• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
    • Idara
      • Fedha
      • Rasilimali watu
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
  • Nyaraka
    • Fomu za kujinga na Kidato cha Tano
      • Shule ya Sekondari Kishapu
      • Shule ya Sekondari Shinyanga
    • Mpango wa bajeti wa mwaka 2021/2022
    • Matangazo
    • Sheria ndogo ya ushuru wa huduma
    • Mifumo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
      • Uvuvi wa Samaki katika Bwawa la Songwa, Bwawa mhumbu
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Mhe. William Luhende Jijimya - Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Mhe. Francis Manyanda - Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Mhe. Joel Ndettoson - Diwani kata ya Kishapu
      • Mhe. Mohamed Aman - Diwani kata ya Ndoleleji
      • Mhe. Lucas Nkende - Diwani kata ya Mwamashele
      • Mhe. Pontias Daud - Diwani kata ya Mwataga
      • Mhe. James Kasomi - Diwani kata ya Bubiki
      • Mhe. Bushi Mpina - Diwani kata ya Mwamalasa
      • Mhe. Nyama Kisinza - Diwani kata ya Somagedi
      • Mhe. Mashini W. Washima - Diwani kata ya Uchunga
      • Mhe. Anderson Mandia - Diwani kata ya Ukenyenge
      • Mhe. Edward Manyama - Diwani kata ya Kiloleli
      • Mhe. Reuben Siyabo - Diwani kata ya Bupigi
      • Mhe. Bujiku Nyanda - Diwani kata ya Mwaweja
      • Mhe. Michael Paul - Diwani kata ya Shagihilu
      • Mhe. Luhende S. Luhende - Diwani kata ya Lagana
      • Mhe. Richard Dominico - Diwani kata ya Talaga
      • Mhe. James Kamuga - Diwani kata ya Igaga
      • Mhe. Lameck Nsubata - Diwani kata ya Itilima
      • Mhe. Mpemba Malangahe - Diwani kata ya Bunambiyu
      • Mhe. Makenzi Charles - Diwani kata ya Busangwa
      • Mhe. Nestory Kalugula - Diwani kata ya Ngofila
      • Mhe. Lwinzi Kidiga - Diwani kata ya Maganzo
      • Mhe. Samson Gelewa - Diwani kata ya Mwasubi
      • Mhe. Sarah Marco - Diwani kata ya Idukilo
      • Mhe. Enock Bundala - Diwani kata ya Masanga
      • Mhe. Thabidha Mmbando - Diwani kata ya Mwakipoya
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Mwenyekiti wa Halmashauri
  • miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
  • Kituo Cha Habari
    • maktaba ya picha
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa za Vyombo vya Habari
  • Maeneo
    • Kata
      • Orodha ya Kata
    • Tarafa
      • Orodha ya Tarafa
    • Vijiji
      • Orodha ya Vijiji

BANK YA CRDB YATOA MADAWATI 120 SHULE ZA MSINGI KISHAPU

Posted on: July 28th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Mhe.Peter Masindi akikabidhiwa dawati na watumishi toka Benki ya CRDB Julai 28,2025 

Wanafunzi 120 kutoka Shule za Msingi Mwakolomwa Kata ya Seke bugoro na Ndoleleji Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga wamenufaika na msaada wa madawati 120 yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 8 kutoka Benki ya CRDB, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa sera ya uwajibikaji kwa jamii ya 1% ya faida ya benki hiyo.

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika Julai 28,2025 katika shule ya Msingi Mwakolomwa na Ndoleleji Mgeni rasmi ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Peter Masindi ameipongeza CRDB kwa moyo wa kujitoa kusaidia maendeleo ya elimu Wilayani humo.

"Nawashukuru CRDB kwa moyo wenu wa kizalendo mnaoonesha kuwa mnawekeza si tu kwenye biashara, bali pia kwenye ndoto za watoto wetu hivyo wazazi tuache kukatisha ndoto za watoto wetu kwa kuwaoza au kuwapeleka kuchunga mifugo badala ya kuwapa nafasi wasome" amesema Masindi

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Mhe Peter Masindi 

Mhe.Masindi amewahimiza wanafunzi kutenga muda wa kusoma na kuwa na nidhamu kwani ndiyo zawadi na amana kubwa katika maisha ya shule na baada ya shule

"Msingi mnaopewa ni kwa maisha na faida yenu pekee acheni utoro,jisomeeni na kuelekezana Ninyi kwa Ninyi,msiwe wabinafsi kwenye masomo hakuna aliyefanikiwa bila kusoma wakati huo muwatii na wazazi wenu" amesema Masindi

Amewataka waalimu kuongeza juhudi na kubuni mbinu mbalimbali za ufundishaji ili kuongeza ufaulu kwa wanafunzi.

"CRDB wameonesha upekee wa kuwajali watoto wetu na nyie wazazi msiwafanye watoto ni vitega uchumi majumbani kwenu hasa wa kike na hao sio wachungaji wa mifugo mliyonayo wapeni nafasi wasome na mwahimize kwenda shule na kufanya vizuri ili baadae wawe msaada kwenu" Ameongeza Mkuu wa Wilaya huyo.

Naye Mwakilishi wa Mkurugenzi wa CRDB Bank Tanzania ambaye pia ni Mkuu wa Kitengo cha Malipo CRDB Makao makuu Bw.Madaha Chabba ameishukuru Serikali ya Wilaya kwa ushirikiano mkubwa na moyo wa kupokea na kuthamini mchango wa taasisi binafsi kama CRDB.

"Serikali yenu imetupokea kwa moyo mmoja na kutambua thamani ya ushirikiano wa sekta binafsi katika kuchochea maendeleo," amesema Chabba.

Meneja wa CRDB Kanda ya Magharibi Bw. Jumanne Wagana amesema benki hiyo ina utaratibu wa kurejesha asilimia moja (1%) ya faida yake kwa jamii kupitia miradi ya maendeleo hususa katika sekta za elimu, afya na mazingira.

"Tumekabidhi madawati haya 120 kwa shule mbili zenye changamoto kubwa ya miundombinu tunatambua kuwa mazingira bora ya kusomea ni msingi wa mafanikio ya mtoto wa Kitanzania," ameeleza Wagana.

Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Wilaya ya Kishapu, Bi. Fatma Haji Mohamed, amewasisitiza wanafunzi kuyatunza madawati hayo na kuyatumia kwa ufanisi kama sehemu ya kujenga nidhamu na uthubutu wa kutimiza ndoto zao.

Wananchi na wazazi walioudhuria hafla hiyo wameonesha furaha na kuipongeza CRDB kwa msaada huo muhimu, wakisema utapunguza msongamano wa wanafunzi madarasani na kuongeza ufanisi katika ujifunzaji.

"Mwenyezi Mungu aibariki CRDB Mtoto wangu alikuwa anakalia mawe na hata kukaa chini anarudi amechafuka sana lakini sasa atakalia dawati kama wengine." amesema mzazi Bunoge Nkinga.

Mwanafunzi wa dalasa la saba shule ya msingi Mwakolomwa Jackline Richard amesema sasa wanauhakika wa mazingira salama ya kujifunzia na kuandika.

Katika taarifa ya shule, Mwakolomwa iliyoko kata ya Sekebugoro imebakiwa na upungufu wa madawati 16 Kwa upande wa Shule ya Msingi Ndoleleji ikiwa na upungufu wa madawati 103 ambapo kila shule wamepokea madawati 60 kutoka CRDB, hivyo kupunguza kwa kiasi kikubwa changamoto hiyo.

Hii ni hatua kubwa katika kuboresha mazingira ya kujifunza kwa watoto wa Kishapu, na ni mfano wa namna sekta binafsi inavyoweza kushirikiana na serikali katika kuinua elimu nchini.

Matangazo

  • TAARIFA YA MTIRIRIKO WA FEDHA KWA KIPINDI KILICHOISHIA TAREHE 30 JUNE. 2022 August 14, 2023
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI November 03, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MFAMASIA December 14, 2021
  • Orodha ya Walioitwa kwenye Usaili September 20, 2024
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • BANK YA CRDB YATOA MADAWATI 120 SHULE ZA MSINGI KISHAPU

    July 28, 2025
  • MCHAKATO WAANZA UJENZI DAMPO LA KISASA KISHAPU KUIMARISHA USAFI WA MAZINGIRA

    July 26, 2025
  • RC MHITA AFANYA ZIARA YA KIKAZI KISHAPU

    July 22, 2025
  • WANANCHI 1,200 VIJIJI VYA MFANO KISHAPU WAPEWA HATI MILKI ZA KIMILA

    July 23, 2025
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa