Ina watumishi 6 kama inavyooneshwa hapo chini;-
Namba
|
Wadhifa
|
Idadi ya Watumishi
|
1
|
Mchumi wa Wilaya
|
1
|
2
|
Wachumi
|
4
|
3
|
Mtakwimu
|
1
|
Lengo.
Kuwa na mipango imara, kutekeleza miradi kwa ufanisi kwa kushirikiana na wananchi ili kuletea wananchi wa Kishapu na Taifa maendeleo.
Idara ya Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji inashughulika na;-
Kubuni vyanzo vya Mapato vya Halmashauri.
Kuratibu uandaaji wa Mpango kazi na Mpango mkakati wa Halmashauri.
Kufuatilia utekelezaji wa Mpango kazi wa Halmashauri.
Kuandaa/kuhuisha wasifu wa kiuchumi na uwekezaji wa Halmashauri.
Kukusanya, kuchakata na kutunza Takwimu za Halmashauri.
Kusimamia na kufuatilia utekelezaji wa shughuli za Maendeleo za Halmashauri.
Kuandaa maandiko ya miradi na kutafuta wadhamini/wafadhili kwa ajili ya utekelezaji.
Uratibu na utayarishaji wa Mpango na Bajeti ya Halmashauri kila mwaka.
Kusimamia utekelezaji wa Mpango wa Matokeo Makubwa sasa (BRN).
Kuratibu uandaaji wa taarifa mbalimbali za Halmashauri pamoja na taarifa za utekelezaji wa maagizo kutoka mamlaka za juu za serikali.
Kusimamia utekelezaji wa Fursa, uibuaji na vikwazo vya maendeleo (O & OD).
Kushauri matumizi sahihi ya fedha za Halmashauri.
Halmashauri ya Wilaya Kishapu
Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU
Simu ya mezani: +255282770020
Simu:
Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz
Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa