• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Utawala
      • Biashara, Viwanda na Uwekezaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya jamii
      • Afya
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Tehama
      • Utamaduni, Sanaa na Michezo
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Usafi wa Mazingira na Udhibiti Taka
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Kilimo na Mifugo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya kuonana na mwenyekiti wa Halmashauri
    • Ratiba ya vikao vya kisheria vya MSM
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Sheria ndogo ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya picha na video za shughuli za maendeleo

RC SHINYANGA APOKEA MWENGE WA UHURU 2025

Posted on: August 3rd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Tabora  Mhe. Paul Chacha (Kushoto) akimkabidhi hati ya makabidhiano Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe.Mboni Mohamed Mhita (Kulia)  katika Viwanja vya Stendi ya Mabasi Kagongwa Kata ya Kagongwa Wilayani Kahama Agosti 8,2025

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mohamed Mhita, leo Agosti 3, 2025, amepokea rasmi Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Paul Chacha, katika viwanja vya Stendi ya Mabasi Kagongwa, wilayani Kahama.

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Mhe Peter Masindi akiwa ameshikilia mwenge wa uhuru uliipokelewa ki Mkoa Stendi ya mabasi Kagongwa Kata ya Kagongwa Wilayani Kahama Mkoani humo kutoka Mkoa wa Tabora Agosti 8,2025

Akizungumza baada ya kupokea Mwenge huo, Mhe.Mhita amesema kuwa Mwenge wa Uhuru ukiwa Mkoani Shinyanga utakimbizwa umbali wa kilomita 819.2 katika Halmashauri sita za Mkoa huo, ambapo utapitia jumla ya miradi 44 kwa ajili ya kukagua, kuzindua na kuweka mawe ya msingi.

Katibu Tawala Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga Bi.Fatma Mohamed akisalimiana na kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru mwaka 2025 Ismail Ali Ussi katika Viwanja vya stand ya mabasi Kagongwa Kata ya Kagongwa Wilayani Kahama wakiingia Mkoani humo kutokea Mkoani Tabora Agosti 3,2025

Mhita Ameeleza kuwa thamani ya miradi hiyo ni Shilingi bilioni 17.3, ikiwa ni ishara ya juhudi za Serikali katika kuimarisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa wananchi wa mkoa wa Shinyanga.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Bw.Emmanuel Johnson akisalimiana na kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru mwaka 2025 Ismail Ali Ussi katika Viwanja vya stand ya mabasi Kagongwa Kata ya Kagongwa Wilayani Kahama wakiingia Mkoani humo kutokea Mkoani Tabora Agosti 3,2025

Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu zinakimbizwa na wakimbiza Mwenge sita wakiongozwa na kiongozi wa mbio hizo, Ismail Ali Ussi.

Kauli mbiu ya Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2025 ni "Jitokeze Kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 kwa Amani na Utulivu", ikisisitiza umuhimu wa ushiriki wa wananchi katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwaka huu kwa njia ya amani na utulivu.

Mwenge wa Uhuru unaanza mbio zake Wilayani Kahama hii Leo na unatarajiwa kukamilisha mbio zake katika Mkoa wa Shinyanga kwa Wilaya ya Kishapu na kukabidhiwa kwa Mkoa wa Simiyu Agosti 9, 2025 katika Kijiji cha Njiapanda huku mapokezi ya Wilaya ya Kishapu yatakuwa katika uwanja wa Kijiji cha Seseko na eneo la mkesha kuwa Uwanja wa Shirecu.

Mwenge huo unatarajiwa kuhamasisha mshikamano wa kitaifa, maendeleo endelevu, na ushirikiano baina ya Serikali na wananchi katika kutatua changamoto mbalimbali za kijamii.

Matangazo

  • TANGAZO LA MWALIKO WA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI January 20, 2026
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI December 22, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI November 21, 2025
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • VIKUNDI 21 MAKUNDI MAALUMU VYAPATIWA MIKOPO KISHAPU

    January 29, 2026
  • BARAZA LA MADIWANI KISHAPU LAAZIMIA SOKO HURIA LA PAMBA, LATOA MSISITIZO WA LISHE NA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    January 28, 2026
  • DED KISHAPU AKABIDHI VIFAA VYA TEHAMA KUWAWEZESHA WAALIMU WENYE CHANGAMOTO YA UONI

    January 28, 2026
  • BARAZA LA MADIWANI KISHAPU LAPOKEA NA KUJADILI TAARIFA ZA KATA ROBO YA PILI 2025/2026

    January 27, 2026
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa