• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Utawala
      • Biashara, Viwanda na Uwekezaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya jamii
      • Afya
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Tehama
      • Utamaduni, Sanaa na Michezo
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Usafi wa Mazingira na Udhibiti Taka
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Kilimo na Mifugo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya picha na video za shughuli za maendeleo

BARAZA LA MADIWANI KISHAPU LAPITISHA BAJETI YA BILIONI 1

Posted on: June 13th, 2025

Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu limepitisha rasmi bajeti ya Shilingi bilioni 1, zilizotolewa na Mgodi wa Almasi Mwadui kupitia mpango wa Uwajibikaji wa Makampuni kwa Jamii (CSR) kwa mwaka wa fedha 2025/2026.

Uamuzi huo umefanyika leo, Juni 13, 2025, katika kikao maalum cha Baraza la Madiwani kilichoitishwa mahsusi kwa ajili ya kujadili na kupitisha matumizi ya fedha hizo.

Afisa Mipango na Mratibu wa CSR katika Halmashauri ya Kishapu, Bw. James Zitto, akiwasilisha bajeti hiyo alisema kuwa fedha hizo zitatumika kutekeleza miradi ya maendeleo katika jamii pamoja na miradi ya kimkakati ya halmashauri.

“Asilimia 40 ya fedha hizi zitatumika kutekeleza miradi ya maendeleo kwenye maeneo yanayozunguka mgodi, na asilimia 60 zitatumika kwa miradi ya kimkakati ya halmashauri,” alisema Zitto.

Baada ya mjadala wa kina kutoka kwa madiwani, Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri aliomba baraza liridhie bajeti hiyo ambapo kwa kauli moja, madiwani waliidhinisha rasmi.

Mkurugenzi wa Halmashauri, Bw. Emmanuel Johnson, aliwataka madiwani kusimamia utekelezaji wa miradi hiyo kwa uadilifu mkubwa na kuonya dhidi ya migogoro ambayo inaweza kuathiri utoaji wa fedha hizo kutoka mgodini.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Mheshimiwa Peter Masindi, alitoa wito kwa viongozi kutowaingilia wakandarasi wala kuwaomba “kitu kidogo”, akisisitiza kuwa tamaa binafsi zisiharibu sifa ya viongozi wala kusababisha miradi hiyo kufeli.


Matangazo

  • TAARIFA YA MTIRIRIKO WA FEDHA KWA KIPINDI KILICHOISHIA TAREHE 30 JUNE. 2022 August 14, 2023
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI November 03, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MFAMASIA December 14, 2021
  • Orodha ya Walioitwa kwenye Usaili September 20, 2024
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI

    November 21, 2025
  • WATUMISHI KISHAPU WAPEWA MAFUNZO YA ELIMU YA FEDHA NA KUKABILIANA NA CHANGAMOTO YA AFYA YA AKILI

    November 20, 2025
  • DC,DED NA MSIMAMIZI WA UCHAGUZI JIMBO LA KISHAPU WAUNGANA NA WANANCHI KUPIGA KURA

    October 29, 2025
  • WASIMAMIZI WA VITUO KISHAPU WAONYWA KUTOKUWA CHANZO CHA MIGOGORO

    October 27, 2025
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa