• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Utawala
      • Biashara, Viwanda na Uwekezaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya jamii
      • Afya
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Tehama
      • Utamaduni, Sanaa na Michezo
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Usafi wa Mazingira na Udhibiti Taka
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Kilimo na Mifugo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya kuonana na mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya picha na video za shughuli za maendeleo

RC MHITA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI NA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI KISHAPU.

Posted on: January 10th, 2026

Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe. Mboni Mhita akizungumza kwenye ziara ya ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa kituo cha afya Masagala kilichopo kata ya Maganzo wilaya ya Kishapu, leo Januari 10, 2026.


Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe. Mboni Mhita amefanya ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo wilaya ya Kishapu leo Januari 10, 2026 katika kituo cha afya Masagala kinachojengwa katika Kijiji cha Masagala kata ya Maganzo, ujenzi wa soko la wafanyabiashara Maganzo na ujenzi wa madarasa 3 na matundu 6 ya vyoo katika Kijiji cha Mwamasololo kilichopo kata ya Sekebugoro.

Akizungumza wakati wa kukagua ujenzi wa kituo hicho cha afya kinachojengwa kwa ufadhili wa kampuni ya Mwadui kupitia mpango wa uwajibikaji wa makampuni kwa jamii (CSR), Mhe. Mhita lengo la mradi huo ni kutatua changamoto kwa kuimarisha huduma za afya kwa wanakijiji. Amesema kuwa ameridhishwa na kasi ya ujenzi wa kituo hicho huku nakiwashukuru wananchi wa Masagala kwa kuanza awali kuibua mradi wa ujenzi huo.

 “Nimeridhishwa sana kwa kasi na ubora wa ujenzi wa kituo hiki. hii ni jitihada kubwa. Ninatarajia mda mfupi ujao wananchi hawatotembea umbali mrefu kufuata huduma za afya”.Alisema Mhe. Mhita

 Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe. Mboni Mhita akikagua ujenzi wa kituo cha afya Masagala kilichopo katika Kijiji cha Masagala kata ya Maganzo wilayani humo leo Januari 10,2026.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kijiji cha Masagala Bw. Juma Kapima amesema kukamilika kwa kituo hicho kutapunguza adha ya wananchi waliokua wakifuata huduma hospitali ya Kolandoto na Mwadui.

Jumla ya sh. milioni 177,600,000 zinatarajiwa kutumika hadi kukamilika kwa kituo hiki cha afya Masagala ifikapo mwishoni mwa mwezi Februari, 2026, ambapo majengo yanayojengwa ni OPD, RCH, maabara, vyoo matundu 5 na kichomea taka.

 Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe. Mhita akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya Mhe. Peter Masindi, wadau kutoka kampuni ya Mwadui pamoja na wananchi wa kijiji cha Masagala Januari 10, 2026.

Katika mradi wa ujenzi wa soko la kisasa la wafanyabiashara Maganzo kupitia mpango wa CSR Mhe. Mhita ameridhishwa na maendeleo ya ujenzi huo huku akitoa agizo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri kuhakikisha kuwa wafanyabiashara wa zamani wa soko hilo wanapewa kipaumbele cha kurejea katika soko hilo jipya pindi ujenzi utakapokamilika.

“Wafanyabiashara waliopisha ujenzi huu wapewe nafasi kwanza kwasababu ndio walikuwa kwenye soko hili awali, wakilipa ushuru na kuchangia mapato ya Halmashauri”.Alisema Mhe. Mhita

Akisoma taarifa ya utekelezaji wa mradi huo, Bi.Hilda Hozza kutoka mgodi wa Mwadui alisema soko hilo linajengwa kwa gharama ya sh. Milioni 260.Aliongeza kuwa hadi sasa ujenzi umefikia asilimia 70 na unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Februari,2026.

 Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe.Mboni Mhita akizungumza kwenye ziara ya ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa soko la wafanyabiashara la Maganzo lililopo kata ya Maganzo wilaya ya Kishapu leo Januari 10, 2026

Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe. Mboni Mhita akinunua bidhaa kwa mmoja wa wafanyabiasha waliopisha ujenzi wa soko jipya la kisasa katika eneo la Maganzo, leo Januari 10,2026.

   Muonekano wa soko la kisasa la wafanyabiashara linalojengwa katika eneo la Maganzo, kata ya Maganzo, wilaya ya Kishapu.

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa mkoa amepata fursa ya kusikiliza kero za wanchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Mipa kata ya Sekebugoro, ambapo wanakijiji waliwasilisha kero na changamoto zao hususani upande wa barabara, maji yaani ukosefu wa maji kutoka ziwa victoria kwenye baadhi ya vijiji, elimu yaani upungufu wa walimu, vituo vya afya yaani upungufu wa madaktari, pamoja na ombi la uimarishwaji wa ulinzi katika makazi yao.

Aidha Mhe. Mhita amezitaka mamlaka husika za taasisi zilizopo ndani ya Wilaya ya Kishapu kushughulikia mahitaji hayo ya wananchi, huku akisema kazi yake ni kurejesha imani na tabasamu kwa wananchi.

  



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI December 22, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI November 21, 2025
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • RC MHITA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI NA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI KISHAPU.

    January 10, 2026
  • RC MHITA AWATAKA MADIWANI KISHAPU KUDUMISHA USHIRIKIANO NA MSHIKAMANO - NGUZO KUFANIKISHA MIPANGO YA MAENDELEO.

    December 19, 2025
  • DED JOHNSON ATOA MAELEKEZO MUHIMU KWA MADEREVA

    December 19, 2025
  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI WAMTEUA MWENYEKITI MPYA HALMASHAURI YA WILAYA KISHAPU

    December 03, 2025
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa