• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
    • Idara
      • Fedha
      • Rasilimali watu
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
  • Nyaraka
    • Fomu za kujinga na Kidato cha Tano
      • Shule ya Sekondari Kishapu
      • Shule ya Sekondari Shinyanga
    • Mpango wa bajeti wa mwaka 2021/2022
    • Matangazo
    • Sheria ndogo ya ushuru wa huduma
    • Mifumo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
      • Uvuvi wa Samaki katika Bwawa la Songwa, Bwawa mhumbu
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Mhe. William Luhende Jijimya - Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Mhe. Francis Manyanda - Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Mhe. Joel Ndettoson - Diwani kata ya Kishapu
      • Mhe. Mohamed Aman - Diwani kata ya Ndoleleji
      • Mhe. Lucas Nkende - Diwani kata ya Mwamashele
      • Mhe. Pontias Daud - Diwani kata ya Mwataga
      • Mhe. James Kasomi - Diwani kata ya Bubiki
      • Mhe. Bushi Mpina - Diwani kata ya Mwamalasa
      • Mhe. Nyama Kisinza - Diwani kata ya Somagedi
      • Mhe. Mashini W. Washima - Diwani kata ya Uchunga
      • Mhe. Anderson Mandia - Diwani kata ya Ukenyenge
      • Mhe. Edward Manyama - Diwani kata ya Kiloleli
      • Mhe. Reuben Siyabo - Diwani kata ya Bupigi
      • Mhe. Bujiku Nyanda - Diwani kata ya Mwaweja
      • Mhe. Michael Paul - Diwani kata ya Shagihilu
      • Mhe. Luhende S. Luhende - Diwani kata ya Lagana
      • Mhe. Richard Dominico - Diwani kata ya Talaga
      • Mhe. James Kamuga - Diwani kata ya Igaga
      • Mhe. Lameck Nsubata - Diwani kata ya Itilima
      • Mhe. Mpemba Malangahe - Diwani kata ya Bunambiyu
      • Mhe. Makenzi Charles - Diwani kata ya Busangwa
      • Mhe. Nestory Kalugula - Diwani kata ya Ngofila
      • Mhe. Lwinzi Kidiga - Diwani kata ya Maganzo
      • Mhe. Samson Gelewa - Diwani kata ya Mwasubi
      • Mhe. Sarah Marco - Diwani kata ya Idukilo
      • Mhe. Enock Bundala - Diwani kata ya Masanga
      • Mhe. Thabidha Mmbando - Diwani kata ya Mwakipoya
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Mwenyekiti wa Halmashauri
  • miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
  • Kituo Cha Habari
    • maktaba ya picha
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa za Vyombo vya Habari
  • Maeneo
    • Kata
      • Orodha ya Kata
    • Tarafa
      • Orodha ya Tarafa
    • Vijiji
      • Orodha ya Vijiji

HELPAGE YAENDESHA MAJADILIANO KISHAPU KUKOMESHA UKATILI WA KIJINSIA

Posted on: May 13th, 2025

Shirika lisilo la kiserikali la HelpAge Tanzania limeendesha majadiliano ya makundi rika katika Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, mkoani Shinyanga, kwa lengo la kukuza usawa wa kijinsia, kutokomeza mila kandamizi, na kuimarisha afya ya uzazi, hususan kwa wanawake, wasichana na watu wenye ulemavu.

Tukio hilo ni sehemu ya utekelezaji wa Mradi wa Chaguo Langu, Haki Yangu, unaofadhiliwa na Serikali ya Finland na kuratibiwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu (UNFPA), kwa kushirikiana na wizara pamoja na taasisi mbalimbali.

Akizungumza wakati wa mjadala huo, Mkuu wa Programu wa HelpAge Tanzania, Leonard Ndamgoba, alisema shirika hilo limeandaa mwongozo maalum wa majadiliano kati ya makundi ya wazee na vijana ili kukabiliana na changamoto zinazokumba jamii, hususan ukeketaji, ndoa za utotoni na ukatili wa kijinsia.

"Kupitia mijadala ya makundi rika, tunatengeneza jukwaa la kuleta mabadiliko ya kweli kutoka kizazi kimoja kwenda kingine," alisema Ndamgoba na kuongeza kuwa wawezeshaji waliopatiwa mafunzo wataendesha mijadala hiyo katika mikutano ya hadhara, vikundi vya kijamii, na matukio ya kijamii kama misiba na harusi, huku wakijengewa uwezo wa kuendeleza juhudi hizo kwa muda mrefu.

Kwa mujibu wa Ndamgoba, lengo ni kuvunja mitazamo potofu ya kijinsia kwa kujenga mazingira salama ya mazungumzo yanayowawezesha wanawake na wasichana, wakiwemo wenye ulemavu, kudai haki zao katika nyanja za elimu, uchumi, afya ya uzazi na ushiriki wa kijamii.

Naye Mratibu wa Mradi wa Chaguo Langu, Haki Yangu ambaye pia ni Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Ibrahim Sakulia, alitoa wito kwa jamii kushiriki kikamilifu katika hatua za utambuzi na utatuzi wa changamoto za ukatili na mila kandamizi.


“Tunahitaji wananchi washiriki kikamilifu mijadala hii kwa sababu wao ndio chachu ya mabadiliko tunayoyakusudia,” alisema Sakulia.

Katika mafunzo hayo, wawakilishi wa makundi ya vijana na wazee kutoka kata za Idukilo, Mwamalasa na Mwamashele walipatiwa mbinu za kuendesha midahalo ya makundi rika katika maeneo yao, kwa lengo la kuchochea mijadala ya wazi kuhusu ukatili wa kijinsia, usawa wa kijinsia na heshima kwa haki za binadamu.

Kwa upande wake, Kaimu Mratibu wa Huduma za Mama na Mtoto katika Hospitali ya Wilaya ya Kishapu, Hilda Ebunka, alisema hali ya mimba za utotoni imeanza kupungua ikilinganishwa na miaka ya nyuma, jambo linaloashiria mafanikio ya juhudi za pamoja kati ya serikali na mashirika ya kiraia.

Afisa Ustawi wa Jamii wa halmashauri hiyo, Paul Lupolaso, alisema ofisi yake hupokea kesi nyingi za ukatili wa kijinsia, zikiwemo ndoa za utotoni, ukatili wa kimwili na unyanyasaji wa kiuchumi, hasa kwa wanawake na watoto.


"Ndoa za utotoni huwakosesha watoto haki ya elimu, afya bora na maendeleo ya baadaye," alibainisha Lupolaso.


Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto wa Wilaya ya Kishapu, Inspekta Rose Mbwambo, alisema dawati hilo limekuwa msaada mkubwa kwa waathirika wa ukatili wa kijinsia, akihimiza jamii kushirikiana na jeshi la polisi kwa kutoa taarifa na ushahidi mapema.

“Tunahitaji jamii kushirikiana nasi kwa ukaribu. Wananchi wafahamu kuwa kazi ya dawati letu ni kusaidia, siyo kuadhibu,” alisisitiza Inspekta Mbwambo.


Aidha, aliwasihi wazazi na walezi kuwafundisha watoto kuhusu haki zao na kuhakikisha wanawalinda dhidi ya ukatili wa aina yoyote.

Baadhi ya wananchi waliotoa maoni yao walisema kuwa mafunzo hayo yamewapa maarifa mapya kuhusu mbinu bora za kupambana na ukatili wa kijinsia, na wakaahidi kuyatumia katika jamii zao ili kuleta mabadiliko chanya.


HelpAge Tanzania inatarajia kuwa mwongozo wa mijadala ya makundi rika utachangia kuleta mabadiliko ya kijamii na kiutamaduni kwa ajili ya kujenga jamii yenye usawa wa kijinsia, heshima kwa haki za binadamu, na uhuru kwa kila mwanajamii – wakiwemo wanawake, watoto, wazee na watu wenye ulemavu.

Matangazo

  • TAARIFA YA MTIRIRIKO WA FEDHA KWA KIPINDI KILICHOISHIA TAREHE 30 JUNE. 2022 August 14, 2023
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI November 03, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MFAMASIA December 14, 2021
  • Orodha ya Walioitwa kwenye Usaili September 20, 2024
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • CPA. MAKALA AIPONGEZA SERIKALI MAENDELEO KISHAPU – BUTONDO AOMBA DED ASIONDOLEWE

    May 23, 2025
  • DC KISHAPU AWAONYA WAVURUGA AMANI KATA YA MWASUBI NA BUNAMBIYU

    May 16, 2025
  • SERIKALI KUTUMIA DOLA MILIONI 77.4 KUZIWEZESHA KAYA DUNI LAKI MBILI NA ELFU 60 KILIMO NA UVUVI TANZANIA BARA

    May 15, 2025
  • WILAYA YA KISHAPU YAANZA MAANDALIZI YA KUPOKEA MWENGE WA UHURU AGOSTI 8, 2025

    May 14, 2025
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa