• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
    • Idara
      • Fedha
      • Rasilimali watu
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
  • Nyaraka
    • Fomu za kujinga na Kidato cha Tano
      • Shule ya Sekondari Kishapu
      • Shule ya Sekondari Shinyanga
    • Mpango wa bajeti wa mwaka 2021/2022
    • Matangazo
    • Sheria ndogo ya ushuru wa huduma
    • Mifumo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
      • Uvuvi wa Samaki katika Bwawa la Songwa, Bwawa mhumbu
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Mhe. William Luhende Jijimya - Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Mhe. Francis Manyanda - Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Mhe. Joel Ndettoson - Diwani kata ya Kishapu
      • Mhe. Mohamed Aman - Diwani kata ya Ndoleleji
      • Mhe. Lucas Nkende - Diwani kata ya Mwamashele
      • Mhe. Pontias Daud - Diwani kata ya Mwataga
      • Mhe. James Kasomi - Diwani kata ya Bubiki
      • Mhe. Bushi Mpina - Diwani kata ya Mwamalasa
      • Mhe. Nyama Kisinza - Diwani kata ya Somagedi
      • Mhe. Mashini W. Washima - Diwani kata ya Uchunga
      • Mhe. Anderson Mandia - Diwani kata ya Ukenyenge
      • Mhe. Edward Manyama - Diwani kata ya Kiloleli
      • Mhe. Reuben Siyabo - Diwani kata ya Bupigi
      • Mhe. Bujiku Nyanda - Diwani kata ya Mwaweja
      • Mhe. Michael Paul - Diwani kata ya Shagihilu
      • Mhe. Luhende S. Luhende - Diwani kata ya Lagana
      • Mhe. Richard Dominico - Diwani kata ya Talaga
      • Mhe. James Kamuga - Diwani kata ya Igaga
      • Mhe. Lameck Nsubata - Diwani kata ya Itilima
      • Mhe. Mpemba Malangahe - Diwani kata ya Bunambiyu
      • Mhe. Makenzi Charles - Diwani kata ya Busangwa
      • Mhe. Nestory Kalugula - Diwani kata ya Ngofila
      • Mhe. Lwinzi Kidiga - Diwani kata ya Maganzo
      • Mhe. Samson Gelewa - Diwani kata ya Mwasubi
      • Mhe. Sarah Marco - Diwani kata ya Idukilo
      • Mhe. Enock Bundala - Diwani kata ya Masanga
      • Mhe. Thabidha Mmbando - Diwani kata ya Mwakipoya
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Mwenyekiti wa Halmashauri
  • miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
  • Kituo Cha Habari
    • maktaba ya picha
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa za Vyombo vya Habari
  • Maeneo
    • Kata
      • Orodha ya Kata
    • Tarafa
      • Orodha ya Tarafa
    • Vijiji
      • Orodha ya Vijiji

DC KISHAPU AZINDUA KAMPENI YA CHANJO NA UTAMBUZI WA MIFUGO

Posted on: September 16th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Peter Masindi akizindua kampeni ya chanjo na utambuzi wa mifugo.

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga, Mhe. Peter Masindi ambaye pia ni mgeni rasmi katika uzinduzi wa zoezi la chanjo Wilayani humo, amezindua rasmi kampeni ya chanjo na utambuzi wa mifugo, akieleza kuwa ni hatua muhimu katika kuboresha afya ya mifugo na kuongeza ushindani wa sekta hiyo nchini Tanzania.

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Peter Masindi akiwa sehemu ya zoezi la utoaji chanjo kwa ng'ombe

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo katika kata ya Mwamashele, Mhe. Masindi amesema kampeni hiyo inatekelezwa kwa msaada wa ruzuku ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, na inalenga kulinda ng’ombe, mbuzi, kondoo na kuku dhidi ya magonjwa hatari, sambamba na kuitambua rasmi mifugo hiyo kitaifa.

Kupitia ruzuku hiyo, chanjo ya homa ya mapafu kwa ng’ombe inatolewa kwa shilingi 500 tu, ikiwa ni nusu ya bei ya kawaida. Chanjo dhidi ya ugonjwa wa Sotoka kwa mbuzi na kondoo zinatolewa kwa shilingi 300 badala ya 600, huku hereni za utambuzi zikitolewa bila malipo.


Mratibu wa zoezi hilo Wilaya ya Kishapu, Bw. John Mchele, amesema wamepokea chanjo 450,000 dhidi ya homa ya mapafu kwa ng’ombe na chanjo 442,000 dhidi ya ugonjwa wa Sotoka kwa mbuzi na kondoo.

Mratibu wa chanjo ya mifugo  Wilaya ya Kishapu Bw. John Mchele 

Kwa upande wake, Mkuu wa Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Bw. Mwita Mwijarubi Mwita, akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Kishapu, ameeleza kuwa kampeni ya awali ya chanjo kwa kuku imefikia asilimia 87 ya utekelezaji. “Chanjo ni bure, na mwitikio umekuwa mzuri sana,” amesema.

Mkuu wa idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Bw. Mwita .M. Mwita

Mhe. Masindi amewasihi wafugaji wote kushiriki kikamilifu katika kampeni hiyo ili kusaidia Serikali kuboresha huduma za mifugo ikiwemo upatikanaji wa dawa za mifugo, malisho bora na fursa za masoko kitaifa na kimataifa. “Tujitahidi wote, hakuna haja ya mtu kuficha ng’ombe wake. Ukificha mifugo wasiende kuchanjwa, unaficha takwimu zinazosaidia serikali kuboresha ustawi wa wafugaji,” amesisitiza.

Mhe. Masindi akiwasihi wananchi kutoa ushirikiano kwenye zoezi la utoaji wa chanjo ya mifugo yao

Aidha, wananchi wa Kata ya Mwamashele, wamepongeza juhudi za Serikali katika kuboresha sekta ya mifugo nchini, na kuahidi kutoa ushirikiano katika zoezi la chanjo na utambuzi wa mifugo. “Tunashukuru Serikali kwa kutuletea chanjo kwa bei nafuu, hii inalinda mifugo yetu na tunatarajia kukuza uchumi wetu,” Bw. Khalid Hamad .

Bw. Khalid Hamad, mfugaji na mkazi wa Kata ya Mwamashele

Kampeni ya chanjo na utambuzi wa mifugo inaendelea katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Kishapu, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kitaifa za kuimarisha sekta ya mifugo kwa maendeleo endelevu ya jamii.

Matangazo

  • TAARIFA YA MTIRIRIKO WA FEDHA KWA KIPINDI KILICHOISHIA TAREHE 30 JUNE. 2022 August 14, 2023
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI November 03, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MFAMASIA December 14, 2021
  • Orodha ya Walioitwa kwenye Usaili September 20, 2024
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • DC KISHAPU AZINDUA KAMPENI YA CHANJO NA UTAMBUZI WA MIFUGO

    September 16, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA VITENDO (DEREVA DARAJA II)

    September 16, 2025
  • MKURUGENZI JOHNSON AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA DARASA LA SABA

    September 09, 2025
  • DED JOHNSON ATAKA USHIRIKIANO KUINUA ELIMU SHULE YA MSINGI NG'WANIMA

    September 04, 2025
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa