayo leo April 25,2024,ikiwa ni siku moja kabla ya kusherehekea Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar hapo kesho,kwenye Mdahalo wa Muungano uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu ulioambatana Sambamba na Dua na Maombi kutoka Madhehebu ya Kiislamu na Kikristo.
Amesema Watanzania wanapo Sherehekea miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, hawana budi kuwaenzi viongozi ambao ni Waasisi wa Muungano huo, kwa kuendelea kudumisha Amani,mshikamano,upendo na umoja, ili nchi iendelee kuwa tulivu na kusongambele kimaendeleo. "Muungano huu wa Tanganyika na Zanzibar umekuwa na faida kwetu, umejenga taifa moja,lenye watu wamoja wanazungumza lugha moja, na hata kufanya kazi na kushika Madaraka kwa nchi zote mbili bila ya ubaguzi, na kufanya biashara bila ya mipaka," amesema Mkude .
Aidha,amesema kupitia Muungano huo hali ya ulinzi na usalama inaendelea kuimarika kwa pande zote mbili, na Amani kuendelea kutawala, huku akiwapongeza Marais wote hadi wa sasa Dk.Samia na Husein Mwinyi kwa kuendelea kuuenzi na kuulinda Muungano. Nao Wazee wilayani Kishapu akiwamo Alexander Manyesha na Felista Masanja, wamesema Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, amesaidia sana kudumisha Amani ya Tanzania hasa katika suala la ulinzi.
Wamesema Watanzania wanapaswa kuendelea kudumisha Muungano na wasije wakajaribu kuuvuruga, sababu ndiyo Tunu ya Amani, ndiyo maana hadi leo nchi ya Tanzania hakujawahi tokea Vita tangu kupatikane kwa Uhuru. Kauli Mbiu katika Sherehe za Muungano Mwaka huu 2024 inasema"Miaka 60 ya Muungano wa Tanzania,tumeshikamana,tumeimarika kwa maendeleo ya Taifa letu."
TAZAMA PICHA HAPA CHINI
Halmashauri ya Wilaya Kishapu
Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU
Simu ya mezani: +255282770020
Simu:
Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz
Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa