• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
    • Idara
      • Fedha
      • Rasilimali watu
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
  • Machapisho
    • Fomu za kujinga na Kidato cha Tano
      • Shule ya Sekondari Kishapu
      • Shule ya Sekondari Shinyanga
    • Mpango wa bajeti wa mwaka 2021/2022
    • MATANGAZO
  • Madiwani

RC SHINYANGA AUPONGEZA UONGOZI WA MGODI WA ALMASI MWADUI KWA KUSAINI MKATABA WA KUBORESHA MASIRAHI YA WAFANYAKAZI.

Posted on: November 4th, 2022


Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Sophia Mjema ameupongeza uongozi wa mgodi wa madini ya almasi Mwadui Williamson Diamod (WLD) kwa kutia saini mkataba wa hali bora ya wafanyakazi, ikiwa ni pamoja na kuboresha masirahi ya wafanyakazi wa kampuni hiyo, 


Pongezi hizo amezitoa leo wakati akishuhudia utiaji saini mkataba wa hali bora ya wafanyakazi wa kampuni hiyo ulifanyika katika viwanja vya Mwadui, ambapo amefurahishwa sana na kampuni ya Williamson kwa kuwathamini wafanyakazi  na kuweza kuwaboreshea masirahi yao.


Mjema amesema kwa hicho kilichofanyika leo anaitaka na migodi mingine, taasisi mbalimbali ziboreshe masrahi ya wafanyakazi wake ili waweze kufanya kazi kwa bidii na kwa ufanisi zaidi na kwa kutimiza matakwa ya wafanyakazi.


,"Bila wafanyakazi kuboreshewa masirahi yao hali ya kufanya kazi inakuwa ni ya kusua sua, lakini  akiboreshewa anakuwa na mori ya kuweza kufanya kazi, hivyo tunakushukuru sana meneja  wa mgodi huu kwa sababu unamuunga mkono Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Samia Suluhu, hivyo na taasisi zote zihakikishe zinawa mikataba wafanyakazi wake,"amesema Mjema.


,"Hakikisheni mnafanya kazi kwa weledi mkubwa na kupendana kwa sababu mmeboreshewa masilahi yenu, pia mhakikishe,  mnasainiwa na kamishina  wa kazi ili uanze kufanya kazi mara moja, kwani mkataba huu una lengo la kukuza fursa na kuboresha utendaji wa kazi,"amesisitiza Mjema.


Aidha Mjema  amewataka wahakikishe wageni wote wanaofika katika kampuni wanakuwa na vibali maalumu vya kufanya kazi kwa kanuni na sheria ya nchi,"amesema mkuu wa mkoa Mjema.


Kwa upande wake meneja mkuu wa mgodi wa WLD mhandisi Ayubu Mwenda amesema ni muda mrefu hawakuwa na mkataba wa namna hiyo kwa sababu ya ugonjwa wa Covid 19, lakini kwa vile alikuwa na malengo ya kuboresha maisha ya wafanyakazi pamoja na kuboresha mahusiano na majirani pamoja na serikali amelitimiza lengo hilo.


"Baada ya kuingia hapa tulikubaliana na wafanyakazi kuwa tutaboresha masirahi ya wafanyakazi, na pia tusisahau kwamba shughuli za uzalishaji zikiongezeka ndio itatuwezesha kuwa na mchango kwenye uchumi wa nchi, mkoa, wilaya na kwenye vijiji vinavyotuzunguka michango itaongezeka zaidi,"amesema.


Naye katibu mkuu wa chama cha wafanyakazi wa migodi TAMICO Lukas Bujashi amesema kupitia mkataba wa hali bora tutaenda kuboresha zaidi wanaamini baada ya miaka mitatu mkataba huo utaendelea, hivyo wafanyakazi waliokengeuka wakaenda kusikojulikana  warudi kwenye vyama vya wafanyakazi.


,"Sisi tunaamini mkataba huu utaleta ufanisi zaidi kwa wafanyakazi na hamasa kubwa, hivyo tutaweza kumshawishi mwajili tuendelee katika kiwango cha juu, hivyo wafanyakazi waliokengeuka rudini kwenye shina, hivyo leo tamico inashukuru kwa tukio hili tunaheshimu majadiliano, kwani mkataba huu utadumu kwa muda wa miaka mitatu,"amesema Bujashi


Akisoma risala katibu tawi Gatti Raphael amesema anaishukuru kampuni hiyo kwakuthamini wafanyakazi wake, kwani hata baada ya kutokea ugonjwa wa Covid 19 haikupoteza hata mfanyakazi mmoja wameshukuru kwa kuwapatia mkataba hivyo wamesema watafanya kazi kwa weledi na kwa bidii kwa sababu wameboreshewa masirahi yao.




Mkuu wa mkoa wa Shinyanga   Sophia Mjema akionyesha keki iliyoandaliwa na wafanyakazi wa mgodi huo 



Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Shinyanga Janeth Magomi akilishwa keki na mfanyakazi wa mgodi huo




Mfanyakazi wa mgodi wa WLD akiandaa keki



Mkuu wa mkoa na viongozi wenzake wakiibariki keki kabla ya kukata



Meneja wa mgodi wa WLD akiwa na katibu wa kanda wakisaini mkataba wa wafanyakazi


Mkuu wa mkoa wa Shinysnga Sophia



Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Sophia  Mjema akishuhudia wakisaini mkataba wa wafanyakazi wa mgodi ws



Mfanyakazi akimlisha keki meneja wa mgodi wa WLD


Meneja wa mgodi wa WLD  na katibu wa kanda TAMICO wakionyesha mikataba hiyo baada ya kusaini






Meneja wa mgodi wa WDL mhandisi Ayubu Mwenda akizungumza 











Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MFAMASIA December 14, 2021
  • RATIBA YA UFANYAJI MAZOEZI KWA KILA WIKI August 16, 2021
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • DC MKUDE ATEMBELEA MGODI WA MWADUI KUJIONEA HATUA ZILIZOCHUKULIWA BAADA YA BWAWA LA MAJI TOPE KUBOMOKA

    January 23, 2023
  • BARAZA LA MADIWANI KISHAPU LAPITISHA MPANGO WA BAJETISH BILIONI 39.4 KWAAJILI YA MAENDELEO

    January 20, 2023
  • KISHAPU YAADHIMISHA MIAKA 59 YA MAPINDUZI ZANZIBAR KWA KUPANDA MITI

    January 12, 2023
  • BALOZI WA PAMBA NCHINI TANZANIA AWATAKA VIONGOZI KUSIMAMIA WAKULIMA WA ZAO LA PAMBA

    January 09, 2023
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu:

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa