Mwenyekiti wa Hamashauri ya Wilaya ya Kishapu, Mhe. William Luhende Jijimya amewapongeza Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu kwa kufuatilia changamoto za wananchi.
Mhe. Jijimya amewapongeza madiwani hao wakati wa mkutano wa baraza la madiwani wa kujadili taarifa za kata leo Novemba 1, 2022.
"Niwapongeze waheshimiwa Madiwani kwa kuendelea kutatua changamoto ambazo zipo kwenye kata zetu, msichoke kuleta changamoto za wananchi na tuzisimamie ziendelee kutatuliwa, kwa taarifa hizi mlizoziwasilisha inaonyesha kabisa mnafatilia kwa ukaribu na mnazifahamu changamoto zilizopo kwa Wananchi," ameeleza.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Ndg. Emmanuel Johnson amewaeleza madiwani kuwa ofisi yake ipo tayari kusimamia na kutatua changamoto.
"Niwahakikishie kwamba ofisi yangu itasimamia kuhakikisha tunafatilia changamoto moja moja kuhakikisha tunazitatua kadri ya uwezo na mapato ya Halmashauri, na kwa changamoto ambazo zinahitajika kufikishwa katika Serikali kuu ambazo zimeelekezwa ofisini kwangu, tutazifanyia kazi"
Aidha, Katibu Mwenezi wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Kishapu Ndg. Jiyenze Seleli amewataka madiwani wazidi kufuatilia changamoto za wananchi na kusisitiza kuwa wasikate tamaa katika kutatua changamoto za wananchi kwa kuwa wamefunga mkataba nao.
MMkurugenzi mtendaji Halmashauri ya Kishapu Ndg. Emmanuel Johnson akizungumza mbele ya baraza la Madiwani
Madiwani wakiwa kwenye mkutano
Wataalamu wakiwa kwenye mkutano
Diwani wa kata ya Mwadui Luhumbo akiwasilisha Taarifa
Halmashauri ya Wilaya Kishapu
Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU
Simu ya mezani: +255282770020
Simu:
Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz
Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa