• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Utawala
      • Biashara, Viwanda na Uwekezaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya jamii
      • Afya
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Tehama
      • Utamaduni, Sanaa na Michezo
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Usafi wa Mazingira na Udhibiti Taka
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Kilimo na Mifugo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya picha na video za shughuli za maendeleo

RC SHINYANGA APOKEA MWENGE WA UHURU 2025

Posted on: August 3rd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Tabora  Mhe. Paul Chacha (Kushoto) akimkabidhi hati ya makabidhiano Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe.Mboni Mohamed Mhita (Kulia)  katika Viwanja vya Stendi ya Mabasi Kagongwa Kata ya Kagongwa Wilayani Kahama Agosti 8,2025

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mohamed Mhita, leo Agosti 3, 2025, amepokea rasmi Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Paul Chacha, katika viwanja vya Stendi ya Mabasi Kagongwa, wilayani Kahama.

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Mhe Peter Masindi akiwa ameshikilia mwenge wa uhuru uliipokelewa ki Mkoa Stendi ya mabasi Kagongwa Kata ya Kagongwa Wilayani Kahama Mkoani humo kutoka Mkoa wa Tabora Agosti 8,2025

Akizungumza baada ya kupokea Mwenge huo, Mhe.Mhita amesema kuwa Mwenge wa Uhuru ukiwa Mkoani Shinyanga utakimbizwa umbali wa kilomita 819.2 katika Halmashauri sita za Mkoa huo, ambapo utapitia jumla ya miradi 44 kwa ajili ya kukagua, kuzindua na kuweka mawe ya msingi.

Katibu Tawala Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga Bi.Fatma Mohamed akisalimiana na kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru mwaka 2025 Ismail Ali Ussi katika Viwanja vya stand ya mabasi Kagongwa Kata ya Kagongwa Wilayani Kahama wakiingia Mkoani humo kutokea Mkoani Tabora Agosti 3,2025

Mhita Ameeleza kuwa thamani ya miradi hiyo ni Shilingi bilioni 17.3, ikiwa ni ishara ya juhudi za Serikali katika kuimarisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa wananchi wa mkoa wa Shinyanga.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Bw.Emmanuel Johnson akisalimiana na kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru mwaka 2025 Ismail Ali Ussi katika Viwanja vya stand ya mabasi Kagongwa Kata ya Kagongwa Wilayani Kahama wakiingia Mkoani humo kutokea Mkoani Tabora Agosti 3,2025

Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu zinakimbizwa na wakimbiza Mwenge sita wakiongozwa na kiongozi wa mbio hizo, Ismail Ali Ussi.

Kauli mbiu ya Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2025 ni "Jitokeze Kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 kwa Amani na Utulivu", ikisisitiza umuhimu wa ushiriki wa wananchi katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwaka huu kwa njia ya amani na utulivu.

Mwenge wa Uhuru unaanza mbio zake Wilayani Kahama hii Leo na unatarajiwa kukamilisha mbio zake katika Mkoa wa Shinyanga kwa Wilaya ya Kishapu na kukabidhiwa kwa Mkoa wa Simiyu Agosti 9, 2025 katika Kijiji cha Njiapanda huku mapokezi ya Wilaya ya Kishapu yatakuwa katika uwanja wa Kijiji cha Seseko na eneo la mkesha kuwa Uwanja wa Shirecu.

Mwenge huo unatarajiwa kuhamasisha mshikamano wa kitaifa, maendeleo endelevu, na ushirikiano baina ya Serikali na wananchi katika kutatua changamoto mbalimbali za kijamii.

Matangazo

  • TAARIFA YA MTIRIRIKO WA FEDHA KWA KIPINDI KILICHOISHIA TAREHE 30 JUNE. 2022 August 14, 2023
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI November 03, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MFAMASIA December 14, 2021
  • Orodha ya Walioitwa kwenye Usaili September 20, 2024
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI

    November 21, 2025
  • WATUMISHI KISHAPU WAPEWA MAFUNZO YA ELIMU YA FEDHA NA KUKABILIANA NA CHANGAMOTO YA AFYA YA AKILI

    November 20, 2025
  • DC,DED NA MSIMAMIZI WA UCHAGUZI JIMBO LA KISHAPU WAUNGANA NA WANANCHI KUPIGA KURA

    October 29, 2025
  • WASIMAMIZI WA VITUO KISHAPU WAONYWA KUTOKUWA CHANZO CHA MIGOGORO

    October 27, 2025
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa