TAARIFA YA MIRADI YA MAENDELEO INAYOENDELEA KWA ROBO YA TATU KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026.
1. JINA LA MRADI; UJENZI WA MADARASA 2 YA AWALI NA MATUNDU 6 YA CHOO, SHULE YA MSINGI ISOSO.
Mradi huu unatekelezwa kwa thamani ya Tsh. 71,800,000/= kutoka chanzo cha fedha cha BOOST. Hali ya mradi mpaka sasa ni; boma la vyumba vya madarasa 2 limekamilika.Kwa upande wa matundu 6 ya vyoo, shughuli zilizobaki ni uchimbaji wa shimo la choo,upauaji, ufungaji wa masinki na kujenga mahali pa kusimamishia matenki ya kuvunia maji.

Ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa Shule ya Msingi Isoso
2. JINA LA MRADI; UJENZI WA VYUMBA 6 VYA MADARASA, JENGO LA UTAWALA,MATUNDU 12 YA CHOO,VYUMBA 2 VYA MADARASA NA MATUNDU 6 YA CHOO SHULE YA SEKONDARI ISOSO.
Mradi huu unatekelezwa kwa thamani ya Tsh. 342,900,000/= unaofadhiliwa na serikali kuu kupitia ufadhili wa BOOST.Hadi kufikia mwezi Januari,2026 miundombinu iko katika hatua ya ukamilishaji, na matundu mawili ya vyoo vya walimu ambavyo viko katika htua ya ujenzi wa boma. Mradi umefikia 75% ya utekelezaji.

Baadhi ya vyumba vya madarasa Shule ya Msingi Isoso

Jengo la Utawala Shule ya Msingi Isoso
3.JINA LA MRADI; UJENZI WA KITUO CHA AFYA LAGANA (JENGO LA OPD NA MAABARA).
Mradi huu unatekelezwa kwa thamani ya Tsh. 250,000,000/= kutoka serikali kuu. Ujenzi wa mradi ulianza kutekelezwa rasmi tarehe 29/10/2025.Mpaka sasa maboma yamekamilika kwa upande wa jengo la OPD na maabara, sawa na 40% ya utekelezaji.

Mwonekano wa ujenzi wa Boma la OPD katika kituo cha afya Lagana

Mwonekano wa ndani wa Jengo la OPD linalojengwa
4. JINA LA MRADI; UJENZI WA VYUMBA 2 VYA MADARASA NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI NHOBOLA.
Mradi huu unatekelezwa kwa thamani ya Tsh. 66,200,000/= kutoka fedha za BOOST. Mradi upo katika hali ya ukamilishaji,kupiga plasta na ufungaji wa dali.
5.JINA LA MRADI; UJENZI WA VIZIMBA 200, SOKO LA MAGANZO
Mradi huu unatekelezwa kwa thamani ya Tsh. 260,000,000/= kupitia fedha za CSR kutoka mgodi wa Mwadui. Kufikia Januari, 2026, mradi uko katika hali ya umwagaji jamvi na usakafiaji.
Ujenzi wa vizimba 200 katika soko la Maganzo.
6.JINA LA MRADI; UJENZI WA MATUNDU 5 YA CHOO,SOKO LA MAGANZO.
Mradi unatekelezwa kwa thamani ya Tsh.20,000,000/= kupitia fedha za CSR kutoka mgodi wa Mwadui.Mradi uko katika hali ya ukamilishaji kwa 95%

Ujenzi wa matunudu 5 ya choo soko la Maganzo
7.JINA LA MRADI; UJENZI WA OFISI YA KIJIJI CHA SONGWA
Mradi unatekelezwa kwa thamani ya Tsh. 47,000,000/= kupitia fedha za CSR kutoka mgodi wa Mwadui.Mradi upo katika hali ya upauaji.

Ujenzi wa ofisi kijiji cha Songwa
8.JINA LA MRADI; UJENZI WA VYUMBA 2 VYA MADARASA, SHULE YA MSINGI BUCHAMBI.
Mradi huu unatekelezwa kwa thamani ya Tsh. 48,000,000/= kupitia fedha za CSR, ambapo kuna vyumba 2 vya madarasa na matundu 5 vya choo. Mradi upo katika hali ya upigaji plasta.

Ujenzi wa vyumba 2 vya madarasa shule ya msingi Buchambi
9.JINA LA MRADI; UJENZI WA ZAHANATI YA SEKE IDIDI.
Mradi huu unatekelezwa kwa thamani ya Tsh. 101,989,971/=, ambapo kuna jengo la OPD na jengo la wazazi, kichomea taka na matundu 5 ya choo. Mradi upo katika hali ya upauaji na upigaji ripu.

Ujenzi wa Zahanati ya kijiji cha Seke Ididi
.
Halmashauri ya Wilaya Kishapu
Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU
Simu ya mezani: +255282770020
Simu: +255282770020
Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz
Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa