• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
    • Idara
      • Fedha
      • Rasilimali watu
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
  • Machapisho
    • Fomu za kujinga na Kidato cha Tano
      • Shule ya Sekondari Kishapu
      • Shule ya Sekondari Shinyanga
    • Mpango wa bajeti wa mwaka 2021/2022
    • MATANGAZO
  • Madiwani

NI RUKUSA KUSOMA BILA SARE ZA SHULE

Posted on: March 2nd, 2023

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kishapu Emmanuel Johnson, amesema katika halmashauri yake wanafunzi wote ambao wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza wanapaswa kuripoti shuleni bila kujali hawana Sare za Sekondari, bali waende hata na Sare za Shule ya Msingi, ili wakaanze masomo wakati taratibu zingine zikiendelea za kununuliwa Sare za Sekondari.

Johnson amebainisha hayo leo Marchi 2, 2023 wakati alipotembelea Shule ya Sekondari Isoso wilayani humo kuona mahudhurio ya wanafunzi wa kidato cha kwanza na kukuta mahudhurio ni mazuri, ambapo wamesalia wanafunzi wawili tu ambao ndiyo hawajaripoti shule, huku wengine wakiwa darasani na Sare za shule ya Msingi.

Amesema katika Halmashauri hiyo ya wilaya ya Kishapu hadi sasa wamefikisha asilimia 98.17 ya wanafunzi wa kidato cha kwanza ambao wamesharipoti shule, na kuagiza wale ambao wamesali hadi kufikia Marchi 29 mwaka huu, wawe wamesharipoti shule hata kama hawana Sare za Sekondari bali wavae za Shule ya Msingi ili wasiendelee kukosa masomo.

“Natoa wito kwa wazazi wapeleke watoto wao shule ambao wamefaulu kujiunga na kidato cha kwanza hata kama hawana Sare za Sekondari bali wavae za Shule ya Msingi, ili waendelee na masomo, na sisi Halmashauri tutaona namna ya kuwasaidia kwa kuwanunulia Sare ili wafanane na wenzao,”amesema Johnson.

“Leo nimetembelea hapa Shule ya Sekondari Isoso na nimekuta wanafunzi wawili wa kidato cha kwanza wakiendelea na masomo yao huku wakiwa wamevaa Sare za Shule ya Msingi nimependa ujasiri wao wakupenda masomo, na mimi nimetoa fedha ili wakanunue Sare za Sekondari na kufanana na wenzao, na nitafanya hivyo kwa shule zote ambazo nitakuta wanafunzi hawana Sare za Sekondari,” ameongeza.


Aidha, amesema pia hali ya uandikishaji watoto darasa la awali wamefikisha asilimia 101, na uandikishaji darasa la kwanza wamefikisha asilimia 108, kidato cha kwanza asilimia 98.17.


Naye Afisa Elimu Sekondari Halmashauri ya wilaya ya Kishapu David Mashauri, amesema kwa wanafunzi ambao wamesalia kuripoti shule wa kidato cha kwanza watawasaka wote kwa kushirikiana na viongozi wa vitongoji, vijiji na Kata ili waanze masomo mara moja na kuungana na wenzao.

Nao wanafunzi ambao wamekutwa wakisoma na Sare za Shule ya Msingi, wamemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kujenga miundombinu ya shule ili wapate elimu katika mazingira Rafiki, pamoja na Mkurugenzi wa Kishapu Emmanuel Johnson kutoa pesa na kuwanunulia Sare za Shule ya Sekondari na kuahidi watasoma kwa bidii na kutimiza ndoto zao.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MFAMASIA December 14, 2021
  • RATIBA YA UFANYAJI MAZOEZI KWA KILA WIKI August 16, 2021
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA YA KISHAPU AFANYA ZIARA YA KUSHITUKIZA SEKE- IDIDI

    March 22, 2023
  • DC MKUDE ATOA MAELEKEZO ULIPAJI FIDIA WAHANGA WA TOPE LA MGODI WA MWADUI

    March 21, 2023
  • DC MKUDE AKABIDHI PIKIPIKI KWA MAOFISA UGANI NA WATENDAJI WA KATA

    March 09, 2023
  • SHULE YA SEKONDARI BUSIYA YA PATA MSAADA WA SARUJI MIFUKO 140

    March 08, 2023
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu:

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa