• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Utawala
      • Biashara, Viwanda na Uwekezaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya jamii
      • Afya
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Tehama
      • Utamaduni, Sanaa na Michezo
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Usafi wa Mazingira na Udhibiti Taka
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Kilimo na Mifugo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya kuonana na mwenyekiti wa Halmashauri
    • Ratiba ya vikao vya kisheria vya MSM
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Sheria ndogo ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya picha na video za shughuli za maendeleo

KISHAPU YAPITISHA BAJETI YA BILIONI 54.3 2026/2027

Posted on: February 12th, 2026

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu Mhe. Josephat Limbe akizungumza kwenye kikao cha baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu Mkoani humo cha kupitisha bajeti ya shilingi bilioni 54.3 kwa mwaka wa fedha 2026/2027 Februari 12,2026 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo

Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga limeidhinisha bajeti ya shilingi bilioni 54.3 kwa mwaka wa fedha 2026/2027 katika kikao kilichofanyika Februari 12, 2026 kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo. Kati ya fedha hizo, bilioni 2.8 zimetengwa mahsusi kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Mhe. Josephat Limbe, amewapongeza Waheshimiwa Madiwani kwa kujadili kwa kina randama ya bajeti kuanzia ngazi ya kamati za kudumu hadi baraza la chama (CCM na ACT Wazalendo) hadi kufikia hatua ya kuidhinishwa rasmi. Akisisitiza umuhimu wa usimamizi wa mapato ya ndani, amesema: “Nawasihi madiwani kushiriki kikamilifu katika kusimamia ukusanyaji wa mapato ndani ya kata zenu ili kufanikisha utekelezaji wa shughuli zote za Halmashauri na miradi ya maendeleo.”

Muwakilishi wa Katibu Tawala Mkoa ameongeza msisitizo kwa kusema, “Tusiposimamia usimamizi wa mapato haya yote tunayoyaomba hayatatimia.” Aidha, ameshauri fedha zielekezwe kwenye miradi yenye matokeo ya moja kwa moja kwa wananchi. Kwa upande wake Katibu Tawala wa Wilaya ya Kishapu, Bi Fatma Mohammed, amewapongeza madiwani kwa kupitisha bajeti hiyo na kushauri kuongeza vyanzo vipya vya mapato ili kuimarisha utekelezaji wa miradi.


Mwakilishi wa Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga ambaye pia ni Afisa Serikali za Mitaa Mkuu  Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Fabian Kamoga akizungumza kwenye kikao cha baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu Mkoani humo cha kupitisha bajeti ya shilingi bilioni 54.3 kwa mwaka wa fedha 2026/2027 Februari 12,2026 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo

Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Kishapu, Ndg. Emmanuel Johnson, amewapongeza wataalamu wa Halmashauri kwa kuandaa bajeti hiyo kwa weledi na kuwakumbusha madiwani kuhakikisha watoto wa shule ya awali na kidato cha kwanza waanaandikishwa na kuanza masomo vilevile, kushiriki katika hatua za awali za uhamasishaji wa bima ya afya kwa wote na utambuzi wa kaya zisizo na uwezo ili kuingia kwenye mpango wa kugharamiwa na Serikali.

Katika kikao hicho, Meneja wa TARURA Wilaya ya Kishapu, Mhandisi Elia Mgaya, amewasilisha mpango wa bajeti ya matengenezo ya barabara kwa mwaka wa fedha 2026/2027. Waheshimiwa Madiwani wameweka azimio la kuomba fedha kutoka Serikali Kuu kwa ajili ya maboresho ya miundombinu ya barabara, wakisisitiza kuwa barabara bora ni kichocheo cha maendeleo ya kiuchumi na kijamii Wilayani humo.

Kupitishwa kwa bajeti ya bilioni 54.3 ni hatua muhimu inayodhihirisha dhamira ya Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu katika kusukuma gurudumu la maendeleo. Utekelezaji wake unatarajiwa kuleta mabadiliko chanya katika sekta mbalimbali hususan miradi ya maendeleo na miundombinu ya barabara, na hivyo kuboresha maisha ya wananchi wa Kishapu.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga Emmanuel Johnson (alievaa shati la draft) akifuatilia kwa makini kikao cha baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya hiyo cha kupitisha bajeti ya shilingi bilioni 54.3 kwa mwaka wa fedha 2026/2027 Februari 12,2026 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo

Matangazo

  • TANGAZO LA MWALIKO WA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI January 20, 2026
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI December 22, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI November 21, 2025
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • KISHAPU YAPITISHA BAJETI YA BILIONI 54.3 2026/2027

    February 12, 2026
  • KISHAPU YAJIPANGA KUONGEZA UZALISHAJI PAMBA

    February 04, 2026
  • BARAZA LA WAFANYAKAZI KISHAPU LAPITISHA MWELEKEO MPYA MASLAHI YA WATUMISHI

    February 03, 2026
  • VIKUNDI 21 MAKUNDI MAALUMU VYAPATIWA MIKOPO KISHAPU

    January 29, 2026
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa