Mkurugenzi mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu Ndg. Emmanuel Johnson leo amepokea kombe la mabingwa wa mchezo wa Karata walioshinda katika Mashindano ya Shirikikisho la Michezo kwa Serikali za mitaa (SHIMISEMITA) yaliyofanyika Mwaka huu katika Mkoa wa Morogoro
Akikabidhi Kombe hilo leo tarehe 07 Novemba 2022 Afisa Utamaduni na Michezo wilaya ya Kishapu Bi. Queen Mwajilala, Kwa mkurugenzi mtendaji alisema Mashindano yalianza tarehe 19-31 October 2022 huku Kishapu DC ikiwa na timu tatu Volleyball, Handball na karata timu za Volleyball na Handball zilifanikiwa kutinga katika hatua ya Nusu Fainali huku timu ya mchezo wa karata ikifanikiwa kunyakuwa kikombe
Kwa Upande wake Mkurugenzi Mtendaji Ndg. Emmanuel Johnson amewapongeza sana wote walioshiriki Michezo hiyo na kuipatia Halmashauri ya Kishapu heshima ya kubeba ubingwa wa Karata
"Niwapongeze sana wale wote walioshiriki katika Michezo hii japo mpo wawakilishi matumaini yangu salamu hizi zitawafikia na washiriki wengine kikubwa mmeleta heshima kwenye Halmashauri yetu, niwakumbushe tu mwisho wa michezo ndiyo mwanzo wa maandalizi mengine jiandae kikamillifu kwa Michezo yote ikiwemo Football na Netball, Na mwakani ikiwezekana twende wengi zaidi" alisema
Viongozi wakikabidhi kombe kwa Mkurugenzi mtendaji
Halmashauri ya Wilaya Kishapu
Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU
Simu ya mezani: +255282770020
Simu:
Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz
Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa