Balozi wa Pamba nchini Tanzania msimu wa mwaka 2022-2023 Bwana Agrey Mwanri amesema hata sita kuwachukulia hatua viongozi ambao hawatatimiza wajibu wao wa kusimamia wakulima wa zao la pamba kulima kwa kufuata sheria katika maeneo yao katika kamati teule ya waziri wa kilimo ya zao la pamba.
Mwanri amesema hayo leo Januari 9, 2023 katika kikao kazi maalum cha kujengeana uwezo kilichowakutanisha watendaji wa vijiji,wenyeviti wa vijiji,maafsa ugani pamoja na baadhi ya watumishi wa serikali ngazi ya halmashauri na wilaya katika ukumbi wa Shirecu wilayani Kishapu mkoani Shinyanga.
“Wakati mwingine kutowajibika kwenu vizuri kunapelekea wakulima kulima kiholela, zao la pamba lipo kwa mjibu wa sheria za nchi na sio kienyeji sheria no.2 ya mwaka 2001 na ile ya 2011 zilitungwa kanuni 10 moja wapo ya kanuni inamtaka kila mkulima kung’oa na kuchoma maotea yoote ya msimu uliopita ili kuua wadudu waharibifu kuhamia kwenye msimumpa,kupanda kwa msitari pamoja na kupulizia dawa ya kuuwa wadudu”
Ameongeza kuwa wilaya ya kishapu na maswa kata ya Itilima bado kunauelewa mdogo juu ya kulima kilimo chenye tija jambo lililopelekea waanzishe kuwepo mkulima mwezeshaji ambae atakuwa ni chambo kwa wakulima wengine,kutoa elimu ya kutosha huku akiwaasha viongozi wawe mfano katika zao hilo kwa kwa kufanya hivo kutainua na kuongeza pato la mtu mmoja na taifa ikilinganishwa na mwaka 2021-2022.
Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati ya ugawaji na usambazaji viuadudu na vinyunyizi Bw Joseph Bukalasa alisema kamati hiyo yenye watu 10 kutoka taasisi mbalimbali za serikali imeundwa kwa maelekezo ya waziri wa kilimo Mhe. Husein Bashe yenye lengo la kudhibiti na kuzuia uchepushaji wa upotevu pamoja na udhibiti ubora baada ya kupokea kutoka kwa mdhabuni kwenda kwa mkulima.
Aidha katibu tawala wa wilaya ya Kishapu Bw Shadrack Tengese alisema kuwa ukosepfu wa uadilifu katika kazi unapelekea uzembe ndani ya baadhi ya vyama vya msingi na kusababisha washindwe kufikia malengo yaliyokusudiwa katika zao hilo la pamba.
“Kwa bahati mbaya mikataba haioneshi kama kiongozi wa amkosi akikosea atawajibika vipi mdhamini wake japo tutafika tuendako, maafisa ugani tusimamie kanuni za kilimo kwenye maeneo yetu iwapo wakulima kila siku wanamwaga mbegu na wewe uko pale je unastahili kuwepo pale? Kila mtu akisimamia kazi yake vizuri tutakuwa tumemsaidia Mhe. Raisi kufikia malengo yale ambayo amekusudia katika sekta ya kilimo. ndugu zangu yamkini nimesema kwa ukali lengo hapa ni kumtaka kila kiongozi kutimiza wajibu wake”
Hata hivyo wake afisa uchunguzi wa kuzuia na kupambana na rushwa kutokea jijini Mwanza Bw Protas Henry ambae pia ni mjumbe wa kamati ya usambazaji pembejeo alisema kuwa lengo la serikali ni kuinua zao la pamba na wataalamu wamethibitisha kwa mkulima atakaefanya vizuri na kuzingatia kanuni mavuno yataongezeka
“Lengo la serikali msimu wa 2022-2023 ni kuzalisha tani 500000 kutoka tani 17300 Kishapu inatakiwa kuzalisha jumla ya tan 50,000 na hili tutafanikiwa baada ya wakulima kulima mapema,kupalilia na viuwadudu na vinyunyizi kufika kwa wakati kwa walengwa na sisi kama kamati tutasimamia vema kugawa na kusimamia mtiririko wa ugawaji kwanzia ngazi ya wilaya,amkosi hadi kwa mkulima ili uzalishaji uweze kuongezeka, kwa yeyote atakaeenda kinyume na sheria hatutasita kumchukulia hatua stahiki”
Hata hivyo wilaya ya Kishapu msimu wa kilimo 2021/2022 haikufikia malengo ya kulima hekali 100,000 kutokana na upungufu wa mvua,upungufu wa vinyunyizi kwa wakulima hivyo kutokana na kampeini ya balozi wa pamba ya octoba 2022 wakulima wameendelea kupewa elimu ya kutosha kukabiliana na changamoto hizo huku wakikusudia ongezeko kubwa la wakulima wa pamba kwa msimu wa 2022/2023.
Balozi wa Pamba nchini Tanzania Agrey Mwanri akizungumza kwenye Kikaoo
Kikaoo cha Pamba kikiendelea
Katibu Tawala wilaya ya Kishapu Ndugu. Shadrack Kengese akizungumza kwenye Kikaoo
Halmashauri ya Wilaya Kishapu
Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU
Simu ya mezani: +255282770020
Simu:
Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz
Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa