• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
    • Idara
      • Fedha
      • Rasilimali watu
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
  • Nyaraka
    • Fomu za kujinga na Kidato cha Tano
      • Shule ya Sekondari Kishapu
      • Shule ya Sekondari Shinyanga
    • Mpango wa bajeti wa mwaka 2021/2022
    • Matangazo
    • Sheria ndogo ya ushuru wa huduma
    • Mifumo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
      • Uvuvi wa Samaki katika Bwawa la Songwa, Bwawa mhumbu
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Mhe. William Luhende Jijimya - Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Mhe. Francis Manyanda - Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Mhe. Joel Ndettoson - Diwani kata ya Kishapu
      • Mhe. Mohamed Aman - Diwani kata ya Ndoleleji
      • Mhe. Lucas Nkende - Diwani kata ya Mwamashele
      • Mhe. Pontias Daud - Diwani kata ya Mwataga
      • Mhe. James Kasomi - Diwani kata ya Bubiki
      • Mhe. Bushi Mpina - Diwani kata ya Mwamalasa
      • Mhe. Nyama Kisinza - Diwani kata ya Somagedi
      • Mhe. Mashini W. Washima - Diwani kata ya Uchunga
      • Mhe. Anderson Mandia - Diwani kata ya Ukenyenge
      • Mhe. Edward Manyama - Diwani kata ya Kiloleli
      • Mhe. Reuben Siyabo - Diwani kata ya Bupigi
      • Mhe. Bujiku Nyanda - Diwani kata ya Mwaweja
      • Mhe. Michael Paul - Diwani kata ya Shagihilu
      • Mhe. Luhende S. Luhende - Diwani kata ya Lagana
      • Mhe. Richard Dominico - Diwani kata ya Talaga
      • Mhe. James Kamuga - Diwani kata ya Igaga
      • Mhe. Lameck Nsubata - Diwani kata ya Itilima
      • Mhe. Mpemba Malangahe - Diwani kata ya Bunambiyu
      • Mhe. Makenzi Charles - Diwani kata ya Busangwa
      • Mhe. Nestory Kalugula - Diwani kata ya Ngofila
      • Mhe. Lwinzi Kidiga - Diwani kata ya Maganzo
      • Mhe. Samson Gelewa - Diwani kata ya Mwasubi
      • Mhe. Sarah Marco - Diwani kata ya Idukilo
      • Mhe. Enock Bundala - Diwani kata ya Masanga
      • Mhe. Thabidha Mmbando - Diwani kata ya Mwakipoya
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Mwenyekiti wa Halmashauri
  • miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
  • Kituo Cha Habari
    • maktaba ya picha
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa za Vyombo vya Habari
  • Maeneo
    • Kata
      • Orodha ya Kata
    • Tarafa
      • Orodha ya Tarafa
    • Vijiji
      • Orodha ya Vijiji

DC MASINDI ATAKA MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025 ILINDWE

Posted on: September 25th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Mhe.Peter Masindi (kulia) akimkabidhi cheti cha pongezi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu Bw.Emmanuel Johnson(kushoto) katika kikao cha kuvunja kamati ya Mwenge wa Uhuru uliopita Wilayani humo mnamo Agosti 8,2025 walipokuwa kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri Septemba 25,2025

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Mkoani Shinyanga, Mhe. Peter Masindi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Mwenge wa Uhuru Wilayani humo ametoa wito kwa Watuishi na wananchi kuhakikisha miradi yote iliyopitiwa na Mwenge wa Uhuru inalindwa na kuendelezwa kwa manufaa ya jamii.

Akizungumza wakati akivunja Kamati ya Mwenge Septemba 25,2025 Katika ukumbi wa Halmashauri Mhe. Masindi amesema Mwenge umekuwa chachu ya mshikamano na maendeleo, huku pia ukihimiza Watanzania kushiriki kikamilifu kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29,2025.

“Uwezo wa kujenga Taifa lenye maendeleo na mabadiliko upo mikononi mwa wananchi kupitia kuchagua viongozi bora. Ni muhimu kuendelea kuishi kwa upendo, mshikamano na kukubali matokeo ya uchaguzi kwa utulivu na amani,” amesema Mhe. Masindi.

Aidha, amesisitiza kuwa wananchi hawapaswi kushirikiana na watu wanaolenga kuleta mafarakano, bali waendelee kushirikiana kwa mshikamano na umoja ili kulinda amani ya Taifa kipindi cha uChaguzi na baada ya Uchaguzi.

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Wilaya amewataka wananchi waendelee kujitokeza kwa wingi katika mapokezi na mkesha wa Mwenge wa Uhuru mwaka ujao wa 2026, huku akiwasihi watumishi washirikiane kwa upendo na mshikamano ili kuhakikisha maandalizi yanakuwa bora zaidi.

Akihitimisha hotuba yake, Mhe. Masindi amekabidhi vyeti vya pongezi kwa Kamati zote zilizoshiriki maandalizi ya Mwenge wa Uhuru pamoja na watu maalum waliotoa mchango mkubwa kufanikisha zoezi hilo.

Ikumbukwe kuwa Mwenge wa Uhuru ulipitia Jumla ya miradi saba(7) Wilayani humo ikiwemo Mwenge wa uhuru ulikagua Kikundi cha Vijana Wachapakazi kilichopo Kata ya Songwa kinatekeleza mradi wa kilimo cha nyanya kwenye ekari tano kwa mkopo wa Shilingi 20,752,209/= kutoka asilimia 10 ya mapato ya Halmashauri,Mwenge huo pia umezindua na kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa ujenzi wa vyumba saba vya madarasa na matundu nane ya vyoo katika shule mpya ya sekondari ya Masagala kwa gharama ya Shilingi 196,400,000.

Mwenge huo ulizindua na kuweka jiwe la msingi mradi wa Maji uliotekelezwa na Serikali kupitia Mradi huo umehusisha ujenzi wa tenki la maji la lita 100,000, vituo vitatu vya kuchotea maji, mtandao wa bomba wa mita 2,670, uzio na alama za bomba, kwa gharama ya Shilingi milioni 445.05 kupitia Programu ya Malipo kwa Matokeo (P for R).Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) imekamilisha ujenzi wa mradi wa maji ya Ziwa Victoria kutoka Nyenze hadi Ng’wangh’olo Wilayani Kishapu, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa dhamira ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kumtua mama ndoo kichwani.

Pia Mwenge wa Uhuru ulitembelea na kuweka jiwe la msingi katika Zahanati ya Wela iliyopo Kata ya Bupigi ikiwa ni zao la jitihada za wananchi waliokuwa wakitembea zaidi ya kilomita 15 kufuata huduma za afya, ambapo mwaka 2011 walichangisha Shilingi 10,500,000/= kuanzisha ujenzi huo.Serikali kupitia Serikali Kuu na mapato ya ndani ya Halmashauri imechangia Shilingi 75,000,000/= kukamilisha ujenzi huo unaojumuisha jengo la zahanati, vyoo matundu matano, kichomea taka na Placenta Pit.Mradi huu wenye thamani ya Shilingi 85,500,000/= unatarajiwa kuhudumia wananchi zaidi ya 7,600 wa Kata ya Bupigi na Vijiji jirani.

Mwenge wa Uhuru mwaka 2025 ulikagua na kuweweka jiwe la msingi katika bweni la wasichana katika Shule ya Sekondari Mwamashele mradi ulianzishwa na wananchi mwaka 2019 kwa lengo la kuwalinda watoto wa kike dhidi ya changamoto za umbali mrefu, mimba za utotoni, unyanyasaji na utoro.Mradi huo unathamani ya Shilingi 88,105,200/=

Mwenge wa Uhuru uliweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa barabara ya DED - DC yenye urefu wa kilomita 1 kwa kiwango cha lami nyepesi (DSD), mradi unaogharimu zaidi ya shilingi milioni 688. Mradi huo unatekelezwa na TARURA  pamoja na Mradi wa mwekezaji Mzawa Wilayani humo Mradi wa Kituo cha mafuta cha Bin Salum.




Matangazo

  • TAARIFA YA MTIRIRIKO WA FEDHA KWA KIPINDI KILICHOISHIA TAREHE 30 JUNE. 2022 August 14, 2023
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI November 03, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MFAMASIA December 14, 2021
  • Orodha ya Walioitwa kwenye Usaili September 20, 2024
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI

    November 21, 2025
  • WATUMISHI KISHAPU WAPEWA MAFUNZO YA ELIMU YA FEDHA NA KUKABILIANA NA CHANGAMOTO YA AFYA YA AKILI

    November 20, 2025
  • DC,DED NA MSIMAMIZI WA UCHAGUZI JIMBO LA KISHAPU WAUNGANA NA WANANCHI KUPIGA KURA

    October 29, 2025
  • WASIMAMIZI WA VITUO KISHAPU WAONYWA KUTOKUWA CHANZO CHA MIGOGORO

    October 27, 2025
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa