• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Utawala
      • Biashara, Viwanda na Uwekezaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya jamii
      • Afya
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Tehama
      • Utamaduni, Sanaa na Michezo
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Usafi wa Mazingira na Udhibiti Taka
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Kilimo na Mifugo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya kuonana na mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya picha na video za shughuli za maendeleo

DC KISHAPU AWATAKA WANANCHI KUTUMIA KWA TIJA MBEGU ZILIZOBARIKIWA BUSIYA

Posted on: July 8th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Mhe. Peter Masindi, ametoa wito kwa wananchi waliopokea mbegu zilizobarikiwa katika kilele cha Tamasha la Utamaduni wa Kisukuma "Sanjo ya Busiya", kuzitumia kwa tija katika msimu ujao wa kilimo ili kuboresha maisha na uchumi wa familia zao.

Akihutubia maelfu ya wakazi waliohudhuria tamasha hilo lililofanyika katika viwanja vya Ikulu ya Busiya – Ukenyenge Julai 7,2025 Mhe. Masindi amesema matumizi sahihi ya mbegu hizo ni msingi wa mafanikio kwa familia na jamii kwa ujumla.

"Wote mtakaochukua mbegu hizi zilizobarikiwa hakikisheni mnalima kwa wingi. Baada ya mavuno, watoto wasome, familia zinufaike. La sivyo, mkiziingiza kwenye matumizi ya anasa, fedha hizo zitageuka kuwa laana badala ya baraka," ameonya Mhe. Masindi.

MKuu wa Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Mhe Peter Masindi (kulia) akizungumza na wananchi kwenye sherehe za Tamasha la Utamaduni la Sanjo ya Busiya kwenye viwanja vya Ikulu ya Busiya Ukenyenge Wilayani humo Julai 7,2025

Aidha, Mkuu huyo wa Wilaya ameeleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, maarufu kwa jina la heshima Chifu Hangaya, itaendelea kuhimiza jamii kuenzi na kulinda tamaduni njema kama sehemu ya urithi na maendeleo ya Taifa.

Akizungumza katika tamasha hilo, Mtemi Faustine Makwaia wa III wa Utemi wa Busiya, unaojumuisha kata kumi za Wilaya ya Kishapu amesisitiza kuwa upendo ni silaha muhimu ya kuleta maendeleo na kuondoa chuki katika jamii.

"Tukiwa na upendo ndipo maendeleo yatakuwepo. Kinyume cha upendo ni chuki, na pale panapokuwepo chuki hakuna maendeleo kwa kuwa hakuna maono ya pamoja.Amesema Makwaia wa III

Tamasha la Sanjo ya Busiya limejumuisha mashindano ya ngoma na muziki wa asili kutoka ndani na nje ya Wilaya ya Kishapu, maonesho ya vyakula vya jadi vya Kisukuma, mavazi ya asili, na matumizi ya vyombo vya kijadi. Mgeni rasmi, Mtemi Makwaia wa III, alikabidhi zawadi kwa vikundi vilivyoshiriki, wanawake waliotoa mchango mkubwa katika mavazi na mapishi ya asili, na watoa huduma mbalimbali wa kitamaduni.

Mtemi wa Busiya Chifu Faustine Makwaia wa III Utemi wenye makao yake makuu Ukenyenge Wilayani  Kishapu Mkoani Shinyanga akizungumza na wananchi kwenye sherehe za tamasha la Sanjo ya Busiya Julai 7,2025

Kwa ujumla, tamasha hilo limeonyesha mshikamano wa jamii, kuenzi mila na desturi za Kisukuma, pamoja na kuhimiza matumizi ya rasilimali za asili kwa maendeleo endelevu.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI December 22, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI November 21, 2025
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWATAKA MADIWANI KISHAPU KUDUMISHA USHIRIKIANO NA MSHIKAMANO - NGUZO KUFANIKISHA MIPANGO YA MAENDELEO.

    December 19, 2025
  • DED JOHNSON ATOA MAELEKEZO MUHIMU KWA MADEREVA

    December 19, 2025
  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI WAMTEUA MWENYEKITI MPYA HALMASHAURI YA WILAYA KISHAPU

    December 03, 2025
  • WATUMISHI KISHAPU WAPEWA MAFUNZO YA ELIMU YA FEDHA NA KUKABILIANA NA CHANGAMOTO YA AFYA YA AKILI

    November 20, 2025
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa