• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
    • Idara
      • Fedha
      • Rasilimali watu
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
  • Machapisho
    • Fomu za kujinga na Kidato cha Tano
      • Shule ya Sekondari Kishapu
      • Shule ya Sekondari Shinyanga
    • Mpango wa bajeti wa mwaka 2021/2022
    • MATANGAZO
  • Madiwani

WANANCHI KISHAPU WATAKIWA KUPAZA SAUTI KUHUSU MMONYOKO WA MAADILI

Posted on: May 15th, 2023

Wananchi wa wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga wametakiwa kupaza sauti juu ya Mmomonyoko wa maadili na vitendo vya ukatili wa kijinsia, ikiwa ni pamoja na kukemea mabaya yote yasiendelee kutokea wilayani humo.

Agizo hilo limetolewa na mkuu wa wilaya ya Kishapu Joseph Mkude kwenye maadhimisho ya siku ya familia Duniani iliyofanyika leo Mei, 15, 2023 katika Kata ya Kishapu na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa maendeleo, viongozi wa Serikali, Chama, sambamba na utoaji wa elimu kuhusu kushuka kwa maadili kwa watoto.

Mkude ambaye alikuwa mgeni Rasmi kwenye maadhimisho hayo amewataka wananchi wilayani humo kukemea mabaya yote na kuwafundisha watoto kuhusu maadili mema ili wasijiingize kwenye vitendo visivyo faa katika jamii, na pia amewataka wananchi kupinga masuala ya Mila na Desturi zenye madhara ambazo zinaleta Maadili mabaya kwenye jamii.

"Kwanza kabisa natoa shukurani za dhati kwa serikali yetu chini ya Rais wetu Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutambua Jambo hili la familia na kuelekeza tufanye jambo hili kupitia Waziri Mkuu, ambalo tumeanzia, amesema Mkude.

"Tumeenda hospitalini tumekuta mambo mazuri tumekuta wababa wameleta watoto cliniki, ni jinsi gani inaonyesha upendo kwenye familia, hivyo ni wajibu wetu kuwafundisha watoto wetu maadili mema ili wakiwa wanakua wakue kwenye maadili yaliyo mazuri," amesema Mkude.

Diwani wa Kata ya Kishapu Joel Ndettoson amewataka Wananchi kuwapa Elimu watoto kuhusu Maadili mema na kuwakanya kuacha kujiingiza kwenye vitendo viovu ambavyo vinaweza kuwaletea madhara makubwa kwenye Maisha yao.

Kwa upande wake Afisa Ustawi wa Jamii wilaya ya Kishapu Mwajuma Liyanga amewata wazazi kuvunja ukimya kwenye Familia zao licha ya kuwa na majukumu mengi ambayo yanawabana kwa muda mwingi, amewasisitiza wazazi kuwa na muda wa kuzungumza na watoto na kuwaelekeza mambo mazuri ambapo itasaidia sana kwa watoto kuepuka mambo ambayo siyo mazuri kwao.

Hata hivyo Kauli Mbiu katika Maadhimisho hayo ilikuwa ni Imarisha Maadili na Upendo kwa Familia imara

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MFAMASIA December 14, 2021
  • RATIBA YA UFANYAJI MAZOEZI KWA KILA WIKI August 16, 2021
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • WANANCHI KISHAPU WATAKIWA KUPAZA SAUTI KUHUSU MMONYOKO WA MAADILI

    May 15, 2023
  • BARAZA LA MADIWANI LA MPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA UKUSANYAJI MZURI WA MAPATO YA NDANI.

    May 10, 2023
  • WAZIRI JAFO APONGEZA MIRADI ILIYOTEKELEZWA

    May 06, 2023
  • RC MNDEME AMEAGIZA UJENZI WA BWAWA JIPYA LA MGODI WA ALMASI MWADUI LIJENGWE KWA KIWANGO BORA

    May 02, 2023
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu:

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa