• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Utawala
      • Biashara, Viwanda na Uwekezaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya jamii
      • Afya
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Tehama
      • Utamaduni, Sanaa na Michezo
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Usafi wa Mazingira na Udhibiti Taka
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Kilimo na Mifugo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya picha na video za shughuli za maendeleo

RC MHITA AWATAKA MADIWANI KISHAPU KUDUMISHA USHIRIKIANO NA MSHIKAMANO - NGUZO KUFANIKSHA MIPANGO YA MAENDELEO.

Posted on: December 19th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Mboni .M. Mhita akizungumza katika kikao maalumu na madiwani wa Wilaya ya Kishapu kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Mboni .M. Mhita amefanya ziara katika Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu Disemba 18, 2025 katika ukumbi wa Halmashauri hiyo, ambapo amekutana na baraza jipya la Madiwani pamoja na wakuu wa divisheni na vitengo vya Halmashauri hiyo.

Lengo la ziara hiyo lilikuwa ni kuzungumza na madiwani 39 wa Halmashauri ya wilaya ya Kishapu, kuwapongeza na kuwaambia kuwa wananchi wana imani kubwa juu yao katika kuwasilikiza na kutatua kero zao, huku akiwataka madiwani hao kudumisha ushirikiano na mshikamano kama nguzo ya kufanikisha mipango ya maendeleo. “Udiwani ni dhamana ambayo wananchi wamewapatia kuwa na imani kubwa na ninyi,hivyo mna dhamana kubwa kwao kama wawakilishi wao kuwasikiliza na kuwajibika.” Amesema Mhe. Mhita.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa alipokelewa na kukaribishwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Ndg. Emmanuel Johnson, Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Peter Masindi na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Kishapu Mhe. Josephat Limbe.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Mhita amewasisitiza madiwani hao kutimiza majukumu yao ipasavyo, sambamba na kuimarisha demokrasia baina yao na wananchi kwa kuitisha mikutano ya hadhara mara kwa mara na wananchi wa kata zao ili kutatua changamoto zinazowakabili. Aidha amesema miradi ya maendeleo izingatie maslahi mapana ya wananchi wa Wilaya ya Kishapu.

Madiwani wa kata mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu wakisikiliza kikao maalumu cha Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo, Disemba 18,2025.

Ameongeza kuwa Serikali ya awamu ya sita inaendelea kuwalinda viongozi wote, wakiwemo madiwani katika kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao bila kuathiriwa na nia ovu kutoka kwa baadhi ya watu wasiolitakia mema taifa.

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa mkoa ameutaka uongozi wa Halmashauri na menejimenti yake vyanzo vipya vya kuongeza mapato ya ndani ya Halmashauri hiyo, kadhalika kubuni mifumo thabiti ya kuziba mianya ya upotevu wa fedha za umma.

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu mkoani Shiyanga Mhe.Peter Masindi akizungumza katika kikao maalumu cha Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo, Disemba 18, 2025.

Naye, Mwenyekiti wa Halmashauri kwa niaba ya madiwani amemshukuru Mkuu wa mkoa kwa maelekezo na ushauri aliowapatia, huku akiahidi kuyafanyia kazi kwa weledi na uadilifu kupitia ilani ya chama ili kuleta matokeo chanya.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu Mhe. Josephat Limbe akizungumza katika kikao maalumu cha Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri hiyo, Disemba 18,2025.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Kishapu Ndg. Emmanuel Johnson amesema kuwa yeye pamoja na menejimenti yake wataendelea kusimamia utekelezaji wa maelekezo yote yaliyotolewa na Mkuu huyo wa Mkoa kwa uadilifu, uwazi na uwajibikaji, huku akisisitiza kuwa lengo kuu ni kuwaletea wananchi huduma bora na kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma.

 “Menejimenti kwa ujumla wake tutaendelea kusimamia na kutekeleza maelekezo yote uliyoyatoa, ili kuhakikisha miradi ya maendeleo inatekelezwa kwa thamani ya fedha na kwa maslahi mapana ya wananchi.” Amesema Mkurugenzi

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu akizungumza katika kikao maalumu cha Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga,kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri hiyo, Disemba 18,2025.


Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu pamoja na wawakilishi kutoka taasisi tofauti wakifuatilia kikao kazi cha Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, kilichofanyika katikaukumbi wa Halmashauri hiyo, Disemba 18, 2025.

Ziara hiyo imeudhuriwa pia na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Kishapu, Katibu Tawala wa Wilaya, Mwakilishi wa Katibu Tawala Mkoa, wawakilishi kutoka Taasisi tofauti pamoja na wajumbe wa kamati ya usalama wa Mkoa na Wilaya.


Matangazo

  • TAARIFA YA MTIRIRIKO WA FEDHA KWA KIPINDI KILICHOISHIA TAREHE 30 JUNE. 2022 August 14, 2023
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI November 03, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MFAMASIA December 14, 2021
  • Orodha ya Walioitwa kwenye Usaili September 20, 2024
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI

    December 22, 2025
  • RC MHITA AWATAKA MADIWANI KISHAPU KUDUMISHA USHIRIKIANO NA MSHIKAMANO - NGUZO KUFANIKSHA MIPANGO YA MAENDELEO.

    December 19, 2025
  • DED JOHNSON ATOA MAELEKEZO MUHIMU KWA MADEREVA

    December 19, 2025
  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI WAMTEUA MWENYEKITI MPYA HALMASHAURI YA WILAYA KISHAPU

    December 03, 2025
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa