• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
    • Idara
      • Fedha
      • Rasilimali watu
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
  • Nyaraka
    • Fomu za kujinga na Kidato cha Tano
      • Shule ya Sekondari Kishapu
      • Shule ya Sekondari Shinyanga
    • Mpango wa bajeti wa mwaka 2021/2022
    • Matangazo
    • Sheria ndogo ya ushuru wa huduma
    • Mifumo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
      • Uvuvi wa Samaki katika Bwawa la Songwa, Bwawa mhumbu
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Mhe. William Luhende Jijimya - Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Mhe. Francis Manyanda - Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Mhe. Joel Ndettoson - Diwani kata ya Kishapu
      • Mhe. Mohamed Aman - Diwani kata ya Ndoleleji
      • Mhe. Lucas Nkende - Diwani kata ya Mwamashele
      • Mhe. Pontias Daud - Diwani kata ya Mwataga
      • Mhe. James Kasomi - Diwani kata ya Bubiki
      • Mhe. Bushi Mpina - Diwani kata ya Mwamalasa
      • Mhe. Nyama Kisinza - Diwani kata ya Somagedi
      • Mhe. Mashini W. Washima - Diwani kata ya Uchunga
      • Mhe. Anderson Mandia - Diwani kata ya Ukenyenge
      • Mhe. Edward Manyama - Diwani kata ya Kiloleli
      • Mhe. Reuben Siyabo - Diwani kata ya Bupigi
      • Mhe. Bujiku Nyanda - Diwani kata ya Mwaweja
      • Mhe. Michael Paul - Diwani kata ya Shagihilu
      • Mhe. Luhende S. Luhende - Diwani kata ya Lagana
      • Mhe. Richard Dominico - Diwani kata ya Talaga
      • Mhe. James Kamuga - Diwani kata ya Igaga
      • Mhe. Lameck Nsubata - Diwani kata ya Itilima
      • Mhe. Mpemba Malangahe - Diwani kata ya Bunambiyu
      • Mhe. Makenzi Charles - Diwani kata ya Busangwa
      • Mhe. Nestory Kalugula - Diwani kata ya Ngofila
      • Mhe. Lwinzi Kidiga - Diwani kata ya Maganzo
      • Mhe. Samson Gelewa - Diwani kata ya Mwasubi
      • Mhe. Sarah Marco - Diwani kata ya Idukilo
      • Mhe. Enock Bundala - Diwani kata ya Masanga
      • Mhe. Thabidha Mmbando - Diwani kata ya Mwakipoya
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Mwenyekiti wa Halmashauri
  • miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
  • Kituo Cha Habari
    • maktaba ya picha
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa za Vyombo vya Habari
  • Maeneo
    • Kata
      • Orodha ya Kata
    • Tarafa
      • Orodha ya Tarafa
    • Vijiji
      • Orodha ya Vijiji

DC KISHAPU ASIKILIZA NA KUTATUA KERO ZA WANANCHI TARAFA YA KISHAPU

Posted on: August 25th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Mhe.Peter N.Masindi akizungumza kwenye ziara yake ya kikazi ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi wa Kata ya Mwataga,Kishapu na Kata ya Uchunga Agosti 25,2025


Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga, Mhe. Peter Masindi, amesikiliza na kutatua kero za wananchi wa Kata za Mwataga, Kishapu na Uchunga katika mkutano wa hadhara uliofanyika Agosti 25, 2025 katika maeneo hayo.


Miongoni mwa changamoto zilizowasilishwa ni huduma ya maji safi, upatikanaji wa umeme, uboreshaji wa barabara,uboreshaji wa miundombinu ya mawasiliano ya simu Uchunga, huduma za afya katika Zahanati ya Lubaga na ujenzi wa nyumba ya walimu katika Shule ya Msingi Lubaga.

"Ndugu zangu wananchi niwapongeze kwa kuendelea kuiamni serikali ya awamu ya sita na pia napenda kuhamasisha kuendelea kufanya kazi kwa bidii, kuepuka mikusanyiko isiyo na tija na kuwekeza zaidi katika familia zenu hususa ni katika maendeleo ya wanawake na watoto" amesema Masindi

Aidha Mkuu huyo wa Wilaya amewataka wazazi kuwasomesha watoto wao na kuwaendeleza kwenye vipaji mbalimbali waliofeli masomo huku wakiwawekeza zaidi kwenye malezi bora yenye kufuata maadili ya KiTanzania huku akiahidi mahitaji mengine ambayo hayapata utatuzi serikali inaendeleza jitihada ya kuzitatua kwa haraka ili wananchi wanufaike na nchi yao.


Katibu Tawala Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga Bi.Fatma Mohamed akizungumza kwenye ziara ya Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe.Peter N.Masindi ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi wa Kata ya Mwataga,Kishapu na Kata ya Uchunga Agosti 25,2025

Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Kishapu, David Mashauri,akijibu maswali ya sekta ya elimu amesema Halmashauri imeanza kupokea fedha kwa ajili ya kujenga Shule shikizi katika maeneo yenye changamoto ya watoto kutembea umbali mrefu huku Kitongoji cha Lubaga kilichoko Kata ya kishapu kikiwa ni miongoni wa wanufaika.

Mashauri ameongeza kuwa Shule ya Msingi Bukingwa-Mandenge na Bulima tayari zimepangiwa fedha kwa ujenzi wa madarasa, huku nyumba ya Walimu Shule ya Msingi Lubaga ikiwa kwenye bajeti ya mwaka wa fedha 2025/2026 wanasubiria fedha ili kuboresha jengo hilo.


Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Kishapu Mkoani Shinyanga David Mashauri akizungumza kwenye ziara ya Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe.Peter N.Masindi ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi wa Kata ya Mwataga,Kishapu na Kata ya Uchunga Agosti 25,2025


Meneja wa RUWASA Wilayani humo, Dickson Kamazima, amesema serikali inaendelea kusogeza huduma ya maji safi kwa wananchi ambapo kwa Kitongoji cha Mwataga utekelezaji umefikia asilimia 95, na maeneo mengine yatapatiwa huduma kupitia maji ya Ziwa Viktoria na visima vinavyochimbwa kisasa.


Aidha amesema wiki ya kwanza ya Septemba watafanya uthamini katika Kitongoji cha Migunga ili kusogeza huduma hiyo kupitia kwenye bomba kubwa la maji linaloelekea Kata ya Lagana, huku Kitongoji cha Mwanulu kikiwa kwenye mpango wa kusogezewa huduma pia baada ya kupokea fedha kutoka serikalini.

Meneja wa RUWASA Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga Dickson Kamazima akijibu maswali ya wananchi kwenye ziara ya Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe.Peter N.Masindi ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi wa Kata ya Mwataga,Kishapu na Kata ya Uchunga Agosti 25,2025

Kwa upande wa umeme, Mwakilishi wa Meneja wa TANESCO Wilayani humo, Gidion Kanan, amesema serikali inaendelea kusambaza nishati hiyo kwenye Vijiji na vitongoji kote Wilayani humo.

Ametoa wito kwa wananchi kuendelea kulinda miundombinu ya umeme na kuunga mkono matumizi ya nishati safi ili kutunza mazingira.

Wananchi wameendelea kuzipongeza jitihada za serikali kwa kusogeza huduma muhimu za kijamii jambo linalosaidia kujenga jamii bora na yenye matumaini imara.


Mwakilishi wa Meneja wa Tanesco Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga Gidion Kanan akijibu maswali ya wananchi kwenye ziara ya Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe.Peter N.Masindi ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi wa Kata ya Mwataga,Kishapu na Kata ya Uchunga Agosti 25,2025


Afisa Tarafa ya Kishapu Mkoani Shinyanga Tano John ziara ya Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe.Peter N.Masindi ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi wa Kata ya Mwataga,Kishapu na Kata ya Uchunga Agosti 25,2025

Muonekano wa Awali wa choo kilichokuwa kikitumiwa na Wanafunzi wa Shule ya Msingi Lubaga iliyoko Kata ya Kishapu Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga


Muonekano wa choo cha kisasa kinachojengwa katika Shule ya Msingi Lubaga Kata ya Kishapu Wilayani Kishapu Mkoani Shimyanga kupitia fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga

Matangazo

  • TAARIFA YA MTIRIRIKO WA FEDHA KWA KIPINDI KILICHOISHIA TAREHE 30 JUNE. 2022 August 14, 2023
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI November 03, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MFAMASIA December 14, 2021
  • Orodha ya Walioitwa kwenye Usaili September 20, 2024
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI

    November 21, 2025
  • WATUMISHI KISHAPU WAPEWA MAFUNZO YA ELIMU YA FEDHA NA KUKABILIANA NA CHANGAMOTO YA AFYA YA AKILI

    November 20, 2025
  • DC,DED NA MSIMAMIZI WA UCHAGUZI JIMBO LA KISHAPU WAUNGANA NA WANANCHI KUPIGA KURA

    October 29, 2025
  • WASIMAMIZI WA VITUO KISHAPU WAONYWA KUTOKUWA CHANZO CHA MIGOGORO

    October 27, 2025
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa