• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Utawala
      • Biashara, Viwanda na Uwekezaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya jamii
      • Afya
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Tehama
      • Utamaduni, Sanaa na Michezo
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Usafi wa Mazingira na Udhibiti Taka
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Kilimo na Mifugo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya kuonana na mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya picha na video za shughuli za maendeleo

PICHA UZINDUZI WA BARAZA LA MAMLAKA YA MJI MDOGO KISHAPU NA VIONGOZI WAKE

Posted on: May 11th, 2025

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Emmanuel Johnson(kushoto) Akimkabidhi kanuni za kudumu za utendaji katika Baraza hilo Mtendaji wa Baraza la Mamlaka ya Mji Mdogo Kishapu Godwin Everygist (kulia).

Baraza la Mamlaka ya Mji Mdogo Kishapu limezinduliwa rasmi Mei 6, 2025 na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Bw. Emmanuel Johnson katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali na chama.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Mhe. Willium Jijimya (kushoto)akimkabidhi kanuni za kudumu za utendaji Mwenyekiti wa Baraza la Mamlaka Mhe.Fabian Makongo (kulia).

Akizungumza katika uzinduzi huo Mkurugenzi Johnson amesema Kishapu ilitangazwa kuwa Mamlaka ya Mji Mdogo tangu mwaka 2004 lakini utekelezaji wake ulikwamishwa na changamoto za kiuchumi.

Mwakilishi wa Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Mhandisi Eugine Soka. 

Johnson amesema hatua ya sasa imewezekana kutokana na jitihada za pamoja za viongozi na wananchi waliokubali mageuzi muhimu, ikiwemo kupunguza idadi ya vitongoji.

"Serikali ya awamu ya sita chini ya Dkt Samia Suluhu inasisitiza ushirikiano,uwajibikaji na kujituma kwa maslahi ya wananchi hivyo mkafanye kazi" Ameongeza Mkurugenzi Johnson

Mwakilishi wa Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Mhandisi Eugine Soka amewapongeza kwa hatua hiyo na kusema uzalendo wa viongozi walioteuliwa ni chachu ya kuleta mabadiliko ya haraka.

Mtendaji wa Mamlaka hiyo ya Mji Mdogo Godwin Everygist, ameeleza kuwa mpango wa awali ni kuboresha miundombinu, mazingira, na usimamizi wa ujenzi unaozingatia sheria,kanuni na taratibu ili kufikia hadhi ya kuwa Halmashauri ya Mji kamili.

Mwenyekiti wa Baraza la Mamlaka ya Mji Mdogo Kishapu Mhe.Fabian Makongo(kulia) na Makamu Mwenyekiti wa Baraza hilo Dionis Makala(kushoto)

Baraza hilo lina jumla ya wajumbe 17 na linaongozwa na Mhe. Fabian Makongo (Mwenyekiti) na Mhe. Dionis Makala (Makamu Mwenyekiti).

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga Shika Ntelezu akizungumza kwenye uzinduzi wa Baraza la Mamlaka ya Mji Mdogo Kishapu. 

Mamlaka ya Mji Mdogo Kishapu sasa inaanza safari yake rasmi huku msukumo ukiwa ni kuhakikisha maendeleo yanawafikia wananchi kwa ukaribu na kwa kasi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI December 22, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI November 21, 2025
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWATAKA MADIWANI KISHAPU KUDUMISHA USHIRIKIANO NA MSHIKAMANO - NGUZO KUFANIKISHA MIPANGO YA MAENDELEO.

    December 19, 2025
  • DED JOHNSON ATOA MAELEKEZO MUHIMU KWA MADEREVA

    December 19, 2025
  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI WAMTEUA MWENYEKITI MPYA HALMASHAURI YA WILAYA KISHAPU

    December 03, 2025
  • WATUMISHI KISHAPU WAPEWA MAFUNZO YA ELIMU YA FEDHA NA KUKABILIANA NA CHANGAMOTO YA AFYA YA AKILI

    November 20, 2025
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa