• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
    • Idara
      • Fedha
      • Rasilimali watu
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
  • Machapisho
    • Fomu za kujinga na Kidato cha Tano
      • Shule ya Sekondari Kishapu
      • Shule ya Sekondari Shinyanga
    • Mpango wa bajeti wa mwaka 2021/2022
    • MATANGAZO
  • Madiwani

WAZIRI JAFO APONGEZA MIRADI ILIYOTEKELEZWA

Posted on: May 6th, 2023

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Dkt. Seleman Jafo, ameeleza kuridhishwa na utekelezaji wa miradi ya kuhimili mabadiliko ya tabia nchi (EBARR) wilayani Kishapu.

Jafo amebainisha hayo leo Mei 6,2023 wakati alipofanya ziara wilayani Kishapu, kutembelea kuona utekelezaji wa miradi hiyo ya kuhimili mabadiliko ya tabia nchi.

Amesema katika ziara yake wilayani Kishapu ya kutembelea miradi hiyo ya kuhimili mabadiliko ya tabia nchi, ameridhika nayo baada ya kuona imetekelezwa vizuri, huku akiagiza kwa ile ambayo bado haijakamilika ikamilike haraka kabla ya mwaka wa fedha mwezi Julai iwe tayari na kuanza kutumika.


“Nimeridhika na ziara yangu hapa Kishapu nimeona miradi iko vizuri, na Rais Samia anapoona miradi ambayo anatoa fedha inatekelezwa vizuri anafarijika sana,”anasema Waziri Jafo.

“Naomba wananchi muitumie vyema miradi hii kwa tija, pamoja na kutunza mazingira kwa kupanda miti,”ameongeza.


Aidha, Miradi ambayo Waziri Jafo ameitembea ya kuhimili mabadiliko ya tabia nchi pamoja na mingine kuweka jiwe la msingi na kuzindua ni Mradi wa unenepeshaji Mifugo katika Kijiji cha Muguda, na kuweka jiwe la msingi katika jengo la kusaga mahidi na kukamua Alzeti, Bwawa la Maji Kijiji cha Kiloleli na Kiwanda cha kutengeneza bidhaa za ngozi vikiwamo viatu.


Miradi mingine ambayo inatekelezwa ni ujenzi wa Majosho, Majiko Banifu yatakayosaidia kupunguza matumizi ya kuni, ufugaji wa nyuki, na kilimo zao la Mkonge,


Anesema Serikali imetoa fedha kwa ajili ya kutekelezwa miradi hiyo ya kuhimili mabadiliko ya tabia nchi, ili wananchi wawe na shughuli mbadala za kufanya ambazo zitawaingizia kipato na kuacha kuharibu mazingira kwa kukata miti hovyo ikiwamo kufanya biashara za kuchoma mikaa.


Katika hatua nyingine Waziri Jafo, ameziagiza halmashauri zote hapa nchini kutekeleza agizo la upandaji miti Milioni 1.5 kwa kila mwaka, pamoja na kuihamasisha kampeni ya soma na mti ambayo kila mwanafunzi anapaswa kupanda mti.

Naye Mkuu wa wilaya ya Kishapu Joseph Mkude, amesema Serikali ilipeleka kiasi cha fedha Sh.bilioni 1.4 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo ya kuhimili mabadiliko ya tabia nchi. ambayo inatekelezwa katika Kata mbili ya Lagana na Kiloleli, na imekuwa na tija kwa wananchi katika suala zima la utunzaji wa Mazingira.

Nao baadhi ya wananchi ambao ni wanufaika wa miradi hiyo, wameishukuru Serikali kwamba licha ya kutunza mazingira, pia imekuwa ikiwasaidia kuwaingizia kipato na kuendesha maisha yao.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MFAMASIA December 14, 2021
  • RATIBA YA UFANYAJI MAZOEZI KWA KILA WIKI August 16, 2021
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • WANANCHI KISHAPU WATAKIWA KUPAZA SAUTI KUHUSU MMONYOKO WA MAADILI

    May 15, 2023
  • BARAZA LA MADIWANI LA MPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA UKUSANYAJI MZURI WA MAPATO YA NDANI.

    May 10, 2023
  • WAZIRI JAFO APONGEZA MIRADI ILIYOTEKELEZWA

    May 06, 2023
  • RC MNDEME AMEAGIZA UJENZI WA BWAWA JIPYA LA MGODI WA ALMASI MWADUI LIJENGWE KWA KIWANGO BORA

    May 02, 2023
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu:

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa