• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
    • Idara
      • Fedha
      • Rasilimali watu
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
  • Nyaraka
    • Fomu za kujinga na Kidato cha Tano
      • Shule ya Sekondari Kishapu
      • Shule ya Sekondari Shinyanga
    • Mpango wa bajeti wa mwaka 2021/2022
    • Matangazo
    • Sheria ndogo ya ushuru wa huduma
    • Mifumo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
      • Uvuvi wa Samaki katika Bwawa la Songwa, Bwawa mhumbu
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Mhe. William Luhende Jijimya - Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Mhe. Francis Manyanda - Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Mhe. Joel Ndettoson - Diwani kata ya Kishapu
      • Mhe. Mohamed Aman - Diwani kata ya Ndoleleji
      • Mhe. Lucas Nkende - Diwani kata ya Mwamashele
      • Mhe. Pontias Daud - Diwani kata ya Mwataga
      • Mhe. James Kasomi - Diwani kata ya Bubiki
      • Mhe. Bushi Mpina - Diwani kata ya Mwamalasa
      • Mhe. Nyama Kisinza - Diwani kata ya Somagedi
      • Mhe. Mashini W. Washima - Diwani kata ya Uchunga
      • Mhe. Anderson Mandia - Diwani kata ya Ukenyenge
      • Mhe. Edward Manyama - Diwani kata ya Kiloleli
      • Mhe. Reuben Siyabo - Diwani kata ya Bupigi
      • Mhe. Bujiku Nyanda - Diwani kata ya Mwaweja
      • Mhe. Michael Paul - Diwani kata ya Shagihilu
      • Mhe. Luhende S. Luhende - Diwani kata ya Lagana
      • Mhe. Richard Dominico - Diwani kata ya Talaga
      • Mhe. James Kamuga - Diwani kata ya Igaga
      • Mhe. Lameck Nsubata - Diwani kata ya Itilima
      • Mhe. Mpemba Malangahe - Diwani kata ya Bunambiyu
      • Mhe. Makenzi Charles - Diwani kata ya Busangwa
      • Mhe. Nestory Kalugula - Diwani kata ya Ngofila
      • Mhe. Lwinzi Kidiga - Diwani kata ya Maganzo
      • Mhe. Samson Gelewa - Diwani kata ya Mwasubi
      • Mhe. Sarah Marco - Diwani kata ya Idukilo
      • Mhe. Enock Bundala - Diwani kata ya Masanga
      • Mhe. Thabidha Mmbando - Diwani kata ya Mwakipoya
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Mwenyekiti wa Halmashauri
  • miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
  • Kituo Cha Habari
    • maktaba ya picha
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa za Vyombo vya Habari
  • Maeneo
    • Kata
      • Orodha ya Kata
    • Tarafa
      • Orodha ya Tarafa
    • Vijiji
      • Orodha ya Vijiji

MCHAKATO WAANZA UJENZI DAMPO LA KISASA KISHAPU KUIMARISHA USAFI WA MAZINGIRA

Posted on: July 26th, 2025

Afisa mazingira Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga Charles Kanwakabo

Katika kuhakikisha mazingira yanabaki kuwa safi na salama kwa afya ya jamii, Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga imepiga hatua muhimu kwa kuanzisha mchakato wa ujenzi wa dampo la kisasa na la kudumu katika eneo la Sulagi, hatua inayolenga kuimarisha usimamizi wa taka na kulinda mazingira kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

Afisa Mazingira wa Wilaya ya Kishapu, Charles Kanwakabo, amesema desturi ya kufanya usafi wa maeneo yote ya shughuli za kijamii imeendelea kuungwa mkono kwa kiwango cha kuridhisha.

Ametoa pongezi kwa wananchi, wanafunzi na viongozi waliojitokeza kushiriki zoezi la usafi lililofanyika Julai 26, 2025, akibainisha kuwa hali ya usafi imefikia kiwango cha asilimia 85 ishara ya mwamko mpya wa utunzaji wa mazingira miongoni mwa jamii.

“Tunashukuru wananchi, viongozi na wanafunzi wa Kishapu Sekondari kwa kushiriki kikamilifu. Licha ya mafanikio haya, tunasisitiza kuwa usafi usiwe tu wa kila mwisho wa mwezi bali uwe sehemu ya maisha ya kila siku,” amesema Kanwakabo.

Aidha, ametoa wito kwa wakazi wa Kishapu kuacha kusubiri maagizo ya viongozi ili kushiriki katika usafi, bali kujenga tabia endelevu ya kuhifadhi mazingira kwa maslahi ya pamoja.

Kwa upande wake, Mtendaji wa Mamlaka ya Mji Mdogo Kishapu, Godwin Everygist, amesema kuwa tayari mamlaka imeanza mchakato wa ujenzi wa dampo la kisasa katika eneo la Sulagi, hatua inayolenga kupunguza changamoto za utupaji holela wa taka na kukuza miji safi na salama.

Mtendaji wa Mamlaka ya Mji Mdogo Kishapu, Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga Godwin Everygist

“Katika kipindi hiki cha mpito, tunasisitiza uhifadhi sahihi wa taka kwenye dampo la muda, huku tukielekea kwenye mji wa kisasa wenye miundombinu bora ya usimamizi wa taka,” amesema Everygist.

Ameongeza kuwa ni muhimu kwa kila kaya kuhakikisha inakuwa na choo bora na salama ili kuzuia uharibifu wa mazingira na milipuko ya magonjwa yanayochochewa na uchafu.

Baadhi ya Wanafunzi kutoka Shule ya Sekondari Kishapu Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga wakifanya usafi

Zoezi la usafi wa pamoja lililofanyika Julai 26 limehusisha maeneo muhimu ikiwemo Soko la Swalala, uwanja wa Shirecu, pamoja na dampo la muda, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kujenga utamaduni wa kudumu wa usafi na kujali afya ya jamii katika Wilaya ya Kishapu.


Matangazo

  • TAARIFA YA MTIRIRIKO WA FEDHA KWA KIPINDI KILICHOISHIA TAREHE 30 JUNE. 2022 August 14, 2023
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI November 03, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MFAMASIA December 14, 2021
  • Orodha ya Walioitwa kwenye Usaili September 20, 2024
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • MCHAKATO WAANZA UJENZI DAMPO LA KISASA KISHAPU KUIMARISHA USAFI WA MAZINGIRA

    July 26, 2025
  • RC MHITA AFANYA ZIARA YA KIKAZI KISHAPU

    July 22, 2025
  • WANANCHI 1,200 VIJIJI VYA MFANO KISHAPU WAPEWA HATI MILKI ZA KIMILA

    July 23, 2025
  • LISHE BORA YAPAA SHULENI KISHAPU

    July 16, 2025
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa