• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kishapu District Council
Kishapu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
    • Idara
      • Fedha
      • Rasilimali watu
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
  • Nyaraka
    • Fomu za kujinga na Kidato cha Tano
      • Shule ya Sekondari Kishapu
      • Shule ya Sekondari Shinyanga
    • Mpango wa bajeti wa mwaka 2021/2022
    • Matangazo
    • Sheria ndogo ya ushuru wa huduma
    • Mifumo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
      • Uvuvi wa Samaki katika Bwawa la Songwa, Bwawa mhumbu
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Mhe. William Luhende Jijimya - Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Mhe. Francis Manyanda - Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Mhe. Joel Ndettoson - Diwani kata ya Kishapu
      • Mhe. Mohamed Aman - Diwani kata ya Ndoleleji
      • Mhe. Lucas Nkende - Diwani kata ya Mwamashele
      • Mhe. Pontias Daud - Diwani kata ya Mwataga
      • Mhe. James Kasomi - Diwani kata ya Bubiki
      • Mhe. Bushi Mpina - Diwani kata ya Mwamalasa
      • Mhe. Nyama Kisinza - Diwani kata ya Somagedi
      • Mhe. Mashini W. Washima - Diwani kata ya Uchunga
      • Mhe. Anderson Mandia - Diwani kata ya Ukenyenge
      • Mhe. Edward Manyama - Diwani kata ya Kiloleli
      • Mhe. Reuben Siyabo - Diwani kata ya Bupigi
      • Mhe. Bujiku Nyanda - Diwani kata ya Mwaweja
      • Mhe. Michael Paul - Diwani kata ya Shagihilu
      • Mhe. Luhende S. Luhende - Diwani kata ya Lagana
      • Mhe. Richard Dominico - Diwani kata ya Talaga
      • Mhe. James Kamuga - Diwani kata ya Igaga
      • Mhe. Lameck Nsubata - Diwani kata ya Itilima
      • Mhe. Mpemba Malangahe - Diwani kata ya Bunambiyu
      • Mhe. Makenzi Charles - Diwani kata ya Busangwa
      • Mhe. Nestory Kalugula - Diwani kata ya Ngofila
      • Mhe. Lwinzi Kidiga - Diwani kata ya Maganzo
      • Mhe. Samson Gelewa - Diwani kata ya Mwasubi
      • Mhe. Sarah Marco - Diwani kata ya Idukilo
      • Mhe. Enock Bundala - Diwani kata ya Masanga
      • Mhe. Thabidha Mmbando - Diwani kata ya Mwakipoya
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Mwenyekiti wa Halmashauri
  • miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
  • Kituo Cha Habari
    • maktaba ya picha
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa za Vyombo vya Habari
  • Maeneo
    • Kata
      • Orodha ya Kata
    • Tarafa
      • Orodha ya Tarafa
    • Vijiji
      • Orodha ya Vijiji

TAKUKURU KISHAPU YAKUTANA NA WADAU KUWAPA ELIMU YA RUSHWA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025

Posted on: October 2nd, 2025

Mkuu wa TAKUKURU Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Atuganile Stephen akizunguza kwenye semina iliyohusisha Viongozi wa dini,Viongozi wa siasa na Waandishi wa Habari kuhusiana na makosa ya Rushwa kuelekea Uchaguzi Mkuu walipokuwa ofisi za Taasisi hiyo Oktoba 2,2025

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga imeendesha semina maalum kwa viongozi wa dini, viongozi wa vyama vya siasa na waandishi wa habari ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025.

Akizungumza katika kikao hicho kilichofanyika Ofisini hapo Oktoba 2,2025, Mkuu wa TAKUKURU Wilaya ya Kishapu, Atuganile Stephen, amesema lengo la semina hiyo ni kutoa elimu ya kina kuhusu makosa ya Rushwa yanayoweza kujitokeza katika kipindi cha uchaguzi na athari zake kwa jamii. 

Atuganile amebainisha kuwa Rushwa wakati wa uchaguzi siyo tu kosa la kisheria bali pia ni udhalilishaji wa haki ya msingi ya wananchi kuchagua viongozi wao kwa uhuru.

"Kila mdau ana jukumu la kuhakikisha uchaguzi unakuwa huru na wa haki bila kushawishiwa kwa Rushwa ya aina yoyote, huku akiwataka viongozi wa dini kutumia nafasi zao kuelimisha waumini kuhusu madhara ya kupokea au kutoa Rushwa huku akiwataka viongozi wa vyama vya siasa kuendesha kampeni zenye kuzingatia maadili na sheria badala ya kutumia mbinu za kifisadi kuwanunua wapiga kura.

Kwa upande wake, Afisa wa TAKUKURU Wilayani Kishapu Neema Samamba, akiwasilisha mada kuhusu makosa ya Rushwa, ameeleza kwa kina baadhi ya vitendo vinavyokatazwa kisheria ikiwemo kutumia wadhifa kushawishi uteuzi wa wagombea, mwenendo usiofaa wa Maafisa waandikishaji, makosa yanayohusu daftari na kadi za wapiga kura pamoja na ukiukaji wa taratibu za usimamizi wa uchaguzi.

Afisa wa TAKUKURU Wilayani Kishapu Neema Samamba akizunguza kwenye semina iliyohusisha Viongozi wa dini,Viongozi wa siasa na Waandishi wa Habari kuhusiana na makosa ya Rushwa kuelekea Uchaguzi Mkuu walipokuwa ofisi za Taasisi hiyo Oktoba 2,2025

“Lengo la kuwaelezea haya yote ni kutokana na umuhimu wenu kwa jamii na jinsi mnavyoaminika na watu mnaowaongoza, ili muwe mabalozi wa kutoa elimu hii kwa wananchi. Ni wajibu wenu kuhakikisha kila mmoja anafahamu makosa ya Rushwa pamoja na adhabu zilizowekwa chini ya Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Namba 1 ya mwaka 2024,” amesisitiza Samamba.

Semina hiyo imepokelewa kwa hamasa kubwa na washiriki ambapo viongozi wa dini wameahidi kuwa mabalozi wa maadili mema kwa waumini wao, viongozi wa vyama vya siasa wakiahidi kuzingatia sheria na maadili wakati wa kampeni, huku waandishi wa habari wakiahidi kuendelea kuelimisha wananchi kupitia uandishi unaozingatia ukweli na uwajibikaji.

Katika kuhitimisha kikao hicho, washiriki wamekubaliana kwa pamoja kuwa mapambano dhidi ya Rushwa ni jukumu la kila mmoja, na kwamba mafunzo hayo yatawasaidia kuhakikisha Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 unafanyika kwa haki, uwazi na amani.

Matangazo

  • TAARIFA YA MTIRIRIKO WA FEDHA KWA KIPINDI KILICHOISHIA TAREHE 30 JUNE. 2022 August 14, 2023
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI November 03, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MFAMASIA December 14, 2021
  • Orodha ya Walioitwa kwenye Usaili September 20, 2024
  • Tazama yote

Habari Mpya

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI

    November 21, 2025
  • WATUMISHI KISHAPU WAPEWA MAFUNZO YA ELIMU YA FEDHA NA KUKABILIANA NA CHANGAMOTO YA AFYA YA AKILI

    November 20, 2025
  • DC,DED NA MSIMAMIZI WA UCHAGUZI JIMBO LA KISHAPU WAUNGANA NA WANANCHI KUPIGA KURA

    October 29, 2025
  • WASIMAMIZI WA VITUO KISHAPU WAONYWA KUTOKUWA CHANZO CHA MIGOGORO

    October 27, 2025
  • Tazama yote

Video

EGA ANNOUNCIMENT
Video zaidi

Viunganishi cha Haraka

  • fomu mbalimbali
  • Dira na Dhima ya Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu
  • Tovuti ya Idara ya Habari Maelezo

Watazamaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kishapu

    Anwani ya Posta: S.L.P. 1288 KISHAPU

    Simu ya mezani: +255282770020

    Simu: +255282770020

    Barua pepe: info@kishapudc.go.tz/ded.kishapudc@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki © 2016 Halmashauri ya wilaya ya Kishapu. Haki zote zimehifadhiwa