• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Utawala
      • Biashara, Viwanda na Uwekezaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya jamii
      • Afya
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Tehama
      • Utamaduni, Sanaa na Michezo
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Usafi wa Mazingira na Udhibiti Taka
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Kilimo na Mifugo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya picha na video za shughuli za maendeleo

DED JOHNSON ATOA MAELEKEZO MUHIMU KWA MADEREVA

Posted on: December 19th, 2025

Picha ya pamoja ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga, Emmanuel Johnso (wa nne kulia) na madereva wa Halmashauri hiyo katika kikao kazi maalum kilicholenga kuimarisha maadili ya kazi, uwajibikaji na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga Emmanuel Johnson amekutana na madereva wa Halmashauri hiyo katika kikao kazi maalum kilicholenga kuimarisha maadili ya kazi, uwajibikaji na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.


Akizungumza Disemba 19,2025 katika kikao hicho kilichofanyika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo,Mkurugenzi Johnson amesisitiza umuhimu wa madereva kuzingatia maadili ya kazi kuanzia kwenye matengenezo ya magari, matumizi sahihi ya rasilimali za Serikali pamoja na utunzaji wa vyombo vya usafiri wanavyovisimamia.

Ameeleza kuwa madereva wanapaswa kutambua nafasi yao muhimu katika utekelezaji wa majukumu ya Halmashauri, kufanya kazi kwa kujiamini, uaminifu na kwa kuzingatia taratibu na miongozo ya utumishi wa umma.

“Madereva ni sehemu muhimu ya mfumo wa utoaji huduma. Ni wajibu wenu kuhakikisha magari yanatunzwa vizuri, yanatumika kwa malengo yaliyokusudiwa na mnafanya kazi kwa uadilifu na kujiamini,” amesema Mkurugenzi Johnson.

Aidha, amewataka madereva kuwa na tabia ya kueleza changamoto wanazokutana nazo kazini, ili uongozi uweze kuzifanyia kazi kwa lengo la kuboresha mazingira ya kazi na kuongeza ufanisi.

Katika hatua nyingine, Mkurugenzi Mtendaji ameielekeza Idara ya Utumishi kuhakikisha inakuwa na utaratibu wa kukutana na madereva wapya mara kwa mara, ili kuwakumbusha maadili ya kazi, haki na wajibu wao pamoja na kuboresha taratibu za ufanyaji kazi ndani ya Halmashauri.

Kikao hicho ni sehemu ya jitihada za Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu za kuimarisha nidhamu, uwajibikaji na ubora wa huduma kwa wananchi kupitia usimamizi mzuri wa rasilimali watu na mali za umma.

Matangazo

  • TAARIFA YA MTIRIRIKO WA FEDHA KWA KIPINDI KILICHOISHIA TAREHE 30 JUNE. 2022 August 14, 2023
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI November 03, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MFAMASIA December 14, 2021
  • Orodha ya Walioitwa kwenye Usaili September 20, 2024
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI

    December 22, 2025
  • RC MHITA AWATAKA MADIWANI KISHAPU KUDUMISHA USHIRIKIANO NA MSHIKAMANO - NGUZO KUFANIKSHA MIPANGO YA MAENDELEO.

    December 19, 2025
  • DED JOHNSON ATOA MAELEKEZO MUHIMU KWA MADEREVA

    December 19, 2025
  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI WAMTEUA MWENYEKITI MPYA HALMASHAURI YA WILAYA KISHAPU

    December 03, 2025
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa