• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
    • Idara
      • Fedha
      • Rasilimali watu
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
  • Machapisho
    • Fomu za kujinga na Kidato cha Tano
      • Shule ya Sekondari Kishapu
      • Shule ya Sekondari Shinyanga
    • Mpango wa bajeti wa mwaka 2021/2022
    • MATANGAZO
  • Madiwani

MWENGE WA UHURU UMERIDHISHWA NA MIRADI KISHAPU.

Posted on: July 27th, 2023

Mwenge wa uhuru umezindua na kuweka mawe ya msingi miradi mbalimbali ya maendeleo wilayani Kishapu, huku wananchi wakihimizwa kutunza Mazingira pamoja na vyanzo vya maji.

Kauli mbiu ya mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka huu (2023) inasema' Tunza Mazingira,Okoa vyanzo vya maji kwa Ustawi wa viumbe Hai kwa uchumi wa Taifa.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Christina Mndeme amemkabidhi Mwenge wa Uhuru Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Josephe Modest Mkude kwa ajili ya kuukimbiza wilayani Kishapu na kuipitia Miradi mbalimbali ya maendeleo na kuzinduliwa, mara baada ya kumaliza kuupokea kwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Dk,Yahaya Nawanda.

Mwenge wa Uhuru katika Mkoa wa Shinyanga, umeanza kukimbizwa leo wilayani Kishapu kwa umbali wa kilomita 118 pamoja na kuifikia Miradi Sita yenye thamani ya Sh.bilioni 1.3.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Abdalla Shaib Kaim, amesema ameridhika na miradi hiyo ya maendeleo wilayani Kishapu, na yote ameizindua hakuna hata mmoja ambao umekataliwa, huku akiwataka wananchi watunze mazingira na vyanzo vya maji.

"Tunampongeza Rais Samia kwa kutoa fedha na kutekelezwa miradi mbalimbali ya maendeleo, na leo nimeikagua na kuizindua tumpongeze sana Rais wetu,"amesema Karim.

Aidha, akiwa katika upanuzi wa Mradi wa Maji ya Ziwa Victoria wa Maganzo- Masagala, amesema mradi huo ni muhimu sana katika kutatua Changamoto ya wananchi kufuata maji safi na salama umbali mrefu pamoja na kumtua ndoo kichwani Mwanamke.

Naye Mbunge wa Kishapu Boniphace Butondo, amempongeza Rais Samia kwa kutoa fedha nyingi jimboni humo na kutekelezwa miradi mingi ya Maendeleo ikiwamo hiyo ya Maji.

Miradi ya maendeleo ambayo imepitiwa na Mwenge wa Uhuru kuwa ni Barabara ya Buganika- Kabila Kilomita 11, vyumba viwili vya Madarasa na vyoo Sita katika shule ya Msingi ya Awali Idukilo.

Miradi mingine ni Kituo cha Afya Negezi, Mradi wa Maji Maganzo- Masagala, Mradi wa kuhifadhi Mazingira na vyanzo vya Maji katika Bwawa la Songwa, Klabu ya wapinga Rushwa Shule ya Sekondari Maganzo na kuweka jiwe la Msingi Stendi ya Maganzo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MFAMASIA December 14, 2021
  • RATIBA YA UFANYAJI MAZOEZI KWA KILA WIKI August 16, 2021
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • TANGAZO LA AJIRA

    September 11, 2023
  • MWENGE WA UHURU UMERIDHISHWA NA MIRADI KISHAPU.

    July 27, 2023
  • SHUGHULI ZA UZALISHAJI KATIKA MGODI WA MWADUI ZA ZINDULIWA

    July 17, 2023
  • WAZIRI WA MADINI DOTTO BITEKO ATEMBELEA MGODI WA ALMASI MWADUI

    June 30, 2023
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu:

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa