• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
    • Idara
      • Fedha
      • Rasilimali watu
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
  • Nyaraka
    • Fomu za kujinga na Kidato cha Tano
      • Shule ya Sekondari Kishapu
      • Shule ya Sekondari Shinyanga
    • Mpango wa bajeti wa mwaka 2021/2022
    • Matangazo
    • Sheria ndogo ya ushuru wa huduma
    • Mifumo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
      • Uvuvi wa Samaki katika Bwawa la Songwa, Bwawa mhumbu
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Mhe. William Luhende Jijimya - Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Mhe. Francis Manyanda - Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Mhe. Joel Ndettoson - Diwani kata ya Kishapu
      • Mhe. Mohamed Aman - Diwani kata ya Ndoleleji
      • Mhe. Lucas Nkende - Diwani kata ya Mwamashele
      • Mhe. Pontias Daud - Diwani kata ya Mwataga
      • Mhe. James Kasomi - Diwani kata ya Bubiki
      • Mhe. Bushi Mpina - Diwani kata ya Mwamalasa
      • Mhe. Nyama Kisinza - Diwani kata ya Somagedi
      • Mhe. Mashini W. Washima - Diwani kata ya Uchunga
      • Mhe. Anderson Mandia - Diwani kata ya Ukenyenge
      • Mhe. Edward Manyama - Diwani kata ya Kiloleli
      • Mhe. Reuben Siyabo - Diwani kata ya Bupigi
      • Mhe. Bujiku Nyanda - Diwani kata ya Mwaweja
      • Mhe. Michael Paul - Diwani kata ya Shagihilu
      • Mhe. Luhende S. Luhende - Diwani kata ya Lagana
      • Mhe. Richard Dominico - Diwani kata ya Talaga
      • Mhe. James Kamuga - Diwani kata ya Igaga
      • Mhe. Lameck Nsubata - Diwani kata ya Itilima
      • Mhe. Mpemba Malangahe - Diwani kata ya Bunambiyu
      • Mhe. Makenzi Charles - Diwani kata ya Busangwa
      • Mhe. Nestory Kalugula - Diwani kata ya Ngofila
      • Mhe. Lwinzi Kidiga - Diwani kata ya Maganzo
      • Mhe. Samson Gelewa - Diwani kata ya Mwasubi
      • Mhe. Sarah Marco - Diwani kata ya Idukilo
      • Mhe. Enock Bundala - Diwani kata ya Masanga
      • Mhe. Thabidha Mmbando - Diwani kata ya Mwakipoya
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Mwenyekiti wa Halmashauri
  • miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
  • Kituo Cha Habari
    • maktaba ya picha
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa za Vyombo vya Habari
  • Maeneo
    • Kata
      • Orodha ya Kata
    • Tarafa
      • Orodha ya Tarafa
    • Vijiji
      • Orodha ya Vijiji

DC KISHAPU AWATAKA WANANCHI KUTUMIA KWA TIJA MBEGU ZILIZOBARIKIWA BUSIYA

Posted on: July 8th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Mhe. Peter Masindi, ametoa wito kwa wananchi waliopokea mbegu zilizobarikiwa katika kilele cha Tamasha la Utamaduni wa Kisukuma "Sanjo ya Busiya", kuzitumia kwa tija katika msimu ujao wa kilimo ili kuboresha maisha na uchumi wa familia zao.

Akihutubia maelfu ya wakazi waliohudhuria tamasha hilo lililofanyika katika viwanja vya Ikulu ya Busiya – Ukenyenge Julai 7,2025 Mhe. Masindi amesema matumizi sahihi ya mbegu hizo ni msingi wa mafanikio kwa familia na jamii kwa ujumla.

"Wote mtakaochukua mbegu hizi zilizobarikiwa hakikisheni mnalima kwa wingi. Baada ya mavuno, watoto wasome, familia zinufaike. La sivyo, mkiziingiza kwenye matumizi ya anasa, fedha hizo zitageuka kuwa laana badala ya baraka," ameonya Mhe. Masindi.

MKuu wa Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Mhe Peter Masindi (kulia) akizungumza na wananchi kwenye sherehe za Tamasha la Utamaduni la Sanjo ya Busiya kwenye viwanja vya Ikulu ya Busiya Ukenyenge Wilayani humo Julai 7,2025

Aidha, Mkuu huyo wa Wilaya ameeleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, maarufu kwa jina la heshima Chifu Hangaya, itaendelea kuhimiza jamii kuenzi na kulinda tamaduni njema kama sehemu ya urithi na maendeleo ya Taifa.

Akizungumza katika tamasha hilo, Mtemi Faustine Makwaia wa III wa Utemi wa Busiya, unaojumuisha kata kumi za Wilaya ya Kishapu amesisitiza kuwa upendo ni silaha muhimu ya kuleta maendeleo na kuondoa chuki katika jamii.

"Tukiwa na upendo ndipo maendeleo yatakuwepo. Kinyume cha upendo ni chuki, na pale panapokuwepo chuki hakuna maendeleo kwa kuwa hakuna maono ya pamoja.Amesema Makwaia wa III

Tamasha la Sanjo ya Busiya limejumuisha mashindano ya ngoma na muziki wa asili kutoka ndani na nje ya Wilaya ya Kishapu, maonesho ya vyakula vya jadi vya Kisukuma, mavazi ya asili, na matumizi ya vyombo vya kijadi. Mgeni rasmi, Mtemi Makwaia wa III, alikabidhi zawadi kwa vikundi vilivyoshiriki, wanawake waliotoa mchango mkubwa katika mavazi na mapishi ya asili, na watoa huduma mbalimbali wa kitamaduni.

Mtemi wa Busiya Chifu Faustine Makwaia wa III Utemi wenye makao yake makuu Ukenyenge Wilayani  Kishapu Mkoani Shinyanga akizungumza na wananchi kwenye sherehe za tamasha la Sanjo ya Busiya Julai 7,2025

Kwa ujumla, tamasha hilo limeonyesha mshikamano wa jamii, kuenzi mila na desturi za Kisukuma, pamoja na kuhimiza matumizi ya rasilimali za asili kwa maendeleo endelevu.

Matangazo

  • TAARIFA YA MTIRIRIKO WA FEDHA KWA KIPINDI KILICHOISHIA TAREHE 30 JUNE. 2022 August 14, 2023
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI November 03, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MFAMASIA December 14, 2021
  • Orodha ya Walioitwa kwenye Usaili September 20, 2024
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • DC KISHAPU AWATAKA WANANCHI KUTUMIA KWA TIJA MBEGU ZILIZOBARIKIWA BUSIYA

    July 08, 2025
  • KISHAPU YAGAWA CHANJO 300,000 YA KUKU WA KIENYEJI

    July 01, 2025
  • VIJIJI 16 VINAVYOZUNGUKA MIGODI KISHAPU MIGOGORO YA ARDHI KUKOMESHWA

    June 27, 2025
  • TAKUKURU YAZINDUA JENGO JIPYA KISHAPU, LAWAPA WANANCHI IMANI NA UJASIRI KUPINGA RUSHWA

    June 26, 2025
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa