Kitengo cha Ufugaji Nyuki kina jukumu la kusimamia na kuhakikisha mazao ya nyuki yanazalishwa kwa tija na kuwa njia mbadala ya kuongeza kipato na kukuza uchumi kwa wananchi baada ya shughuli zitokanazo na kilimo.
Ufugaji Nyuki ulikuwa ukifanyika kwa baadhi ya kaya kwa sababu maalumu na warina asali walikuwa na taratibu za kutafuta asali katika mapango na misitu ambako makundi ya nyuki yalipatikana kwa urahisi.
Ufinyu wa ardhi, kupanuka kwa shughuli za kilimo na makazi kulichangia kuhamisha na kupunguza mtawanyiko sawia wa makundi ya nyuki katika maeneo mbalimbali wilayani. Changamoto hii na umuhimu wa mazao ya Nyuki imepelekea kitengo cha ufugaji Nyuki kwa kushirikiana na wadau wengine kuhamasisha ufugaji na hasa kwa kutumia mbinu ya inayosisitiza ufugaji wa makundi mengi katika eneo dogo ili kukabiliana na changamoto ya ufinyu wa ardhi.
Kuhamasisha wananchi juu ya Ufugaji wa kisasa wa Nyuki kwa kutumia mizinga ya kisasa, ufugaji wa nyuki kwa kutumia teknologia ya Nyumba (Bee house Technology) na uundwaji wa vikundi vya ufugaji nyuki.
Hadi sasa kuna vikundi na watu binafsi wapatao 61 wanaojishughulisha na Ufugaji wa nyuki, kati ya hao kuna vikundi 10 na watu binafsi 11 ambao tayari wana mizinga na maeneo ya kufugia. Idadi ya mizinga iliyopo kwa sasa ni mizinga 755 katika maeneo mbalimbali ya Wilaya.
vikundi na watu binafsi wanaojishughulisha na ufugaji wa nyuki wameweza kuvuna jumla ya kilo 1174 yenye thamani ya Tshs 11,740,000/= kwa bei ya Tshs 10,000 kwa kilo moja ya asali.
Wilaya kwa kushirikiana na wadau wa Mazingira na Ufugaji nyuki imefanikiwa kuhamasisha ufugaji wa Nyuki kwa kutumia teknologia ya nyumba katika Vijjiji vya Mwamashele, Inolelo, Miyuguyu, Nyasamba na Mipa. Mpaka sasa kuna Nyumba mbili (Bee house) za kufugia nyuki ambazo zimeanzishwa katika kijiji cha Mipa eneo la Mission yenye mizinga 100 ambayo imefadhiliwa na TaFF (Tanzania Forest Fund) na manzuki ya mfano katika kijiji cha Mwamashele yenye mizinga 4 ambayo imetolewa na Halmashauri ya Wilaya.
Halmashauri ya Wilaya Kishapu
Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU
Simu ya mezani: +255282770020
Simu:
Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz
Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa