• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
    • Idara
      • Fedha
      • Rasilimali watu
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
  • Machapisho
    • Fomu za kujinga na Kidato cha Tano
      • Shule ya Sekondari Kishapu
      • Shule ya Sekondari Shinyanga
    • Mpango wa bajeti wa mwaka 2021/2022
    • MATANGAZO
  • Madiwani

MKUU WA MKOA WA SHINYANGA AWAKUMBUSHA WATUMISHI WAJIBU WAO.

Posted on: May 1st, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme amewakumbusha Watumishi  juu ya wajibu wao katika uwajibikaji wa kweli kwenye majukumu yao ili kuleta maendeleo yenye tija Serikalini.


Mhe. Mndeme ameyasema hayo leo 01.05.2023 akiwa Mgeni Rasmi  katika sherehe za Maadhimisho ya Mei Mosi ambayo ki Mkoa, yamefanyika katika Uwanja wa Mwadui, Wilaya ya Kishapu yakiwa na KAULI MBIU: Mishahara Bora na Ajira za staha ni Nguzo kwa Maendeleo ya Wafanyakazi. Wakati ni sasa.


Aidha amewakumbusha juu ya kulinda Maadili ya kitanzania, ambapo amewaeleza kuwa Tanzania kama Nchi tuna maadili na tamaduni zetu tulizorithi kutoka kwa mababu zetu na viongozi wetu huku akiwataarifu kuwa Mkoa wa Shinyanga umeanzisha Kampeni ijulikanayo kama DON'T TOUCH ME, HAPA NI KWANGU ambayo inalenga kuwaelimisha watu wote na kwamba elimu hii iende mpaka kwa familia.


" Wakati tunasherehekea Maadhimisho haya, pamoja na kuipongeza sana Serikali yetu lakini tujiandae kuipokea Kampeni hii ambapo itakwenda mpaka ngazi ya familia ambapo tuwafundishe watoto na tunaowalea kukataa kabisa tabia zote zisizokuwa na maadili na wawe tayari kusema DON'T TOUCH ME, HAPA NI KWANGU pia mkumbuke uwajibikaji na maadili yetu pamoja na kuthamini Ulinzi na Usalama ambapo wenyeviti wetu wasiruhusu mtu kuingia maeneo yao kama hajulikani na ikitokea watoe taarifa kwa Mamlaka za Usalama," alisema Mhe. Mndeme.



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MFAMASIA December 14, 2021
  • RATIBA YA UFANYAJI MAZOEZI KWA KILA WIKI August 16, 2021
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • WANANCHI KISHAPU WATAKIWA KUPAZA SAUTI KUHUSU MMONYOKO WA MAADILI

    May 15, 2023
  • BARAZA LA MADIWANI LA MPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA UKUSANYAJI MZURI WA MAPATO YA NDANI.

    May 10, 2023
  • WAZIRI JAFO APONGEZA MIRADI ILIYOTEKELEZWA

    May 06, 2023
  • RC MNDEME AMEAGIZA UJENZI WA BWAWA JIPYA LA MGODI WA ALMASI MWADUI LIJENGWE KWA KIWANGO BORA

    May 02, 2023
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu:

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa