• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Utawala
      • Biashara, Viwanda na Uwekezaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya jamii
      • Afya
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Tehama
      • Utamaduni, Sanaa na Michezo
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Usafi wa Mazingira na Udhibiti Taka
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Kilimo na Mifugo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya kuonana na mwenyekiti wa Halmashauri
    • Ratiba ya vikao vya kisheria vya MSM
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Sheria ndogo ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya picha na video za shughuli za maendeleo

BARAZA LA MADIWANI KISHAPU LAPITISHA BAJETI YA BILIONI 1

Posted on: June 13th, 2025

Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu limepitisha rasmi bajeti ya Shilingi bilioni 1, zilizotolewa na Mgodi wa Almasi Mwadui kupitia mpango wa Uwajibikaji wa Makampuni kwa Jamii (CSR) kwa mwaka wa fedha 2025/2026.

Uamuzi huo umefanyika leo, Juni 13, 2025, katika kikao maalum cha Baraza la Madiwani kilichoitishwa mahsusi kwa ajili ya kujadili na kupitisha matumizi ya fedha hizo.

Afisa Mipango na Mratibu wa CSR katika Halmashauri ya Kishapu, Bw. James Zitto, akiwasilisha bajeti hiyo alisema kuwa fedha hizo zitatumika kutekeleza miradi ya maendeleo katika jamii pamoja na miradi ya kimkakati ya halmashauri.

“Asilimia 40 ya fedha hizi zitatumika kutekeleza miradi ya maendeleo kwenye maeneo yanayozunguka mgodi, na asilimia 60 zitatumika kwa miradi ya kimkakati ya halmashauri,” alisema Zitto.

Baada ya mjadala wa kina kutoka kwa madiwani, Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri aliomba baraza liridhie bajeti hiyo ambapo kwa kauli moja, madiwani waliidhinisha rasmi.

Mkurugenzi wa Halmashauri, Bw. Emmanuel Johnson, aliwataka madiwani kusimamia utekelezaji wa miradi hiyo kwa uadilifu mkubwa na kuonya dhidi ya migogoro ambayo inaweza kuathiri utoaji wa fedha hizo kutoka mgodini.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Mheshimiwa Peter Masindi, alitoa wito kwa viongozi kutowaingilia wakandarasi wala kuwaomba “kitu kidogo”, akisisitiza kuwa tamaa binafsi zisiharibu sifa ya viongozi wala kusababisha miradi hiyo kufeli.


Matangazo

  • TANGAZO LA MWALIKO WA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI January 20, 2026
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI December 22, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI November 21, 2025
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA WAFANYAKAZI KISHAPU LAPITISHA MWELEKEO MPYA MASLAHI YA WATUMISHI

    February 03, 2026
  • VIKUNDI 21 MAKUNDI MAALUMU VYAPATIWA MIKOPO KISHAPU

    January 29, 2026
  • BARAZA LA MADIWANI KISHAPU LAAZIMIA SOKO HURIA LA PAMBA, LATOA MSISITIZO WA LISHE NA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    January 28, 2026
  • DED KISHAPU AKABIDHI VIFAA VYA TEHAMA KUWAWEZESHA WAALIMU WENYE CHANGAMOTO YA UONI

    January 28, 2026
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa