• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Utawala
      • Biashara, Viwanda na Uwekezaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya jamii
      • Afya
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Tehama
      • Utamaduni, Sanaa na Michezo
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Usafi wa Mazingira na Udhibiti Taka
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Kilimo na Mifugo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya kuonana na mwenyekiti wa Halmashauri
    • Ratiba ya vikao vya kisheria vya MSM
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Sheria ndogo ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya picha na video za shughuli za maendeleo

DC MASINDI AWATAKA WAGOMBEA KUTUMIA LUGHA YA STAHA JUKWAANI AHITIMISHA ZIARA

Posted on: August 27th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Mhe.Peter Masindi akizungumza kwenye mkutano wa hadhara wakati wa ziara yake ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi Tarafa ya Mondo Agosti 27,2025

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga, Mhe. Peter Masindi amewataka wagombea wote wa Jimbo la Kishapu wanaoelekea kuanza kampeni za uchaguzi kutumia lugha ya heshima na sera zenye kujenga badala ya matusi au kejeli wanapokuwa jukwaani.


Akizungumza Agosti 27, 2025 katika ziara yake ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi wa Tarafa ya Mondo,Masindi amesema siasa za matusi hazina tija, na kuwakumbusha wagombea kwamba kuna maisha baada ya uchaguzi, hivyo hakuna sababu ya kuchochea uhasama.

“Wananchi wanataka kusikia sera zinazogusa maisha yao na namna mtakavyoboresha huduma za kijamii. Huu sio muda wa matusi wala kejeli. Tufanye siasa zenye heshima na staha,” amesema Masindi.

Aidha, amewataka wananchi kusikiliza kwa makini sera za wagombea na kufanya maamuzi sahihi ifikapo Oktoba 29, 2025, akisisitiza kuwa msingi wa maendeleo upo mikononi mwao. Vilevile, Masindi amewahimiza wananchi kuendelea kuchangamkia fursa za kiuchumi, kufanya kazi kwa bidii, kuishi kwa nidhamu na kumtanguliza Mungu katika kila jambo.

Afisa Tarafa ya Mondo Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga Atka Faki akizungumza kwenye mkutano wa hadhara wa Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe.Peter Masindi wa kusikiliza na kutatua kero za wananchi Agosti 27,2025

Mkuu huyo wa Wilaya amewataka wazazi pia kuhakikisha wanalea watoto wao kwenye maadili, nidhamu na ujasiri ili wawe nguzo ya maendeleo ya jamii.

Katika wito wake kwa jamii, amewahimiza kushiriki kikamilifu katika miradi ya maendeleo ikiwemo uanzishaji wa maboma ya madarasa, nyumba za walimu, vituo vya afya pamoja na kulinda miundombinu ya maji na umeme iliyowekwa kwa manufaa ya wananchi.

Mbali na hayo, amewahimiza watendaji wa Halmashauri na wakuu wa taasisi zingine za Umma na za fedha kuhakikisha wanafanya kazi kwa maslahi ya wananchi na kuwasogezea huduma muhimu ambazo serikali imekusudia kuwafikishia.

Aidha, wananchi wameelimishwa kuhusu huduma za mikopo zinazotolewa na Halmashauri na Taasisi ya Kifedha (CRDB), huku wakihimizwa kuchangamkia fursa hizo ili kuepuka kuingia kwenye mikopo isiyo rasmi inayochochea migogoro ya kifamilia.

Mhe.Masindi amehitimisha ziara yake ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi katika tarafa ya Mondo Vijiji vya Nyasamba Kata ya Bubiki, Mwajiningu Kata ya Busongwa,Itongoitale Kata ya Mwasubi pamoja na Kijiji cha Idukilo Kata ya Idukilo.

 

Mkutano wa hadhara wa Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Mhe.Peter Masindi wa kusikiliza na kutatua kero kwa wananchi katika   Kijiji cha Nyasamba kilichoko Kata ya Bubiki Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga Agosti 27,2025

Mkutano wa hadhara wa Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Mhe.Peter Masindi wa kusikiliza na kutatua kero kwa wananchi katika   Kijiji cha Mwajiningu Kata ya Busongwa Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga Agosti 27,2025


Mkutano wa hadhara wa Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Mhe.Peter Masindi wa kusikiliza na kutatua kero kwa wananchi katika  Kijiji cha Itongoitale Kata ya Mwasubi Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga Agosti 27,2025

 

Mkutano wa hadhara wa Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Mhe.Peter Masindi wa kusikiliza na kutatua kero kwa wananchi katika Kijiji cha Idukilo Kata ya Idukilo Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga Agosti 27,2025

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA February 16, 2026
  • TANGAZO LA MWALIKO WA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI January 20, 2026
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI December 22, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI November 21, 2025
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • CP. HAMDUNI AZINDUA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI KISHAPU, BEI YA CHOROKO YAPAA

    March 03, 2026
  • KILELE CHA TAMASHA LA AMANI NA MAENDELEO KISHAPU CHAFANA, MHE. MAYENGA ATOA WITO WA MSHIKAMANO

    February 28, 2026
  • DC MASINDI AZINDUA BIMA YA AFYA KWA WOTE KISHAPU

    February 27, 2026
  • MWENYEKITI KISHAPU ARIDHISHWA NA HUDUMA ZA AFYA

    February 19, 2026
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa