• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Utawala
      • Biashara, Viwanda na Uwekezaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya jamii
      • Afya
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Tehama
      • Utamaduni, Sanaa na Michezo
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Usafi wa Mazingira na Udhibiti Taka
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Kilimo na Mifugo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya kuonana na mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya picha na video za shughuli za maendeleo

MCHAKATO WAANZA UJENZI DAMPO LA KISASA KISHAPU KUIMARISHA USAFI WA MAZINGIRA

Posted on: July 26th, 2025

Afisa mazingira Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga Charles Kanwakabo

Katika kuhakikisha mazingira yanabaki kuwa safi na salama kwa afya ya jamii, Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga imepiga hatua muhimu kwa kuanzisha mchakato wa ujenzi wa dampo la kisasa na la kudumu katika eneo la Sulagi, hatua inayolenga kuimarisha usimamizi wa taka na kulinda mazingira kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

Afisa Mazingira wa Wilaya ya Kishapu, Charles Kanwakabo, amesema desturi ya kufanya usafi wa maeneo yote ya shughuli za kijamii imeendelea kuungwa mkono kwa kiwango cha kuridhisha.

Ametoa pongezi kwa wananchi, wanafunzi na viongozi waliojitokeza kushiriki zoezi la usafi lililofanyika Julai 26, 2025, akibainisha kuwa hali ya usafi imefikia kiwango cha asilimia 85 ishara ya mwamko mpya wa utunzaji wa mazingira miongoni mwa jamii.

“Tunashukuru wananchi, viongozi na wanafunzi wa Kishapu Sekondari kwa kushiriki kikamilifu. Licha ya mafanikio haya, tunasisitiza kuwa usafi usiwe tu wa kila mwisho wa mwezi bali uwe sehemu ya maisha ya kila siku,” amesema Kanwakabo.

Aidha, ametoa wito kwa wakazi wa Kishapu kuacha kusubiri maagizo ya viongozi ili kushiriki katika usafi, bali kujenga tabia endelevu ya kuhifadhi mazingira kwa maslahi ya pamoja.

Kwa upande wake, Mtendaji wa Mamlaka ya Mji Mdogo Kishapu, Godwin Everygist, amesema kuwa tayari mamlaka imeanza mchakato wa ujenzi wa dampo la kisasa katika eneo la Sulagi, hatua inayolenga kupunguza changamoto za utupaji holela wa taka na kukuza miji safi na salama.

Mtendaji wa Mamlaka ya Mji Mdogo Kishapu, Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga Godwin Everygist

“Katika kipindi hiki cha mpito, tunasisitiza uhifadhi sahihi wa taka kwenye dampo la muda, huku tukielekea kwenye mji wa kisasa wenye miundombinu bora ya usimamizi wa taka,” amesema Everygist.

Ameongeza kuwa ni muhimu kwa kila kaya kuhakikisha inakuwa na choo bora na salama ili kuzuia uharibifu wa mazingira na milipuko ya magonjwa yanayochochewa na uchafu.

Baadhi ya Wanafunzi kutoka Shule ya Sekondari Kishapu Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga wakifanya usafi

Zoezi la usafi wa pamoja lililofanyika Julai 26 limehusisha maeneo muhimu ikiwemo Soko la Swalala, uwanja wa Shirecu, pamoja na dampo la muda, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kujenga utamaduni wa kudumu wa usafi na kujali afya ya jamii katika Wilaya ya Kishapu.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI December 22, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI November 21, 2025
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWATAKA MADIWANI KISHAPU KUDUMISHA USHIRIKIANO NA MSHIKAMANO - NGUZO KUFANIKISHA MIPANGO YA MAENDELEO.

    December 19, 2025
  • DED JOHNSON ATOA MAELEKEZO MUHIMU KWA MADEREVA

    December 19, 2025
  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI WAMTEUA MWENYEKITI MPYA HALMASHAURI YA WILAYA KISHAPU

    December 03, 2025
  • WATUMISHI KISHAPU WAPEWA MAFUNZO YA ELIMU YA FEDHA NA KUKABILIANA NA CHANGAMOTO YA AFYA YA AKILI

    November 20, 2025
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa