• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
    • Idara
      • Fedha
      • Rasilimali watu
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
  • Nyaraka
    • Fomu za kujinga na Kidato cha Tano
      • Shule ya Sekondari Kishapu
      • Shule ya Sekondari Shinyanga
    • Mpango wa bajeti wa mwaka 2021/2022
    • Matangazo
    • Sheria ndogo ya ushuru wa huduma
    • Mifumo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
      • Uvuvi wa Samaki katika Bwawa la Songwa, Bwawa mhumbu
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Mhe. William Luhende Jijimya - Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Mhe. Francis Manyanda - Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Mhe. Joel Ndettoson - Diwani kata ya Kishapu
      • Mhe. Mohamed Aman - Diwani kata ya Ndoleleji
      • Mhe. Lucas Nkende - Diwani kata ya Mwamashele
      • Mhe. Pontias Daud - Diwani kata ya Mwataga
      • Mhe. James Kasomi - Diwani kata ya Bubiki
      • Mhe. Bushi Mpina - Diwani kata ya Mwamalasa
      • Mhe. Nyama Kisinza - Diwani kata ya Somagedi
      • Mhe. Mashini W. Washima - Diwani kata ya Uchunga
      • Mhe. Anderson Mandia - Diwani kata ya Ukenyenge
      • Mhe. Edward Manyama - Diwani kata ya Kiloleli
      • Mhe. Reuben Siyabo - Diwani kata ya Bupigi
      • Mhe. Bujiku Nyanda - Diwani kata ya Mwaweja
      • Mhe. Michael Paul - Diwani kata ya Shagihilu
      • Mhe. Luhende S. Luhende - Diwani kata ya Lagana
      • Mhe. Richard Dominico - Diwani kata ya Talaga
      • Mhe. James Kamuga - Diwani kata ya Igaga
      • Mhe. Lameck Nsubata - Diwani kata ya Itilima
      • Mhe. Mpemba Malangahe - Diwani kata ya Bunambiyu
      • Mhe. Makenzi Charles - Diwani kata ya Busangwa
      • Mhe. Nestory Kalugula - Diwani kata ya Ngofila
      • Mhe. Lwinzi Kidiga - Diwani kata ya Maganzo
      • Mhe. Samson Gelewa - Diwani kata ya Mwasubi
      • Mhe. Sarah Marco - Diwani kata ya Idukilo
      • Mhe. Enock Bundala - Diwani kata ya Masanga
      • Mhe. Thabidha Mmbando - Diwani kata ya Mwakipoya
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Mwenyekiti wa Halmashauri
  • miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
  • Kituo Cha Habari
    • maktaba ya picha
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa za Vyombo vya Habari
  • Maeneo
    • Kata
      • Orodha ya Kata
    • Tarafa
      • Orodha ya Tarafa
    • Vijiji
      • Orodha ya Vijiji

MWENGE WA UHURU 2025 WALIDHISHWA NA MIRADI YOTE KISHAPU

Posted on: August 8th, 2025


Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ndugu Ismail Ali Ussi ameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita kwa kupeleka miradi ya maendeleo inayotekelezwa Wilayani Kishapu, 

akieleza kuridhishwa na namna miradi hiyo inavyowanufaisha wananchi kwa uhalisia.


Ussi ametoa pongezi hizo leo Agosti 8, 2025, wakati wa mbio za mwenge wa uhuru Wilayani Kishapu Mkoani shinyanga ambapo amezindua, ameweka mawe ya msingi na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo.

Amesema Kishapu imekuwa mfano wa kuigwa kutokana na usimamizi mzuri wa miradi unaofanywa na viongozi wa Wilaya hiyo wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya Mhe. Peter Masindi pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu Bw. Emmanuel Johnson.

“Nimefurahishwa sana na kazi kubwa inayofanyika hapa Kishapu. Miradi yote niliyotembelea leo imetekelezwa kwa ubora, thamani ya fedha inaonekana na wananchi wameanza kunufaika moja kwa moja"ameongeza.

Aidha, amesisitiza kuwa usimamizi madhubuti kama huo unapaswa kuwa mfano kwa Halmashauri nyingine nchini, ili kuhakikisha rasilimali za umma zinatumika kikamilifu kwa maendeleo ya wananchi.

Katika ziara hiyo, Mwenge wa Uhuru umegusa miradi ya sekta ya maji,barabara,elimu,uwekezaji,afya na maendeleo ya vijana, ambapo miradi yote ilikidhi vigezo na kupita bila dosari.

Mwenge wa uhuru umekagua Kikundi cha Vijana Wachapakazi kilichopo Kata ya Songwa kinatekeleza mradi wa kilimo cha nyanya kwenye ekari tano kwa mkopo wa Shilingi 20,752,209/= kutoka asilimia 10 ya mapato ya Halmashauri, ambapo tayari wameanza kurejesha kiasi cha Shilingi milioni 5, mradi huu unalenga kuinua uchumi wa wanakikundi na jamii inayowazunguka kwa kuwapatia ajira na kuongeza kipato chao kupitia kilimo cha mbogamboga.

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe.Peter Msindi (kushoto) akikabidhiwa mwenge wa uhuru na Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Manispaa Wakili Julius Mtatiro (Kulia) Agosti 8,2025 Katika Uwanja wa Kijiji cha Seseko Kata ya Songwa Wilayani Kishapu

Mwenge huo pia umezindua na kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa ujenzi wa vyumba saba vya madarasa na matundu nane ya vyoo katika shule mpya ya sekondari ya Masagala kwa gharama ya Shilingi 196,400,000.

Lengo la mradi ni kuwasogezea wananchi wa kijiji cha Masagala huduma ya elimu karibu na makazi yao, kupunguza msongamano wa wanafunzi katika shule mama ya Maganzo, na kuboresha mazingira ya ujifunzaji kwa wanafunzi wanaotoka maeneo ya jirani.

Mwenge huo umezindua na kuweka jiwe la msingi mradi wa Maji uliotekelezwa naSerikali kupitia Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) imekamilisha ujenzi wa mradi wa maji ya Ziwa Victoria kutoka Nyenze hadi Ng’wangh’olo Wilayani Kishapu, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa dhamira ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kumtua mama ndoo kichwani.

Mradi huo umehusisha ujenzi wa tenki la maji la lita 100,000, vituo vitatu vya kuchotea maji, mtandao wa bomba wa mita 2,670, uzio na alama za bomba, kwa gharama ya Shilingi milioni 445.05 kupitia Programu ya Malipo kwa Matokeo (P for R). Mkandarasi M/s Geo–Spatial Classic Works Ltd kutoka Mwanza ndiye aliyetekeleza mradi huo chini ya usimamizi wa RUWASA Kishapu.

Mradi unatarajiwa kuwahudumia wananchi wapatao 2,345 wa kijiji cha Ng’wangh’olo na maeneo ya jirani kwa kuwapatia huduma ya maji safi na salama, kupunguza magonjwa yatokanayo na matumizi ya maji machafu, na kuwaongezea muda wa kushiriki shughuli za kijamii na kiuchumi.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru umetembelea na kuweka jiwe la msingi katika Zahanati ya Wela iliyopo Kata ya Bupigi ikiwa ni zao la jitihada za wananchi waliokuwa wakitembea zaidi ya kilomita 15 kufuata huduma za afya, ambapo mwaka 2011 walichangisha Shilingi 10,500,000/= kuanzisha ujenzi huo.

Serikali kupitia Serikali Kuu na mapato ya ndani ya Halmashauri imechangia Shilingi 75,000,000/= kukamilisha ujenzi huo unaojumuisha jengo la zahanati, vyoo matundu matano, kichomea taka na Placenta Pit.

Mradi huu wenye thamani ya Shilingi 85,500,000/= unatarajiwa kuhudumia wananchi zaidi ya 7,600 wa Kata ya Bupigi na Vijiji jirani, huku ukilenga kusogeza huduma za afya karibu na makazi ya wananchi na kupunguza vifo vya mama na mtoto.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge amepongeza mshikamano na uzalendo wa wananchi pamoja na juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuimarisha huduma za afya Vijijini.


Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2025 amekagua na kuweweka jiwe la msingi katika bweni la wasichana katika Shule ya Sekondari Mwamashele mradi ulianzishwa na wananchi mwaka 2019 kwa lengo la kuwalinda watoto wa kike dhidi ya changamoto za umbali mrefu, mimba za utotoni, unyanyasaji na utoro.

Wananchi kwa kushirikiana na wadau mbalimbali walichangisha zaidi ya Shilingi milioni 25 kuanzisha mradi huo, na Serikali kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri ilichangia zaidi ya Shilingi milioni 62 kukamilisha ujenzi.
Mradi huu wenye thamani ya Shilingi 88,105,200/= umekamilika na unawanufaisha wanafunzi wa kike 48 wanaolala katika bweni hilo hivyo watoto wa kike wamepata mazingira salama ya kusomea na kuishi shuleni, hatua inayochochea ufaulu na kuimarisha usawa wa kijinsia katika elimu.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge amepongeza mshikamano wa wananchi na uongozi wa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwekeza katika elimu ya mtoto wa kike huku akizindua klabu za kupinga Rushwa na kuzuia ukatili wa Kijinsia.

Mwenge wa Uhuru umeweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa barabara ya DED - DC yenye urefu wa kilomita 1 kwa kiwango cha lami nyepesi (DSD), mradi unaogharimu zaidi ya shilingi milioni 688. Mradi huo unatekelezwa na TARURA kwa lengo la kuboresha miundombinu ya usafiri na kuongeza ufanisi wa huduma kwa jamii.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ndugu Ismail Ali Ussi, amempongeza mwekezaji mzawa Bw. Bin Salum kwa uzalendo wake mkubwa na mchango wake katika maendeleo ya Wilaya ya Kishapu.

Amesema Bin Salum ni mfano wa kuigwa kutokana na uwekezaji mkubwa alioufanya kwa manufaa ya jamii, huku akibainisha kuwa juhudi kama hizo zinaiweka Kishapu katika nafasi ya kuwa Manispaa na hatimaye jiji katika miaka ijayo.

“Bin Salum ameonyesha moyo wa kizalendo kwa kuwekeza fedha nyingi katika miradi mbalimbali ya maendeleo. Huyu ni miongoni mwa wazawa wanaoonesha kwa vitendo kuunga mkono jitihada za Mhe. Rais katika kuwaletea wananchi maendeleo,” amesema Ussi.

Aidha, amewataka wananchi wa Kishapu kuendelea kumpa ushirikiano mwekezaji huyo na wawekezaji wengine wazawa kwa kuwa mchango wao ni muhimu katika kufanikisha ajenda ya maendeleo endelevu nchini.

Aidha, Mwenge wa Uhuru umetembelea na kuzindua Klabu ya kuzuia ukatili na Wapinga Rushwa katika Shule ya Sekondari Mwamashere, ambapo wanafunzi waliwasilisha ujumbe wa kupinga vitendo vya rushwa kwa kauli mbiu ya mwaka huu isemayo "Kuzuia Rushwa ni Jukumu Lako na Langu, Tutimize Wajibu Wetu".

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Peter Masindi(kushoto) na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu Emmanuel Johnson(Kulia)

 wakiendelea na ziara ya mwenge wa uhuru Wilayani humo Agosti 8,2025

Katika miradi yote iliyokaguliwa, kiongozi huyo wa Mwenge wa Uhuru Kitaifa amesisitiza umuhimu wa usimamizi makini wa miradi ya maendeleo, uwazi na uwajibikaji kwa manufaa ya wananchi.

Mwenge wa uhuru utakabidhiwa kesho Agosti 9,2025 na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga mhe.Mboni Mhita baada ta kumaliza ziara yake Mkoani Shinyanga katika Kijiji cha Njiapanda kwa ajili ya kuendelea na mbio zake Mkoani Simiyu. 

Matangazo

  • TAARIFA YA MTIRIRIKO WA FEDHA KWA KIPINDI KILICHOISHIA TAREHE 30 JUNE. 2022 August 14, 2023
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI November 03, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MFAMASIA December 14, 2021
  • Orodha ya Walioitwa kwenye Usaili September 20, 2024
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • JOHNSON AHAMASISHA MAPINDUZI KUWALINDA WANAWAKE NA WATOTO KISHAPU

    August 15, 2025
  • MGOMBEA UBUNGE CHAMA CHA MAKINI JIMBO LA KISHAPU ACHUKUA FOMU

    August 14, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WALIDHISHWA NA MIRADI YOTE KISHAPU

    August 08, 2025
  • KILELE CHA MAADHIMISHO WIKI YA UNYONYESHAJI KISHAPU YAFANYIKA SHAGIHILU

    August 07, 2025
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa